MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA
MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE
MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA
MASOMO
Somo I: Acts 2:1-11
Somo II: 1Cor
12:3b-7, 12-13
Injili: John/Jean 20:19-23
SALA: Ee Mungu Baba
Mwenyezi, kwa ushirika wa Yesu Mkombozi wetu na kwa uwepo na nguvu ya Roho
Mtakatifu, Kanisa lako lilitakatifuzwa, basi ee Baba tunakuomba, utusaidie sisi
viungo vya Kanisa lako kusudi tubaki waaminifu kwa kulishika Neno na Amri yako.
Uwatakase na kuwalinda Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amen.
UTANGULIZI
Taifa la Mungu, SHALOOM: wapendwa leo tunao furaha ya
kuhitimisha mahadhisho ya sherehe ya Pasaka ambalo kiliturgia leo tunahesabu
siku 50 tangu tulipoanza kusherekea mafumbo ya wokovu wetu yaani: Kuteswa,
Kufa, Kufufuka na Kupaa Mbinguni Bwana wetu Yesu: Ndio sababu leo ni Sherehe ya
Pentekoste maana yake ni “siku ya hamsini”.(50th) Ni
siku ya hamsini tangu tulipo sherehekea Jumapili ya Pasaka yaani Jumapili ya
Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo: Basi kwa namna ya pekee Katika Sherehe tunakumbuka
kwanza ujio wa Roho Mtakatifu kwa Mitume, tunakumbuka kuzaliwa kwa Kanisa na
mwanzo wa utume wa Kanisa. Na pili, Mama Kanisa uweka Sherehe hii kuwa Sherehe
ya waamini walei wote.(feast of lay people or la fête des laics) Kwa hiyo,
tukiwa na dhamira hiyo tutafakari kuusu Roho Mtakatifu Katika Maisha yetu na
Katika Kanisa letu.
UFAFANUZI
Wapendwa katika Kristo, wengi kati yetu uwa najiuliza kila mwaka kwa nini sherehe ya Pentecoste? neno Pentecoste limetoka wapi na asili yake ni nini ? na ni kwa
sababu gani Kanisa letu usherekeya siku hiyo kama Mwanzo wa Kanisa na ujio wa
Roho Mtakatifu? Bila shaka tunasehemu mbili ambao inatupa ufafanuzi wa matukio
kama haya katika safari ya imani na wokovu wetu : Sehemu ya kwanza bila
shaka ni Biblia Takatifu na sehemu ya pili ni historia ambao ufasiria vizuri
maisha fulani ya watu fulani, na kwa namna ya pekee kuusu swali letu ni historia
ya wana teule wa Mungu yaani wa Israeli. Wapendwa katika
Kristo, basi mimi leo napenda kuchukua sehemu ya kwanza ambao ni Biblia kusudi
niwaelekeze kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu limbuko, asili ya sherehe hii ya
Pentecoste.
Kwanza nivizuri
kutambuwa kwamba sherehe ya Pentecoste inatoka kwa Mungu wetu Mwenyewe wala sio
kwa maneno ya wanadamu. Tukisoma kitabu cha MAMBO YA WALAWI(Leviticus au Levitique) sura ya 23 tutaona
wazi namna gani Mungu kupitia Musa, anawapa wana wa Israeli sikukuu za israeli
ambalo ni sikukuu zake Mwenyewe : Tusome Walawi sura 23 :1-2 : Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, nena na wana wa
Israeli, na kuwaambia, sikukuu za Bwana, ambazo mtazipigia mbiu kuwa ni
makusanyiko matakatifu, hizi ni sikukuu zangu. Kwa hiyo ukiendelea
kusoma mustari ama verset ile ya 3 hadi ile ya 44 utakuta sikukuu mbali mbali za
Mungu ambalo huwapa wana wa Israeli kuwa sikukuu muhimu kabisa katika maisha
yoa : ni kama vile sabato(Walawi 23,3-4), Pasaka ya Mkate usiotiwa chachu (Walawi
23,5-8), Mganda wa Malimbuko(Walawi 23,9-14), siku ya kwanza kisha mwezi wa
saba(Walawi 23,23-25), siku ya Upatanisho(Walawi 23,26-32), sikukuu ya vibanda(Walawi
23,33-44) na sikukuu ya majuma ambao ni sikukuu ya Pentecoste ya wayahudi.(Walawi
23,15-22)
Maana yake,
sikukuu ya Petencoste kwanza asili yake nikutoka kwa wayahudi ambao waliomriwa
kuhadhimisha sikukuu hiyi(soma Waliwa 23, 15-22) siku 50 baada ya pasaka ya
Kiyahudi ambamo kwa wayahudi Pentecoste ao sikukuu ya majuma ao ya
Mavuno : ni siku ya Kumshukuru Mungu kwa kutoa sadaka ya mavuno yao,
vifugo vyao na vitu vingine kwa ukumbusho wa ukombozi wao ambao ufamika kama
pasaka ya kwanza yaani pasaka ya
Kiyahudi. Katika sherehe hiyo wayahudi uwa natoka sehemu ao nchi tafouti (wakiongea
lugha mbali mbali ambao walijiufunza huko waliko toka) na kuelekea Hekaluni Yerusalemu kusudi kumpa Mungu shukrani…
Basi kwa kifupi : Pentecoste (ilikuwa) ni sikukuu ya
wakulima ambao baada ya kuvuna mazao yao ya kwanza, walimshukuru Mungu kwa yale
waliyojaliwa na papo hapo kumwomba awajalie tena mavuno mema msimu ufuatao.
Ndiyo maana iliitwa sikukuu ya mavuno. Iliitwa pia sikukuu ya majuma kwa vile
ilisherehekewa majuma machache tu baada ya pasaka ya Wayahudi. Hivyo ina maana
kwamba Sherehe hii ilianza baada ya kuwekwa rasmi tarehe maalumu ya Pasaka ya
Wayahudi, kwani wahusika wa Sherehe hii walikuwa ni Wayahudi au Waisraeli. Kadiri ya muda
ulivyoendelea, polepole sherehe ya Pentekoste ilipata maana mpya ambayo ni ya
kidini. Waisraeli walianza kuadhimisha sherehe ya Pentekoste kama ukumbusho wa
siku Musa alipopewa amri kumi za Mungu mlimani Sinai. Ni siku hiyo ambapo Taifa
la Israeli lilizaliwa kwa kupewa kanuni rasmi za kuwaongoza, yaani Amri za
Mungu. Sherehe hiyo sasa ilichukua sura mpya ikiwakumbusha tukio kubwa
na la maana sana kwao yaani kuzaliwa kwa Taifa lao la Israeli. (tusome Kutoka 19)
Sasa
tukiwa na picha ya sherehi ya kiyahudi na baada ya kuelewa maana halisi ya sikukuu ya Pentecoste ya
wayahudi basi tutaelewa pia mahadhimisho ya sikukuu hii ya leo kwetu sisi
wakristu. Kwa hiyo mama Kanisa kupitia mafundisho ya mtaguso wake wa Pili ama
council Vatican II utufundisha kwamba: Kila wakati
na katika kila taifa mtu amchaye Mungu na kutenda haki hukubaliwa na yeye (tusome Acts10, 35). Lakini ilimpendeza Mungu kuwatakatifuza na kuwaokoa watu, siyo
mmoja mmoja na pasipo muunguno kati yao, bali kwa kuwaunda kama taifa moja,
lenye kumjua katika ukweli na kumtumikia kitakatifu. Kwa hiyo alijichagulia
watu wa Israeli kuwa taifa lake, akafunga agano na taifa hilo, akalifundisha
polepole kwa kujidhihirisha katika historia yake yeye mwenyewe na kufunulia kusudio la mapenzi yakke, naye akaliweka
wakfu(consacré au consecrated) kwa ajili yake. Lakini hayo yote yalitokea kama
matayarisho na mfano wa lile agano lililo jipya na kamilifu ambalo lilitakiwa
kufungwa katika Kristo, na wa ule ufunuo mtimilifu wa kuletwa na Neno wa Mungu
mwenyewe aliyejifanya mwili… (haya mafundisho
tunayapata katika Konstitusio ya Kidogma juu ya Fumbo la Kanisa ukurasa wa 9)
Kumbe
sasa sherehe ya Pentecoste ya wakristu ni bila shaka ukumbusho wa siku 50 baada
ya kukombelewa na Yesu kutoka utumwa wa dhambi a mauti na pia kukusanya naye kwa
upewa wa nguvu ya Roho Mtakatifu kuwa Taifa mpya yaani Kanisa ambao Kristo
Mwenyewe ni Kichwa cha Kanisa hilo mpya. Ndio sababu mafundisho ya Kanisa
hutuimiza ya kuwa: Pale ilipotimilika kazi Baba
aliyomkabidhi Mwana afanye duniani (tusome Yohane 17,4), basi Roho Mtakatifu
akatumwa siku ya Pentecoste ili kulitakatifuza Kanisa siku hadi siku, na
waamini wapate njia ya kumkaribia Baba kwa Kristo katika Roho mmoja( somo Eph
au Waefeso 2,18). Huyu ndiye Roho wa uzima au chemchemi ya maji yabubujikiayo
uzima wa milele.(tusome Yohane 4,14 pia 7, 38-39). (haya mafundisho
tunayapata katika Konstitusio ya Kidogma juu ya Fumbo la Kanisa ukurasa wa 4)
Ndio
maana wapendwa, masomo yetu yote 3 ya leo utuonesha wazi Mwanzo wa Kanisa na
Kazi ya Roho Mtakatifu kaitka kulitakatifuza Kanisa hilo na waamini wake wote
siku hadi siku. Wengi wanaweza sasa kujiuliza: Kanisa lilianza siku gani
au lini? Rasmi, tunaweza kusema kwamba Siku ya Pentecoste ni siku ya kuzaliwa
kwa Kanisa yaani Taifa mpya ya Mungu: lakini nivizuri kufahamu kwamba Bwana
Yesu alianzisha Kanisa lake kwa kuihubiri habari njema, yaani ujio wa ufalme wa
Mungu, ulioahidiwa tangu karne nyingi katika maandiko: “Wakati umetimia, na
ufalme wa Mungu umekaribia, tubuni na kuiamini Injili” ( tusome Marc 1,15 na
Mathew 4,17). Basi ufalme huo unang’aa wazi mbele ya watu katika Neno la
Kristo, katika matendo yake na uwepo wake.
Kwa hiyo upewa wa Roho Mtakatifu sio mwanzo wa maisha
mpya au maisha nyingine ya wokovu wetu. Apana. Lakini ni mwendelezo ya
Mafundisho ya Yesu ambao aliwafundisha wale Mitume wake( na wafuasi wengine)
ambao waliochaguliwa naye Yesu Mwenyewe kwa ajili ya uwenjilisaji wa Injili
takatifu na ufalme wa Mungu dunia Kote.( tusome Mathew/Mathayo 28, 18-20). Kwa
hiyo, Roho Mtakatifu ni mmoja katika ya zile nafsi tatu za Utatu Mtakatifu ambao katika
umoja wao uendelea kulitakatifuza Kanisa na waamini wake siku hadi siku. Ndio
maana Kanisa inatufundisha kama ifatavyo: Mwana wa
Mungu, katika hali ya kibinadamu aliyofungamana nayo aliposhinda mauti kwa kifo
na ufufuko wake, alimkomboa mwanadamu, akamgeuza kuwa kiumbe kipya.(tusome Gal.
6,15 na 2Cor. 5, 17). Maana kwa kuwashirikisha Roho wake, anawafanya ndungu
zake waitwao kutoka katika mataifa yote kuwa mwili wake katika fumbo...
(haya mafundisho tunayapata katika Konstitusio ya Kidogma juu ya Fumbo la
Kanisa ukurasa wa 7)
Ndio sababu Injili yetu inatuonesha wazi kazi na Nguvu ya
Mungu Roho Mtakatifu katika maisha ya Mitume na wafuasi wa kwanza wa Yesu pia
katika maisha yangu na wewe leo. Mitume ambao walikuwa wakishikwa na hofu kubwa
na manunguniko baada ya kifo cha Yesu Mwalimu na Kiongozi wao basi ikawa jioni,
siku ile ya kwanza ya juma, pale walipokuwapo wanafunzi, milango imefungwa kwa
hofu ya wayahudi, akaja Yesu kuwapa amani na baadae akawaonyesha mikono yake na
ubavu wake. Basi wale wanafunzi wakafurahi walipomwona Bwana: akawavuvia,
akawaambia, pokeeni Roho Mtakatifu kama ishara ya kuwapa tena uzima yaani uhai
na nguvu ya kubaki imara katika kuamini kwao. Pia akawapa mamlaka ya
kuwaondolea watu dhambi yaani hapa tunaona mwanzo wa sakramenti ya Kitubio....
Katika somo la kwanza kutoka katika Matendo ya Mitume sura
2:1-11 tunasikia simulizi vile vile ya ujio wa Roho Mtakatifu kwa Mitume na
wafuasi wengeni. Yaani ilikua katika hali hiyo ya sherehe na kusanyiko la
mkutano huo mkubwa siku ya Pentecoste ya Kiyahudi, Mitume kwa hofu ya Wayahudi walikuwa wamejifungia
katika chumba, wakidumu katika kusali, wakisubiri ahadi ya Kristo, yaani ujio
wa Roho Mtakatifu. Humo
ndani ghafla kukaja upepo toka mbinguni,ukaijaza nyumba ile, zikatokea ndimi za
moto zilizogawanyika zikiwakalia kila mmoja. Wote wakajawa Roho Mtakatifu, wakapata
ujasiri wakatoka nje, wakaenda hekaluni kwenye kusanyiko wakaanza kuhubiri kwa
nguvu habari za Yesu Kristo. Jambo la ajabu wanapata pia kipaji cha
kuongea lugha geni. Kwa kuwa siku hiyo kwa sababu ilikuwa sherehe ya Pentecoste
ya kiyahudi, wayahudi walitoka sehemu mbalimbali za dunia na kuelekea
Yerusalemu kama desturi yao kwa ajili ya kusherekea pamoja, huku walijiufunza
lugha mbalimbali lakini cha kushangazwa wakati Mitume baada ya kupokea Roho
Mtakatifu walinena katika lugha mbalimbali nao walishangaa sana kuwaona Mitume
wakiongea lugha ambazo zi na husiana na mataifa nyingine... lakini wote
walikuwa kakielewana.
Basi wapendwa leo Kwetu sisi kwa ubatizo wetu tulipewa
Roho Mtakatifu na katika sakramenti ya Kipaimara(confirmation) tunaimarishwa na
Roho Mtakatifu na kutufanya kuwa askari hodari wa Kristo na wa Injili takatifu.
Kwa hiyo Roho Mtakatifu ni Mungu kwetu ambaye anastahili sifa na shukrani
kutoka kwetu. Akuna mwanadamu ambaye anaweza leo kujidai kuwagawiya wenzake
wanadamu Roho Mtakatifu kama vile tunavyo sikia leo katika mafundisho
mbalimbali katika dunia yetu ya leo. Basi ndugu zangu, ukisha batizwa basi
tambuwa kwamba umebatizwa katika Kristo na Katika Roho Mtakatifu basi hauna
tena budi ya kutafuta kupewa kwa namna ya pekee Roho Mtakatifu lakini ukiishi
katika uaminifu na ukimwomba Mungu kwa msaada wa Roho Mtakatifu wewe utapewa paji
ao vipaji vya Roho ambao vitakusaidia kadiri ya uwezo wako kumtangaza Kristo na
Injili yake ya ufalme wa Mungu.
Leo hii tunaangaika kwa sababu ya upungufu wa imani ambao
umatufanya tutafute ishara, maarifu ao miujiza kusudi tutambuwe kwamba Roho
huyu yupo kati yetu...hii ni imani usio na msingi wa Kristo imani ya kidunia
ambao utupotesha wengi leo. Leo hii kwa jina la Roho Mtakatifu viongozi
mbalimbali ya dini wanagawanyika hadi kuwatenga kondoo wa Mungu, kuharibu
familia mbalimbali licha tu ya utabiri ambao hauwendani na mafundisho ya Roho
huyu mabaye kwetu sisi ni Roho wa haki, ukweli, umoja na uzima. Basi kila mmoja
wetu lazima afanye utafiti wa imani yake na kijipima kwamba kweli ndani mwaka
Roho huyu anafanya kazi. Kila mmoja nivizuri ajiulize kwamba kweli ndani mwake
anao vipaji vya Roho Mtakatifu ambao vinaweza kuwasaidia wengini kumfuata
Kristo.
Ndio maana katika somo la 3 litokalo katika waraka wa
kwanza wa Mtume Paulo kwa Wakorinto sura 12: 3-7, 12-13 utukumbusha wazi
kwamba: hatuwezi kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu. Ingawa
kunatofauti ya karama, bali Roho ni yeye yule. Tena pana tofauti za kutenda
kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. Lakini kila
mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana... kwa maana katika Roho mmoja sisi
sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu wayahudi, au kwamba tu wayunani,
ikiwa tu watumwa au tu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja. Paulo
aliwakumbusha jumuiya ya Korinto na kutukumbusha leo kwamba sio vizuri
kujisifia kwa mimi nilipewa vipaji muhimu kuliko wenzetu bali kujikweza na
kufahamu kwa yote tunaoyatenda leo ni kazi yake Mungu ambao hutenda kupitia hekima ,akili, shauri, nguvu, elimu, ibada na uchaji kwa Mungu.Karama zingine ni kama vile unabii,Uponyaji,
ualimu, kunena kwa lugha na nyingine nyingi ndani yetu
basi sisi ni vyombo tu ambamo Mungu mwenyewe hutenda ishara yake. Basi tuwe
wakweli na wanyenyekevu, tusiwadanganye wenzetu kwa kulitumia vibaya jina la
Mungu Roho Mtakatifu.
Hivyo basi, yatupasa kutambua karama hizo zote ni mali
yake Mungu. Leo hii kutokana na matatizo yatuzungukayo baadhi ya waamini wa
Madhehebu mbalimbali, hata ndani ya Kanisa letu wanaonekana kukazia zaidi
karama mbili tu yaani uponyaji na kunena kwa lugha. Roho
Mtakatifu si fukara(poor au pauvre) wa vipaji,anavyo vingi sana kama vile hekima, akili,
shauri, nguvu, elimu, ibada na uchaji kwa Mungu. Vipaji hivyo na vingine vingi
ambavyo hatujavitaja vipo kwa ajili ya kuhudumiana na kujengana, yaani kwa
lugha nyepesi ni kufaidiana sisi wenyewe. Yatupasa kuvitambua vipaji hivyo
vyote kuwa ni kazi ya Roho Mtakatifu. Tukumbuke kuwa imani inayotegemea miujiza
tu haina nguvu, tena ni imani isiyo ya kweli. Aidha, kuna hatari kubwa ya
kuingiza utapeli katika ile tudhaniyo kuwa ni miujiza. Vipaji tulivyonavyo viwe
kwa manufaa ya wote. Na tujue kuwa karama kubwa
kuliko zote ni upendo.
Na kazia tena nakusema: tunasherehekea ujio wa Roho
Mtakatifu; siku ya Pentekoste, ambapo Roho Mtakatifu alionekana kuwashukia
Mitume. Tusidhani kuwa Roho Mtakatifu alianza kuwepo siku ya Pentecoste: APANA! Yeye ni Mungu nafsi ya tatu ya Utatu Mtakatifu, hana mwanzo wala mwisho, ila tu
siku ya Pentekoste alijidhihirisha kwa namna ya pekee. Tangu hapo yeye ni
kiongozi wa kanisa kama vile ilivyokuwa amri za Mungu kwa taifa la Israeli.
Wote wanaoshukiwa nae hujazwa mapaji yake saba ili tutende kazi ya Mungu.
Hivyo, Roho Mtakatifu, ndiye anayeliongoza kanisa kuwachagua viongozi wa kanisa,
kuwapeleka anakopenda wakafanye utume wao, anawajalia hekima katika utume na
kuwasaidia katika maamuzi, anawasaidia wahubiri wa Injili kuhubiri vema, na
kuongoza usomaji wa Maandiko Matakatifu.Tena Roho Mtakatifu huwajalia watu
vipaji mbalimbali kwa ajili ya kanisa lote na kwa ajili ya wanakanisa wote,kwa
ajili ya wokovu wa wote na kwa ajili ya sifa na utukufu wa Mungu.
Kwa
hiyo wapendwa katika Kristo, sisi leo tuzingatiye mambo muhimu mbili tunapo
sherekeya siku hii ya Petencoste: kwanza tukumbuke
kuwa Roho Mtakatifu anakuja bado kwetu katika sakramenti ya Ubatizo na
Kipa-imara(confirmation). Roho huyo hutujalia vipaji mbalimbali. Tuzikimbilie
sakramenti hizo na tutumie vema vipaji vyetu tulivyojaliwa na Roho Mtakatifu
kwa ajili ya kufaidiana: kwa hiyo tusiwe na majivuno kwa sababu ya vipaji tulio
pewa, tuheshimu vipaji vya wenzetu pia tusiwe na vivu mbaya kwa vipaji vya
wenzetu sisi sote tulipewa vipaja tofauti kwajili ya kazi Ya Mungu sio kwa ajili ya kazi yetu. Pili, tudumishe
umoja katika kanisa, sio sisi na Yesu Kristo tu bali hata sisi kwa sisi.
Muujiza wa Pentekoste ulirudisha umoja uliopotea huko kati ya mataifa: Muujiza
huu uwe mfano wa utume wetu katika dunia yote bila ubaguzi wa rangi, jinsia,
kabila, utaifa, ukanda, ujimbo etc., ili watu wote wapate kulisikia Neno la
Mungu, ili wapate kuliishi na kuokoka: kama wabatizwa yatupasa kuongea lugha
moja tu, lugha ya upendo kwa wote, lugha ambayo hakuna asiyeielewa. Upendo
haufifii kamwe kwani wadumu mpaka Mbinguni. Ni fadhila ya Kimungu iliyotofauti
na nyingine kwani mwisho wake si hapa Duniani.
SHALOOM: MUNGU AWABARIKI
KILA SIKU YA MAISHA YENU
SHEMASI BIENVENU KABEYA
NGUNGWA KUNGWA POULAIN LOQUACE, SDS
Commentaires