MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA MASOMO Somo I : Acts 2:1-11 Somo II: 1Cor 12:3b-7, 12-13 Injili: John/Jean 20:19-23 SALA: Ee Mungu Baba Mwenyezi, kwa ushirika wa Yesu Mkombozi wetu na kwa uwepo na nguvu ya Roho Mtakatifu, Kanisa lako lilitakatifuzwa, basi ee Baba tunakuomba, utusaidie sisi viungo vya Kanisa lako kusudi tubaki waaminifu kwa kulishika Neno na Amri yako. Uwatakase na kuwalinda Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amen. UTANGULIZI Taifa la Mungu, SHALOOM: wapendwa leo tunao furaha ya kuhitimisha mahadhisho ya sherehe ya Pasaka ambalo kiliturgia leo tunahesabu siku 50 tangu tulipoanza kusherekea mafumbo ya wokovu wetu yaani: Kuteswa, Kufa, Kufufuka na Kupaa Mbinguni Bwana wetu Yesu: Ndio sababu leo ni Sherehe ya Pentekoste maana yake ni “ siku ya hamsini ”.(50 th ) Ni siku ya hamsini tangu tulipo sherehekea Jumapili ya Pasaka yaani Jumapili ya Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo: B...
MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA MASOMO Somo I: Ex. 34: 4b-6, 8-9 Somo II: 2Cor. 13: 11-14 Injili: John/Jean 3: 16-18 SALA: Ee Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja, mwenye Upendo na Uzima, tunakuja mbele yako leo kukusifu na kukushukuru kwa ajili ya Uwepo wako katika Maisha yetu, basi tunakuomba uwajalie upendo, amani na masikilizano familia zote, ndoa zote na jamii zote ambayo zinaishi katika shida, vita, ungovi, wivu, migogoro na ubaguzi…tunaomba hayo kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao anayeishi na kutawala nawe na Roho Mtakatifu, Mungu daima na milele. Amen. UTANGULIZI Wapendwa Taifa la Mungu: SHALOOM . Baada ya kusherekeya msimu mzima ya mafumbo ya wokovu wetu yaani Pasaka na pia baada ya kupokea Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste, leo Mama Kanisa utupa nafasi ya kumtukuza na kumshukuru Mungu ambaye kwa imani yetu ni Mmoja katika ...
MAHUBIRI YA SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTO: MWAKA A WA KANISA 2020 MASOMO SOMO I : Deut.8: 2-4, 14-16a SOMO II : 1Cor.1: 16-17 INJILI : John/Jean 6: 51-58 SALA : Tumuombe Mungu, kusudi kwa Mwili na Damu Takatifu ya Bwana Wetu Yesu Kristo Mwanaye Mpendwa, Mungu na Mwokozi wetu na kwa utakaso wa Roho Mtakatifu, mimi na wewe leo tutambuwe upendo utakalo kwa Ekaristi Takatifu katika jumuiya yetu, Maisha na familia zetu pia katika nchi na taifa zetu. UTANGULIZI Wapendwa, baada ya kusherekeya sherehe ya Utatu Mtakatifu Dominika iliopita yaani tulisherekeya Umoja na Upendo usiogawanyika katika Mungu Mmoja, leo tena kwa namna ya pekee tunasherekeya sherehe ya Mwili na Damu Takatifu ya Bwana wetu Yesu Kristo: Maana yake leo tunataka kumshukuru tena Mungu kwa ajili ya upendo wake kwetu kupitia kazi yake ya uumbaji na wokovu wetu. Tukiwa na dhamira hiyo tumuombe Mungu atusaidia tutambuwe uwepo wa Yesu Kristo kila siku katika adhimisho...
Commentaires