MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA


MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA
MASOMO
Somo I: Ex. 34: 4b-6, 8-9
Somo II: 2Cor. 13: 11-14
Injili: John/Jean 3: 16-18

SALA: Ee Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja, mwenye Upendo na Uzima, tunakuja mbele yako leo kukusifu na kukushukuru kwa ajili ya Uwepo wako katika Maisha yetu, basi tunakuomba uwajalie upendo, amani na masikilizano familia zote, ndoa zote na jamii zote ambayo zinaishi katika shida, vita, ungovi, wivu, migogoro na ubaguzi…tunaomba hayo kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao anayeishi na kutawala  nawe na Roho Mtakatifu, Mungu daima na milele. Amen.
UTANGULIZI
Wapendwa Taifa la Mungu: SHALOOM. Baada ya kusherekeya msimu mzima ya mafumbo ya wokovu wetu yaani Pasaka na pia baada ya kupokea Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste, leo Mama Kanisa utupa nafasi ya kumtukuza na kumshukuru Mungu ambaye kwa imani yetu ni Mmoja katika Nafsi Tatu. Sherehe ya Utatu Mtakatifu kwetu sisi wakristu ni kiini cha imani yetu na inachukua nafasi ya pekee katika historia ya uumbaji na wokovu wa ulimwengu mzima ambaye ulijengwa katika Neema yaani Upendo wa Mungu kwetu sisi. Basi tunao sababu ya kumpa Mungu sifa ambaye ni Mmoja katika Nafsi Tatu(3). Tumwombe Mungu atupe Uwezo katika adhimisho ya siku ya leo kusudi tuweze kutambuwa mafumbo matakatifu ya imani na matumaini yetu. Pia tuwaombea wote ambao kwa namna moja ao nyingine ushindwa kuelewa na kusadiki mafundisho ya Mama yetu Kanisa ili Mungu  awaongoze katika fikra zao kusudi waweze kuonja upendo na umoja wa Mungu katika maisha yao.
UFAFANUZI
Bila shaka Sherehe ya leo uwa nawapa watu wengi changamoto kwanza kwa kuelewa na pili kwa kutowa ufafanuzi sahihi ambayo unaweza kufasiria wazi izi Nafsi tatu katika Mungu Mmoja. Wengine kwa sababu ya mchanganiko wa makanisa na dini, wanashawishika na kuhisi kwamba sisi wakatoliki tunaabudu miungu mitatu(3). Jibu ni kwamba APANA. Sisi kama wakristu wakatoliki tunakiri imani kwa Mungu Mmoja TU katika Nafsi Tatu: Umoja usiopimika wa nafsi hizi utuonesha wazi UMOJA NA UPENDO wa Mungu wetu. Basi kwa uweza wa Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu, nakwalika wewe ambaye utasoma homelia hii ujaliwe faraja, amani na baraka katika maisha yako ya imani, familia yako, kazi na shuguli zako mbalimbali kusudi kwa msaada wa Mungu Mmoja ujaliwe neema ya kuelewa vizuri mafumbo haya matakatifu ya imani yetu.
Wapendwa katika Barua ya Mtakatifu Paulo Mtume kwa Warumi(Romain) sura(chapitre) ya 10: 17-18 tunasoma kamaifatavyo: Basi imani, chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo. Lakini nasema: Je, wao hawakusikia? Naam, wamesikia, sauti yao imeenea dunia mwote, na maneno yao na fahamu nitawaghadhibisha. Wapendwa Paulo Mtume anatufunza kwamba imani yetu chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa neno la Kristo: maana yake bila kusikiliza neno la Kristo sisi leo atuwezi kushuhudia Uzima, Upendo na Huruma wa Utatu Mtakatifu kwetu. Kila mmoja wetu lazima aipe neno la Mungu nafasi katika maisha yake kusudi aweze kupewa neema ya kuimarisha imani yake. Tutambuwe kwamba wengi kati yetu uwa najiuliza kuwa Utatu Mtakatifu unamsingi gani katika Biblia? Tunaweza kupata ufafanuzi wa kibiblia ambao unaweza kutusaidia kuelewa huyu Utatu Mtakatifu? Na kwa nini Utatu Mtakatifu? Kabla ya kujibu maswali hizi, lazima kufahamu kwamba Utatu Mtakatifu ni Fumbo la imani. Ndio maana Waebrania(Hebreux) sura(chapitre) ya 11: 1 usema hivi: Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyookekana. Kwa hiyo tunaitaji ufunuo zaidi wa Mungu Mwenyewe kusudi tuweze kuelewa mafumbo yake. 
Kwanza katika lugha ya Agano la Kale(Ancien Testament), inafamika kuwa Mungu yaani Yahweh ni Mmoja na wa Upekee Kabisa. Tusome Kitabu cha Kumbukumbu la Torati(ama Deutéronome) 6: 4: Sikia, ee Israeli: Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye Mmoja. Ni Mungu wenye Wivu wala hakubali miungu mingine. Tusome kitabu cha Kutoka(Exode) 20: 3-5: Usiwe na miungu mingine ila mimi. Usifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini dunia, wala kilicho majini chini ya dunia. usivisujudie wala kuvitumikia. Kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye Wivu... Basi wapendwa, tukibaki katika mtazamo ma maneno haya tunaweza kusema kuwa neno Utatu Mtakatifu aipo katika Agano la Kale. Lakini tukiendelea kusoma Biblia yaani Agano la Kale tutaona kwamba licha neno Utatu Mtakatifu aipo katika Agano la Kale lakini mawazo ambao yanaweza kutoa ufafanuzi wa neno Utatu Mtakatifu yapo. Ndio maana Kanisa katoliki lina tumia Biblia, Mapokeo( Tradition) na Viongozi wake(Papa na Maaskofu wezanke) kwa kuimarisha imani ya waamini. Basi wa baba wa kanisa katika Mapokeo (ya kanisa) walitafsiri baadhi ya vipengele vya Agano la Kale na kuunda wazo kuusu Utatu Mtakatifu ambao ni kiini cha imani yetu sisi wakristu. Kwanza walitambuwa kwamba kuna baadhi ya vipengele vya Agano la Kale ambao vinaonesha wazi Mungu akiongea katika UWINGI: kwa hiyo wakatoa wazo kwamba katika Mungu kuna nafsi zaidi ya Mmoja:
Basi tusome Kitabu Cha Mwanzo(Genesis) 1: 26: Mungu akasema, “Natufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu... tena katika Gen.3: 22 tunasoma hivyo: Bwana Mungu akasema, “Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya, na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele.” Tena ukiendelea kusoma Gen.11: 6-7 utasikia kama ifatavyo: Bwana akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja, na hayo ndiyo wanayoanza kuyafanya, wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya. Haya, na tushuke huko, tuwachufulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao. Pia katika kitabu cha nabii Isaya 6: 8 utupa pia ufafanuzi: Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, “Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?” Ndipo niliposema, “Mimi hapa, nitume mimi.” Basi wapendwa hizi ni baadhi(yaani versets ni nyingi) ya vipengele katika Agano la Kale ambao utupa picture ya wazo la Utatu Mtakatifu. 
Pili katika mafundisho ya Kanisa letu utimilifu wa Agano la Kale ni Agano Jipya.(Nouveau Testament). Ndio maana Katika Agano Jipya tunao sababu ya kutosha kuusu wazo la Utatu Mtakatifu. Agano Jipya utufundisha wazi habari ya Yesu Kristo ambaye ufunua katika kazi, matendo na maisha yake Mungu Baba na Mungu Roho Mtakatifu. Kristo anakuwa kwetu kio ambao tunaona Umoja na Upendo wa Mungu katika Nafsi Tatu(3). Biblia yaani Agano Jipya ujaa na mawazo ya Utatu Mtakatifu. Kwanza tukianza na Injili ya Mathayo3: 13-17, Marko1: 9-11 na Luka3: 21-22 tunaona Ubatizo wa Yesu ambao umetupa ufunuo wa Utatu Mtakatifu: Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka, Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua, sauti ikatoka mbinguni, “Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu, nimependezwa nawe. 
Na katika ushuhuda wa Utatu Mtakatifu katika injili hizi tatu( synoptic) upo zaidi katika Injili ya Mathayo 28: 19: ambao tulipewa siku ya Kupaa(Ascension) Yesu mbinguni mamlaka ya kuwabatiza watu wote katika Utatu Mtakatifu: Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jila la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu. Basi wapendwa katika injili hizi tatu sakramenti ya Ubatizo utuonesha wazi Ufunuo wa wokovu wetu ambao unaanza kwa kuzaliwa mara ya pili katika maisha yetu. Kwa hiyo Utatu Mtakatifu ni Uzima na kwa sakramenti ya ubatizo mimi na wewe tulipewa Uzima wa Mungu. Ndio maana Yesu alimwambia Nicodemo: “Amin, amin, nakuambia: mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.”(Jean/John3: 5) Lakini, Injili ya Mtume Yohane utuonesha zaidi kuusu Utatu Mtakatifu. Mwanzoni kabisa wa Injili hii tunaona wazo kuusu Utatu Mtakatifu. Ndio maana katika sura ya 1 hadi ile ya 12, Yohane utuonesha wazi usiano wa Mungu Mwana na Mungu Baba. Na katika sehemu ya pili ya injili hii yaani kuanzia sura ya 13-17, Yohane ufasiria wazi ujio wa Roho Mtakatifu.(Jn14: 16) ambaye ametoka kwa Baba. (Jn15: 26), anatumwa na Yesu Kristo(Jn16: 7) ambaye Kazi yake ni kutufundisha yote, na kutukumbusha yote tulioambiwa na Yesu. (Jn14: 26). Ni Roho wa Ukweli ambaye anakuja kumshuhudia Kristo.( Jn15: 26 na 16: 13). Kwa hiyo Yohane 14: 26 kwa kifupi utupa picture kamili ya Mungu Roho Mtakatifu: Lakini ni huyu Mzaidizi, huyu Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote nilivyowaambia.
Tena sura ya 17 ya Injili ya Yohane utuonesha utukufu wa Baba na Mwana. Na utukufu huyu ni wokovu ambao Yohane ufundisha kama Uzima. Ndio Yohane 17: 3 utufundisha kama ifatavyo: Na uzima wa milele ndio huu: wakujuwe wewe, Mungu wa pekee wa Kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. Basi wapendwa Katika Injili ya Yohane tunafunzwa kuwa Utatu Mtakatifu ni Upokeayaji wa Uzima katika Maisha Yetu. Kwa hiyo Uzima wetu upo katika kumjuwa Yesu ambaye ni Uzima kwa sababu Uzima wake umetoka katika Uzima, Mungu katika Mungu, Mwanga katika Mwanga. (Jn17: 7). Na hio uonesha Upendo na Umoja wa Utatu Mtakatifu Kwetu. Ndio maana katika waraka wa Kwanza wa Yohane 4: 2: katika hili mwamjua Roho wa Mungu: kila Roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. Pia katika 1Jn5: 8 tunasoma: kwa maana wako watatu washuhudiao: Roho, na Maji na Damu, na watatu hawa hupatana kwa habari moja
Basi Yohane utuonesha wazi kwamba Nafsi hizi tatu katika Mungu Mmoja hufanya kazi pamoja na katika upendo usiopimika ao kutenganishwa na mtu yeyote. Kwa hiyo Utatu Mtakaatifu ni mfano wa Upendo, Umoja na Masikilizano usiokuwa na mipika katika ulimwengu wetu. Na hio ndio Sakramenti ya Eukaristi ambayo kwetu sisi ni Alama ya Upendo na Umoja wa Mungu kwetu: Mungu kwa upendo wake umtowa Mwanae Mpendwa kuwa sadaka ya wokovu wetu kusudi tusafishwe na kurudishwa katika umoja wa kimungu. Ndio maana Paulo anakasia na kuonesha Upendo huo kwetu katika waraka wake kwa Wagalatia 4: 4: Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria, kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate hali ya kuwa wana.( Tusome pia Rom1: 3-7, Rom8: 3-17, 1Cor12: 4-6, 1Cor8: 2, 2Cor3: 17, Col 2: 9...) 
Basi wapendwa, Paulo pia utufunza wazi katika Barua zaka kwamba Utatu Mtakatifu, kwanza unaonesha kazi ya Mungu katika historia ya wokovu ya Mwanadamu na pili mwendelezo wa kazi hii ya wokovu wa Mungu katika Kanisa letu Katoliki la Mitume ambalo msingi wake ni Utatu Mtakatifu. Ndio maana 1Cor 12: 4-6 utujuza hivi: Basi pana tofauti za Karama, bali Roho ni yeye yule. Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.  Basi wapendwa kwa kumailzia, Mitume katika kitabu cha Matendo ya Mitume, utuonesha wazi kwamba Utatu Mtakatifu ndio msingi wa Mahubiri yao.(Acts2: 14-36ff) ambao katika kitabu cha Ufunuo wa Yohane ama Apocalypse tunakiri kwamba Mungu ana mwanzo wala Mwisho: Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi. (Apocalypse1:8) 
Tunajifunza nini katika Biblia na Mapokeo ya Kanisa?
Kwanza tutambuwe kuwa, tunapo sherekeya Utatu Mtakatifu, tunasherekeya Utukufu, Upendo na Umoja wa Mungu katika kazi yake ya Uumbaji na wokovu ambaye Yesu Kristo ni kio, ni Njia, Uzima na Ukweli kwani kupitia Yeye Ulimwengu mzima hushuhudia kazi hio ya Utatu Mtakatifu. Pili Utatu Mtakatifu ni kielelezo kwetu cha Uzima, ambao tunashirikishwa na Yesu kwa Nguvu ya Roho Mtakatifu katika upokeaji wa Sakramenti ya Ubatizo ambao mimi na wewe tulipewa nafasi ya kushiriki tena pamoja Na Mungu na kuonja tena Neema yake. Tatu Utatu Mtakatifu ni kielelezo cha Upendo-Umoja, wa kimungu katika Maisha, familia, shughulu, wokovu wetu(Maisha yetu nzima), ambao katika sakramenti ya Eukaristi tunafundishwa kupendana kama vile Kristo alivyo tupenda, kuishi umoja kama vile Kristo uwa katika Umoja na Baba na Roho Mtakatifu. Basi wapendwa kwa kubatiwza kwetu na kwa ushiriki wetu katika meza ya Bwana, sisi kama wakristu tunapewa Uzima wa milele na Upendo ambao utokalo kwa Utatu Mtakatifu. Kwa hio katika Sakramenti hizi tunaonja kazi ya Utatu Mtakatifu katika Maisha yetu. Ndio maana Juma ijao tutasherekeya sherehe ya MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTO.
Tufanye nini kusudi Tushiriki katika Uzima, Umoja na Upendo huo wa Utatu Mtakatifu? Jibu lipo katika masomo yetu ya leo: Masomo yetu ya leo usisitizia zaidi kuusu neno UPENDO, neno UMOJA, neno AMANI. Katika somo la kwanza katika kitabu cha Kutoka 34 Musa anakutana na Mungu, na katika tokeo la Bwana, Musa alitakaswa na akalitangaza jina la Bwana... pia Musa anatambuwa kuwa watu aliopewa na Mungu wa na shingo ngumu kwa hiyo Musa anamwomba Mungu aende kati yao, awasamehe uovu na dhambi zao kusudi wakuwe warithi wa Mungu. Wapendwa, ni wangapi leo wanamwomba Mungu kusudi awasamehe wale ambao kwa namna moja ao nyingine wamepotea kiimani licha tu ya maisha magumu, shida, njaa, umaskini, kutopata ndoa, watoto, kazi, amani... Musa utufundisha leo kupitia wana wa Israeli kwamba hata sisi leo tunaishi katika shingo ngumu, tunamioyo migumu kwa hiyo tumwombe Mungu aliye Upendo, Uzima, Amani kusudi tupate faraja na neema ya kuitwa wana wa Mungu.
Ndio maana katika Injili Yesu anamwambia Nicodemo kwamba Mungu ni Upendo na Kwa Upendo huo alimtuma Yeye kusudi alinusuru ulimwangu lakini sio kulihukumu. Yesu anataka kutuambia leo kwamba, tusiwe sababu ya kutoa hukumu kwa wezentu kwa ajili ya maisha yao: tupo wengi ambao tunaona tu mabaya na matatizo ya wenzetu huku tukijifanya kuwa watangazaji wa maisha ya wenzetu popote tulipo. Yesu anakwambia leo: tangaza neno la Mungu, neno la upendo, amani na umoja kwa watu, kwa wezentu, majirani... kusudi wapate kuonja upendo na uzima wa Utatu Mtakatifu, pia tuwe mfano bora wa Uzima na Upendo huo, tusiwe chanzo cha kukatisha wengine tamaa ya kumfuate Yesu. Basi tutafanya haya yote kama tu tunaishi katika upendo, amani, umoja, tukifarijiana, tukisalimiana kwa busu takatifu na mwishoni neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu na ushiriki wa Roho Mtakatifu utakaa ndani yetu nyote. Huu ni ujumbe mahususi ambao tunaoupata katika somo la pili.(2Cor. 13: 11-41)
Wapendwa, Yesu kupitia Mtume Paulo utusihi tuzingatie sifa hizo kusudi tupate neema ya Utatu Mtakatifu. Wewe baba, wewe mama leo unaisha katika kuzingatia sifa hizo ndani ya familia yako? Kama sivyo, kwa nini? Mbona unamdanganya mpezi wako na kuishi maisha isio ya ukweli mbele yake? Leo hii ndoa mbali mbali zinapata changamoto nyingi licha tu ya kutokuwa waaminifu katika mambo madogo madogo, waaminifu katika agano letu ya ndoa: na madhara ya hizo tabia mbaya ni ugonvi, talaka, migogoro, utekelezaji wa watoto katika ulimwengu wetu wa kisasa...uzima, upendo na umoja ambao tunashirikishwa na Utata Mtakatifu katika sakramenti ya Ubatizo na Ekerasti vipo wapi? Tupo wengi leo katika kazi zetu tunashindwa kuonesha umoja na upendo sababu tu wale ambao tunafanya nao kazi sio wa kabila letu, sio wa province ama mkoa wetu, sio ndungu zetu... madhara ya tabia kama hizo mbaya ni ubakuguzi, ukabila na unyanyazaji katika maisha yetu ya kibinadamu... leo hii kuna baadhi ya watoto ambao wanashindwa kuwaheshimu wazazi wao kwa sababu ni maskini na sio wasomi... tambuwa kwamba Mzazi anabaki kuwa mzazi wala hauwezi kubadilishwa, wala upendo wake kwako hawezi pimika kwa sababu ya umaskini: madhara ya hizi tabia ni kupiga wazazi, kuwashika uchawi, na kugawanyana katika familia... kwa kifupi familia zetu zote zinaishi katika shida kubwa kwa sababu ya kutokuwa na upendo, amani na umoja... Basi wapendwa tunapo sherekeya sherehe ya Utatu Mtakatifu tujifunze kuishi Umoja na Upendo ambao utuonesha asili ya Mungu kwetu ambaye ni Mmoja katika Nafsi Tatu.

SHALOOM: MUNGU AWABARIKI KATIKA MAISHA, KAZI NA FAMILIA ZENU

SHEMASI BIENVENU KABEYA NGUNGWA KUNGWA POULAIN LOQUACE, SDS

Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA