MAHUBIRI YA SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTO: MWAKA A WA KANISA 2020


MAHUBIRI YA SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTO: MWAKA A WA KANISA 2020
MASOMO
SOMO I: Deut.8: 2-4, 14-16a
SOMO II: 1Cor.1: 16-17
INJILI: John/Jean 6: 51-58
SALA: Tumuombe Mungu, kusudi kwa Mwili na Damu Takatifu ya Bwana Wetu Yesu Kristo Mwanaye Mpendwa, Mungu na Mwokozi wetu na kwa utakaso wa Roho Mtakatifu, mimi na wewe leo tutambuwe upendo utakalo kwa Ekaristi Takatifu katika jumuiya yetu, Maisha na familia zetu pia katika nchi na taifa zetu. 
UTANGULIZI
Wapendwa, baada ya kusherekeya sherehe ya Utatu Mtakatifu Dominika iliopita yaani tulisherekeya Umoja na Upendo usiogawanyika katika Mungu Mmoja, leo tena kwa namna ya pekee tunasherekeya sherehe ya Mwili na Damu Takatifu ya Bwana wetu Yesu Kristo: Maana yake leo tunataka kumshukuru tena Mungu kwa ajili ya upendo wake kwetu kupitia kazi yake ya uumbaji na wokovu wetu. Tukiwa na dhamira hiyo tumuombe Mungu atusaidia tutambuwe uwepo wa Yesu Kristo kila siku katika adhimisho ya Ekaristi kama kielelezo cha umoja na upenda kati yetu na Mungu pia kati yetu sisi kwa sisi wanadamu.
UFAFANUZI
Wapendwa Taifa la Mungu: SHALOOM / TUMSIFU YESU KRISTO: Wapendwa tunaweza kujiuliza kwa nini leo tunasherekeya tena sherehe ya Mwili na Damu Takatifu ya Bwana Wetu Yesu Kristo wakati Alhamisi Kuu (Jeudi Saint) tulisherekeya kuwekwa rasmi kwa sakramenti Ekaristi pia sakramenti ya Upadre? Wapendwa jibu ni kwamba, Alhamisi Kuu, ni kweli tulisherekeya kuwekwa rasmi kwa sakramenti ya Ekaristi na Bwana wetu Yesu Kristu na pia kuwekwa rasmi kwa sakramenti ya Upadirisho. Kwa hiyo Kanisa utufundisha kwamba: Mwokozi wetu, katika karamu ya mwisho, usiku alipotolewa, aliweka sadaka ya Ekaristi ya Mwili wake na Damu yake. Alifanya hivyo ili kuendeleza sadaka ya msalaba siku zote mpaka atakaporudi, kusudi amwachie Bibiarusi Mpendwa yaani Kanisa, ukumbusho wa kifo chake na ufufuko wake: Sakramenti Takatifu, ishara ya Umoja na kifungo cha Upendo.
Lakini leo kwa namna ya pekee baada ya kusherekeya mafumbo ya wokovu wetu yaani Pasaka: tunaadhimisha sherehe hii kwanza kama shukrani kwa Utatu Mtakatifu kwa kuwa kwa njia ya Mateso, Kifo na Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo ulimwengu mzima ulikombolewa na binadamu kupewa tena neema ya kushiriki katika upendo na umoja wa Mungu. Pili Kanisa katika sherehe hii utupa tena nafasi ya kutafakari nguvu na umuhimu wa Ekaristi Takatifu katika Maisha yetu ya Imani na wokovu. Tatu sherehe hii utukumbusha mafundisho ifatavyo kuusu Ekaristi Takatifu: Mosi Ekaristi Takatifu hukamilisha kuingizwa katika ukristo. Wale walioinuliwa katika heshima ya ukohani wa kifalme kwa Ubatizo na kufananishwa kwa ndani Zaidi na Kristo kwa Kipaimara, hushiriki Pamoja na jumuiya yote katika sadaka moja ya Bwana. Pili Ekaristi ni chemchemi na kilele cha Maisha yote ya Kikristo. Sakramenti nyingine, kama zilivyo pia huduma zote za kanisa na kazi za utume, zaungana na Ekaristi na zaelekezwa kwake. Kwani katika Ekaristi Takatifu mna kila hazina ya kiroho ya kanisa, yaani Kristo Mwenyewe, Pasaka wetu. Tatu Ekaristi ndio ishara thabiti na sababu ya hali ya juu kabisa ya ushirika katika uzima wa kimungu na umoja ule wa taifa la Mungu ambao unalifanya Kanisa liwepo. Maana yake Ekaristi ni kilele cha tendo la Mungu la kuutakatifuza ulimwengu katika Kristo, na kilele cha tendo la kumwabudu Mungu wampalo watu Kristo, na kwa njia yake wampalo Baba katika Roho Mtakatifu. Mwishowe, kwa njia ya adhimisho la Ekaristi tunaungana tayari sisi wenyewe na liturjia ya mbinguni na tunaanza kutangulia kushiriki uzima wa milele Mungu atakapokuwa yote katika wote.
Basi wependwa tunao sababu ya kutosha kusudi leo kwa namna ya pekee tutafakari kuusu Ekaristi ambao kwetu sisi leo ni shukrani kwa Mungu ambaye yupo nasi kila siku asa pale ambapo tunashiriki katika Misa Takatifu. Ndio maana masomo yote tatu ya leo utualika kutambuwa Mwili na Damu Takatifu ya Bwana wetu Yesu Kristo kama mafumbo ya wokovu na Imani Yetu. Katika agano la Kale mkate na divai vilitolewa sadaka kati ya mazao ya kwanza ya nchi, ishara ya kumkiri Muumba. Lakini vinapata pia maana mpya katika tendo lote la Kutoka yaani ukombozi wa israeli kutoka utumwani Misri: mikate isiyotiwa chachu ambayo Israeli hula kila mwaka wakati wa Pasaka hukumbusha ukombozi wao kwamba aliishi kwa mkate wa neno la Mungu.(Rejea Deut.8:3) Ndio maana katika somo la kwanza, Musa aliwaambia makutano: utaikumbuka njia ile yote ya Bwana, Mungu wako, aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwani… akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyaijua wewe wala baba zako hawakuijua, apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu bali huishi kwa kila litakalo katika kinywa cha Bwana.
Wapendwa Neno la Mungu ni Kristo ambaye katika Injili ujidhihirisha kwa wayahudi na kwetu leo nakusema: Mimi ni Chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni, mtu akila Chakula hiki, ataishi milele…. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake… Basi wapendwa atuna budi kutafuta neema apa na pale, yatupasa kutambua kwamba Ekaristi ni Yesu Mwenyewe. Na kila mara Padre anapo adhimisha misa ni Yesu Mwenyewe anaadhimisha, ni Yesu Mwenyewe hutoa neema na nguvu za kutuwezesha kuishi Imani yetu. Sasa wakati unapoanza kujitenga kushiriki Ekaristi ao unaposhiriki Ekaristi bila Imani na kwa mazoea tambuwa kwamba ni mwanzo wa mateso na maanguko yako. Sasa wewe na mimi leo tutambuwe kwamba Ekaristi ni Shukrani pia ni sala na kilele cha sala zote. Hakuna njia nyingine ya kukutana na Mungu yenye undani na ukuu zaidi isipokuwa Ekaristi Takatifu ndio maana Yesu anasema: Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba, kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi.
Tena Kanisa inatufundisha kwamba kwa njia ya Liturjia, hasa sadaka takatifu ya Ekaristi, latimizwa tendo la ukombozi wetu. Liturjia inasaidia kikamilifu waamini waonyeshe katika maisha yao na kuwadhirishia wengine fumbo la Kristo na pia maumbile halisi ya Kanisa la kweli. Kusudi kutimiza tendo kubwa namna hii, Kristo yupo daima katika Kanisa lake, kwa jinssi ya pekee katika maadimisho ya kiliturjia. Yupo kwenye Sadaka ya Misa katika nafsi ya Kasisi, Yeye ambaye, akijitoa mara moja msalabani, anajitoa tena mwenyewe kwa huduma ya mapadre. Yupo hasa chini ya maumbo ya Ekaristi. Baasi wapendwa, Kama Ekaristi ni Karamu basi inatupasa kabla ya kesherekeya karamu hiyo fufanya matayarisho ao maandalizi ya kiroho na kimwili kusudi tujaliwe neema itakalo kwa Kristo Kohani Mkuu. Tuwe katika hali gani tunapoijongea meza ya Bwana? Leo hii tuna kumbushwa kuwa tunapo ijongea meza ya Bwana, tuijongee tukiwa katika mapenzi mema. Yaani tusiijongee kwasababu ya mazoea, majivuno, wala kwa kuwapendeza watu, bali kwa nia ya kumpendeza Kristo, kuunganika naye na kupata dawa ya kuushinda udhaifu. Kusudi tuhudumishe upendo na umoja kati yetu na Mungu na pia kati yetu sisi kwa sisi kama wakristo. Kupokea Ekaristi kwasababu ya mazoea, majivuno, kujionyesha ni kufuru kwa Ekaristi Takatifu. Kupokea Ekaristi ukijua kuwa unadhambi ya mauti moyoni ni kufuru.
Basi tunaposherekea sherehe Ekaristi Takatifu tunakumbushwa kuwa sisi sote tumealikwa kushiriki Ekaristi Takatifu ambayo Bwana wetu Yesu Kristu anasema kuwa ni mwili wake na damu yake. Chakula hiki kinatolewa kwa ajili yetu kinatupatia uzima wa milele. Kwa hiyo kila mmoja wet ni mshiriki wa sherehe hii: kwa kusoma, kuimba, kiitikia wakati unatuhusu kutikia na kukaa kimia wakati tunaitajika kukaa kimia: basi wapendwa yatupasa kufanya mandalizi kabla ya kuja kushiriki katika Karamu hii ya wokovu wetu: tambua kuwa unaposoma ni Kristo Mwenyewe anasema kupitia wewe, mtu anapobatiza, ni Kristo mwenyewe anayebatiza, wakati padre anaadhimisha Misa ni Kristo mwenyewe alie Kohani Mkuu huadhimisha misa kupitia padre basi maandalizi ni ya muhimu sana kwa kuboresha misa na liturijia nzima ya Kanisa letu. Ndio maana Paulo katika somo la pili utuonesha wazi kwaamba: kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja. Basi tumwombe Mwenyezi Mungu atujalie kwa njia ya Mwanaye Yesu Kristo Bwana na Mwokozi wetu na katika Umoja wa Roho Mtakatifu tujaliwe neema na baraka katika sherehe hii ya leo.

SHALOOM
SHEMASI BIENVENU KABEYA NGUNGWA KUNGWA POULAIN LOQUACE, SDS

Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA