MAHUBIRI YA DOMINIKA YA 13 YA MWAKA A WA KANISA WAKATI WA KAWAIDA: UKARIMU WAKO UTAKUFANYA WEWE UZIDI KUBARIKIWA NA MUNGU

MAHUBIRI YA DOMINIKA YA 13 YA MWAKA A WA KANISA WAKATI WA KAWAIDA:  UKARIMU WAKO UTAKUFANYA WEWE UZIDI KUBARIKIWA NA MUNGU
MASOMO
SOMO I: 1Fal. 4:8-11, 14-16
SOMO II: 2Rom: 6:3-4, 8-11
INJILI: Mt. 10:37-42
SALA: Ee Baba yetu Mwema, ulituumba kwa sura na mfano wako kusudi tushiriki katika upendo na utukufu wako pia Mwanao Yesu Kristo Mungu na Mkombozi wetu kwa kufa na kufufuka kwake sisi tulijaliwa maisha mapya ambao kwa nguvu na msaada wa Roho Mtakatifu Kanisa inaendelea kuwakirimia watoto wake kwa njia ya sakramenti na huduma mbali mbali. Basi Ee Mungu wetu utusaidie kwanza kukupenda Wewe na Yesu Kristu kusudi tujifunze kuboresha upendo huu katika familia, taifa na dunia nzima hasa zaidi wakati huu ambao tunapambana na janga hii ya vimelea vya Corona. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amen.
UTANGULIZI
Wapendwa Taifa la Mungu SHALOOM, TUMSIFU YESU KRISTO: leo tunaadhimisha Dominika ya 13 ya Mwaka A wa Kanisa (Kanisa letu Katoliki) katika kipindi cha kawaida. Katika Dominika hii ya leo: Yesu anatukumbusha kwamba bila Yeye katika maisha yetu sisi hatuwezi kupata mafanyikiyo na Ufalme wa Mbinguni. Yohane 17: 3 utufundisha kwamba: na uzima wa milele ndio huu: wakujue Wewe, Mungu wa pekee wa Kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Na pili Dominika ya leo inatufundisha pia bila Ukarimu katika maisha yetu ni vigumu sana kuona baraka na utukufu wa Mungu. Basi ndugu yangu, Yesu anakuambia leo kwamba Yeye Mtendaji na Mzimamizi katika Maisha yako kuliko wanadamu na vitu unavyo: tambuwa kwamba wazazi, marafiki, mali ao utajiri, elimu, maisha na uzima... unavyo ni mali yake Mungu basi umpe kwanza Mungu nafasi ya kwanza katika maisha nawe utashuhudia mkono wake wa baraka katika familia, shughuli, kazi, urafiki... wako. Basi leo kila mmoja wetu amwambiye Yesu aje apenye moyo wake kusudi tutambuwe udhaifu wetu ili tuchukue hatua ya kumfuata kwa ukweli kila siku ya maisha yetu.
UFAFANUZI WA MASOMO YETU
Wapendwa katika KATEKESIMU ya Kanisa letu Katoliki tunafundishwa kwamba Ndoa ambao inatunga familia asili yake ni Mungu Mwenyewe(Gen. 1:28): kwa hiyo Baba na mama huanzisha kwa makubaliano yao jumuiya ao familia mpya katika mapenzi yake Mungu. Kwa hiyo mapendo ya mume na mke na uzazi wa watoto huanzisha kati ya watu wa familia moja uhusiano wa pekee na uwajibikaji wa kwanza. Basi Mungu kwa kuwaumba mwanamume na mwanamke alianzisha familia ya kibinadamu na kuijalia katiba yake ya msingi. Wanafamilia hawa ni binadamu walio na hadhi sawa. Basi familia ya kikristo kwanza ni chembe ya kwanza ya maisha ya jamii: ni familia ya imani, ya ukarimu, ya matumaini, ya upendo. Pia ni umoja wa watu ishara ya umoja wa umoja wa Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Tena kwa kazi ya uzazi na malezi ya watoto hunurisha kazi ya Baba ya uumbaji. Kwa hiyo familia yaitwa kushiriki sala na sadaka ya Kristo, upendo na ukarimu wa Kristo, huruma na neno la Kristo kusudi huimarisha upendo ndani yake na ndani ya ulimwengu mzima. Na ni kwa mawazo haya tunaweza kuelewa maandiko yetu ya leo hususani injili Takatifu.
Ndio maana katika somo la kwanza kutoka kitabu cha 2 cha Wafalme utuonya kwamba kwa ukarimu na upendo wao, nabii Elisha anawabariki wanandao wawili ambao walikuwa tayari na umri mkubwa bila kupata uzazi ao watoto na anawahidia mtoto. Baraka ya familia hii inatoka kwa ukarimu wa mama huo na usikivu wa mume wake: mama huu alitambuwa kwamba nabii Elisha ametoka nchi ya mbali na hakuwa na nyumba wala ndugu ao familia kule endako mama huo anamkaribisha na kumuhudumia kama mmoja wao. Pia katika kitabu cha Mwanzo sura 18: 1-15: Abrahamu kwa ukarimu wake anahaidiwa mtoto pamoja na mke wake Sara ambao tayari walikua wakongwe kabisa. Basi wewe ambaye utasoma mahubiri hii tambuwa kwamba familia yako ni baraka na inatoka kwa Mungu kwa hiyo umpe Yesu kwanza nafasi ya kuitawala na kuwa msingi wa maisha yako, maisha yetu mtakirimiwa baraka na utukufu. Wewe mama, wewe baba wakati mnapokea wageni mnafanya nini? Mnajisikiaje? Ni nani mgeni? Waswahili usema kwamba mgeni kila siku ni baraka.
Lakini leo tukichunguza kwa undani kabisa ndoa ao familia nyingi zinabomoka licha tu ya kuhabudu chakula: kuna baadhi ya akina mama ambao wanashindwa kutambuwa ndugu wa waume zao kwa sababu tu ya uchoyo, ubinafsi, tamaa na ubaguzi... wakitazama chakula kama kitu cha muhimu kuliko hata Yule ambaye anayewajalia uzima, chakula na nguvu. Maana wakiwaona wageni wanashikwa na hasira na chuki hadi kutenda matendo ambao kijumwiya hairusiwi kama kubadilisha maji ya ugali na kuyafanya kuwa maji ya kuwaogesha watoto ambao tayari walikua wamesha kuoga na wasafi licha tu kutokuwa na ukarimu... kutumia lugha chafu na kushuhudia uwongo, kupiga watoto na matusi licha tu mgeni atambuwe kwamba hapa nilipo hakuna amani ili ajiandae kuondoka...  Wengi ni akina baba ambao ushindwa kujitambuwa mbele ya chakula na kutambuwa kazi yao kama baba ndani ya familia na kuifanya familia yao kama sehemu ya utumwa, mateso na shida: baba anahesabu vipande vya samaki wengine wanajua kabisa kuku anavipande vingapi ao kuwapimia wake zao kila siku kiasi cha unga, mafuta na kazalika... hayo yote inawafanya akina mama kushindwa kumiliki ofisi yao kama mama na kuona mateso ya kuweza kushiriki maisha ya ndoa...
Basi somo hili ni mfano kwangu mimi na wewe wanandoa hawa wawe kwetu fundisho na nabii Elisha anawakilisha Mitume, mimi na wewe na viongozi wetu wote wa dini ambao Yesu katika injili utualika kwanza kumpenda Yeye kuliko vitu vyote. Tukiwa na Yesu maisha na ndoa zetu zitaneemeka na kustawi katika amani, ukarimu, furaha na uvumilivu. Kumpenda Yesu kuliko vitu vyote ni kuwa tayari kusaidiani sisi kwa sisi hasa zaidi kuwajali wale ambao ni wadogo kabisa katika jamii yetu kama vile maskini, wangonjwa hususani wakati huu wa Corona wengi kati yetu wanashindwa kuendelea na shughuli zao na kupambana na mateso, magumu makali, yatima, wajane na wengine wote ambao kwa mtazamo wetu tunawaona kama waitaji. Haya ndio mafundisho ya Yesu. Maana imani yetu na matendo lazima viendane. Ndio maana mtume Yakobo katika waraka wake sura 1: 14-18: imani bila matendo imekufa. Kwa imani na matendo ya wanandoa hawa katika somo la kwanza, Mungu anawapa furaha ambao ilikuwa itaji katika maisha yao yaani kupata mtoto. 
Basi nakwambia leo: usisema kwamba wakati umeisha na kukataa tamaa na kuhisi kwamba wewe hauwezi kubarikiwa katika ndoa yako na kupata watoto, kuolewa ao kufanyikiwa kimaisha... tambuwa kwamba Yesu Kristo ndiye Ngao na Mwokozi wako, wangu, wetu: wewe unaitajika kufanya jitihada na kutafiti maisha yako ya kimwili na kiroho kusudi Yesu Kristo apate nafasi ya kupenya moyo ao mioyo yetu tukifanya hyvio tutabarikiwa.... hauwezi barikiwa wakati wewe unazuia wengine kupata baraka, wakati unashindwa kuwasaidia wengine... kila mmoja wetu anao chochote cha kutoa basi uwe baraka kwa familia yako, kanisa lako, rafiki zako na uwe tayari kuwaombea wengine wapata kubarikiwa. Basi tukifanya hivyo tutaelewa mafundisho ya Paulo Mtume katika somo letu la pili: Hamfahamu ya kuwa sisi sote tulibatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?... Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye... Basi mkristu ni yule ambaye hutoa uhai, maisha na uzima wake kwa ajili ya wangine. Mungu azidi kuwabariki na kuwapigania kila siku katika familia na ulimwengu wetu huo.

SHALOOM/TUMSIFU YESU KRISTO
SHEMASI BIENVENU KABEYA NGUNGWA KUNGWA POULAIN LOQUACE, SDS       

Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA