DOMINIKA YA KWANZA YA KWARESIMA MWAKA A WA KANISA: TUMTEGEMEE MUNGU TUNAPOPATWA NA VISHAWISHI

JUMAPILI YA I YA KWARESIMA MWAKA A: MARCH 1th 2020
Masomo:
Somo  I:  Mwa 2:7-9, 3:1-7
Somo II: Rum 5:12-19
Injili :     Mt 4:1-11
Utangulizi
Tupo katika kipindi cha Kwaresima, na  leo ni Dominika ya kwanza ya Kwaresima katika Mwaka A wa Kanisa. Kwa hiyo mandiko matakatifu inatufundisha kwamba ni lazima kumtegemea Mungu asa zaidi wakati tunapopatwa na vishawishi.
 

Wapendwa kabla ya kutoa tafakari ya dominika ya kwanza ya kwaresima ni lazima tukumbushane kuusu maana ya kwaresima katika kanisa letu katoliki takatifu. Basi tukiungana na baba Mtakatifu papa Fransisco katika waraka wake wa kwaresima wa  mwaka huu aliendika hivi... yani nitafasiria kwa kifupi tu: papa anakabizi kwanza kwaresima ya mwaka huu juu la ulinzi na maombezi ya mama yetu Bikira Maria mama wa Mungu kusudi kwa mfano na maombezi yake kila mja kati yetu apokee wito wa Mungu ili aungane zaidi na Mungu. Pili kwaresima ni lazima itusaidie kutafakari kwa kina fumbo nzima ya ukombozi wetu tuliopewa kwa upendo wa Utatu Mtakatifu kwanzia tendo ya uumbaji hadi ukombozi wetu kwa njia ya Yesu Kristo katika ushirika wa Mungu Baba na Mungu Roho Mtatakatifu.
Basi wapendwa ni lazima tutambue kwamba ujumbe mku wa kwaresima ni kumtafuta Mungu zaidi kusudi ili kwa kuwaudumia wenzetu  na kuwajalia maskini na wanyonge katika sala, kufunga na kwa kutenda matendo ya huruma tupatanishwe na Mungu na kanisa lake nzima. Ndio sababu papa wetu anatualika tusome na kutafakari ujumbe tunao upata katika waraka wa 2 wa mt. Paulo kwa Wakorinto sura ya 5:20-21: Basi tu wajumbe kwa ajili ya Kristo, kana kwamba Mungu anasihi kwa vinywa Vyetu; twawaomba ninyi kwa ajili ya Kristo: Mpatanishwe na Mungu. Yeye asiye jua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi kuwa haki ya Mungu katika yeye.
Wapendwa tukiwa na lengo hili katika mioyo yetu basi tutatambua kwamba Kwaresima ni kipindi cha siku arobaini za kufunga, kusali, kutafakari Neno la Mungu na kufanya matendo ya huruma. Bwana wetu Yesu Kristo kabla ya kuanza rasmi kazi yake ya kuutangaza Ufalme wa Mungu hapa Duniani alifunga kwa muda wa siku arobaini.  Baada ya mfungo huo, Bwana wetu Yesu Kristo alishawishiwa/alijaribiwa na ibilisi lakini alibaki kuwa mwaminifu kwa Mungu Baba yake. Tofauti na Wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Eva walioshawishiwa na ibilisi wakaanguka dhambini. Sisi nasi tunakutana na vishawishi mbalimbali katika maisha yetu basi tukiwa na Yesu kila siku ya maisha yetu tutashinda vishawishi na tutabaki waminifu katika maisha yetu ya kila siku.
Wapendwa somo la kwanza mosi linatukumbusha historia ya uumbaji wa wazazi wetu wa kwanza. Somo hili linatupa asili ya binadamu. Mungu aliwaumba Adamu na Eva, wazazi wetu wa kwanza, akawaweka katika bustani ya Edeni, maisha ya watu wa kwanza yalikuwa maisha ya heri na amani. Walikaa pamoja na wanyama kwa amani wakajilisha majani na matunda.(cf. Mwanzo 2:15-17). Pili Somo I la leo kutoka kitabu cha Mwanzo(Mwa 2:7-9, 16-18, 3:1-7) linatukumbusha kuanguka kwa wazazi wetu wa kwanza Na madhara ya kuangka kwao yaani ya dhambi ya kwanza ni chimbuko ya kuingia kwa dhambi ya asili na dhambi nyingine katika ulimwengu huu. Adamu na Eva walishawishiwa na nyoka, mnyama aliyekuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu. Hii ndiyo kazi ya shetani, kuwashawishi wanadamu wafanye mambo yaliyo kinyume na mapenzi ya Mungu. Kwa wayahudi, neno “shetani” lilimaanisha kitu chochote kinacholeta mgongano kati ya watu, wenyewe kwa wenyewe na hata kati ya watu na Mungu. Shetani wakati wote yu chini ya mamlaka ya Mungu (Zak 3:1-10; Joe 1-2), kwa hiyo ndugu zangu, “Tumtegemee Mungu tunapopatwa na vishawishi.”
Wapendwa tukisoma Isaya 5: 20-21 tutasikia kama ifatavyo: ole wao wasemao kwamba uovu ni wema, na kwamba wema ni uovu, watiao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza; watio uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu. Ole wao walio wenye hekima katika macho yao wenyewe, na wenye busara katika fikira zao wenyewe. Wapendwa maneno ya nabii Isaya yanaweza kutupa nafasi ya kutafakari kuanguka kwa wazazi wetu wa kwanza. Mungu alituumba katika hali ya uhuru. Na katika hali hio binadamu alipewa nafasi ya kuchagua mema yani uhai ao mabaya yaani kifo. Kitabu cha Mwanzo kinatupa picha ambao inaoneshwa wazi uhuru wa mwanadamu katika kuchagua kifo badala ya uhai. Kwa hiyo mwanadamu alichagua uovu panafasi ya wema, giza panafasi ya nuru, uchungu panafasi ya utamu na mwishoni kabisa aliweka hekima na busara katika macho yake mwenyewe na hiyo ilikuwa kwake ole na mwanzo wa mateso yake hadi kuchafua ulimwengu nzima.
Jambo hilo linaonesha wazi kutokujikubali na kuthamini maisha yetu kama viumbe vya Mungu na kukataa ubinadamu wetu. Wapendwa, tutambue kwamba, unapojikataa wewe  wenyewe ao ninapojikataa mimi wenyewe, tunafungua nafasi ya kutamani maisha ya watu wengine yanaoweza kutusababishia madhara makubwa katika maisha yetu. Basi Mungu anatupa nafasi tena ya kutafakari ubinadamu wetu mbele yake hili tuweze kupiga hatua ya mabadiliko katika Maisha yetu na kumrudia yeye aliye Mti mweye kujaa Uhai, Neema na Baraka.
Ndio sababu somo la pili kutoka katika waraka wa Mt. Paulo Mtume kwa Warumi linatuonesha wazi ukurasa wa uumbaji wa pili katika kuteswa, kufa na kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Basi tunafarijika na maneno ya Mungu kwetu kwamba: kwa kosa moja watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima. Kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi walingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa utii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki.
Wapendwa kutokana ya Utii wa Yesu kwa Baba yake, ulimwengu mzima uliumbwa upya kwa kifo na ufufuo wake. Basi tutambue kwamba kwa wana wa israeli kitabu cha kutoka kina nafasi ya pekee katika historia ya maisha yao na Mungu. Yaani ukombozi kutoka utumwani Misri ni sehemu ya peke katika maisha yao ya imani. Lakini katika kutoka walikutana na vishawishi na mara ninyi walishindwa kupambana na vile vishawishi... Simulizi la kujaribiwa kwa Yesu katika Injili ya leo ni hitimisho wa nyakati mbalimbali za majaribu katika maisha ya wana wa Mungu na katika maisha yetu sisi wana warithi wa Mungu kwa njia ya Yesu. Ndio sababu kwetu sisi wakristu leo nilazima kwanza kuelewa maana ya ufufuko kama chanzo cha imani yetu ili tuweze kusoma na tutafakari vema agano jipya kusudi tutafsiri na kuelewa agano lakale. Masimulizi haya yamefupishwa na kuwekwa mwanzoni mwa utume wa Yesu ili kuonesha kwamba, Yesu ndiye kweli hitimisho ya Agano la kale na kweelelezo cha utii kwamba ingawa alipatwa na majaribu yote katika maisha yake, alichagua kubaki mwaminifu kwa Mungu.
Hali hii ya Yesu inakumbusha ile ya waisraeli walipokuwa jangwani kwa miaka arobaini kabla ya kurudi katika nchi takatifu yaani, nchi ya ahadi. Waisraeli hawakuwa waaminifu kwa Mungu wakati wote, walishindwa kumtegemea Mungu walipopatwa na vishawishi au majaribu au magumu katika maisha yao. Katika simulizi ya leo, Yesu kwanza anamshinda shetani na kujifunguwa na kutufundisha sisi leo kwamba yeye ndiye Neno Timilifu na Mkate wa kweli utokalo mbinguni. Sehemu hii ya jaribio la kwanza linahitimisha kitabu cha kutoka sura ya 16 na sura 17 ambao wana waisraeli walinungunika kuusu chakula huku wakikumbuka sufuria za nyama na chakula walivyo kula huku Misri hadi kutupilia mbali wema wa Mungu kwao... kwa hiyo Mungu akamwambia Musa: Tazama, mimi nitawanyeshea ninyi mvua ya mkate kutoka mbinguni... na mkate huyo ni Yesu Kristo wale sio yale chakula kutoka Misri. Na huku wakigoma kwa sababu ya maji... Ndio sababu tukisoma kitabu cha Kumbukumbu la Torati sura ya 8:2-3 tutasikia kama hifatavyo: nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako, aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu, kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake au sivyo. Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyaijua wewe wala baba zako hawakuijua, apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana. Na kwa kuhitimisha hilo Yesu anasema hivyo katika injili ya Yohane sura ya 6: 54-56: Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywanji cha kweli. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake.
Jaribio la pili linamtaka Yesu ajioneshe mbele ya watu kuwa analindwa na Baba yake. Shetani naye sasa anatumia Maandiko Matakatifu kutegemeza jaribio lake. Katika Zaburi 91:11-12, Mungu anaahidi kuwatuma malaika wamchukue mtumishi wake asije akajikwaa kwenye jiwe. Yesu hana shaka na ulinzi utokao kwa Baba yake. Lakini anakataa kutumia uwezo wa Baba yake bila sababu ya maana. Hataki kujitia mwenyewe katika hatari ili aoneshe uwezo wake. Kufanya hivyo ingekuwa ni kutumia vibaya uwezo wa Mungu. Kwa hiyo, Yesu alimjibu shetani akamwambia: “Usimjaribu Bwana Mungu wako” (Kumb 6:16).
Jaribio la tatu linamtaka Yesu amwache Mungu na amwabudu Shetani kwa malipo ya kupata utawala wa kisiasa. Mambo yanapofikia hatua hiyo, Yesu hawezi kuendeleza mazungumzo na Shetani. “Nenda zako, Shetani” Yesu aliamuru. Mwana wa Mungu hawezi kumwabudu Shetani kwa malipo ya kiasi chochote, kwani imeandikwa, Utamwabudu Bwana Mungu wako na kumtumikia yeye peke yake.
 

Wapendwa katika Kristo, Simulizi la kujaribiwa kwa Yesu linaonesha kazi ya ibilisi ya kuwajaribu watu katika kazi zao wanazopewa na Mungu. Ibilisi anakuja kwa Yesu na kujaribu kupendekeza njia nyingine tofauti za kufanya ile kazi aliyopewa. Njia za ibilisi zinaonekana rahisi na za kuvutia, zenye Utukufu na ufahari. Anajaribu kumchanganya Yesu ambaye ni Mungu na Mwokozi wetu lakini Yesu alibaki Imara na kumufukuza mbali shetani katika kazi ya utume wake.
Wewe na mimi leo tujiulize: wakati tunapo kutana na majaribu, magumu, shida ao mangonjwa tunaenda wapi? Leo hii wengi kati yetu wanahabudu chakula na kugawanyana katika familia kwa sababu ya chakula: wakati umepata wageni kwa nini unakasirika kwa sababu ya chakula hadi kuyachugua maji ya ugali na waogesha watoto... wakati wanyonge na maskini wanakuja kwako kwa nini unashindwa kuwasaidia? Wakati huo wa kwaresima uwe kwetu wakati wa kuwajali maskini, yatima, wangonjwa, wafungwa uku tukiwatendea matendo ya huruma...itampendeza Mungu kama familia siku mmja munawatembelea maskini, wazee, wafungwa na kuwasaidia, na kuwaombea...
Leo hii magonjwa, shida na magumu mbali mbali zinatufanya sisi kumusau Mungu hadi kukufuru na kusau upendo wake ndani yetu huku tukitanganga kutafuta tiba kwa watu wasio na uwezo wakutuokoa katika shida hizo...wakati huu ni vizuri kila mmja wetu, kila familia ampelekee bwana shida, mangonjwa, magumu yake na asali na kufunga huu akitenda matendo ya huruma naye Mungu awezi kukuacha...
Na ninyi wanafunzi, wazazi wanateseka kuwasomesha huku mama akiuza mchicha, baba kila siku asubuhi akiamka mapema na kwenda kutafuta apa na pale kusudi wewe uboreshe maisha yako ya kesho...sasa kwa nini tunashindwa kuwaombea wazazi wetu na ndungu wetu wengine wanaotusaidia kusudi tusome? Kwa nini tunajisau huku tukitamani maisha ya wengini inaozidi kipato cha familia zetu hadi kushawishika huku tikikuza tamaa, kuanguka na kuharibu maisha yetu? Mmtafute kwanza Yesu na kuwaombea wazazi wenu naye Mungu atawasaidia nyote...Basi ndungu zangu tukiwa na Yesu Kristo siku zote za maisha yetu, tutamushinda muovu shetani anaekuja kila siku katika ali mbali mbali ya maisha yetu.
Wapendwa katika Kristo, Jumatano iliyopita, ndiyo Jumatano ya Majivu, tulianza rasmi safari yetu ya mfungo wa Kwaresima kwa siku arobaini. Kusali, kujitoa sadaka kwa ukarimu kwa wahitaji na kufunga, ndizo nguzo kuu tatu za kipindi cha Kwaresima. Tumesikia katika masomo yetu ya leo habari za vishawishi au majaribu. Leo tunapewa himizo tukiwa mwanzoni kabisa mwa kipindi cha Kwaresima, “Tumtegemee Mungu tunapopatwa na vishawishi.”
Tumsifu Yesu Kristo
 
Shemasi Bienvenu Kabeya Kungwa Ngungwa Poulain Loquace, sds
 
 
                                                                                                                                                    

Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA