MAHUBIRI YA DOMINIKA YA TANO YA KWARESIMA MWAKA A

MASOMO
Somo I: Eze. 37: 12-14
Somo II: Rum. 8: 8-11
Injili: Jn 11: 1-45

SALA: Ee Bwana, tunakuja mbele yako kukusifu na kukushukuru kwa ajali ya upendo wako mkuu kwetu: Bwana utusaidie kushinda maradhi ya Coronavirus.

UTANGULIZI
Leo Kanisa Katoliki Takatifu inaadhimisha Dominika ya Tano ya Kwaresima basi wapendwa tuungane na kutafakari na Bwana Wetu Yesu Kristu anaposema: Mimi ndimi huo ufufuo, na Uzima... Yeye aniaminiye mimi, hatakufa kabisa hata milele.

UFAFANUZI
Wapendwa, leo katika jamii yetu ya kisasa kifo bado kinabaki kuwa funguo ya ulizo: mwanadamu ni nani? Kwa nini kufa? Kwanza tutambue kuwa kuna njia mbili ambazo wandadamu waweza kuelezea kuusu kifo: papa Benedicto wa XVI aliandika na kutafsiri hizi njia mbili. Alisema hivi: watu wengi zamani, na baadhi yao wapo bado leo, walifuata njia ya watalamu ya elimu ama wanafalsafa na kujaribu kufasiriya kifo...walizani kwamba kunamvutano kati ya mwili na roho katika mwanadamu huku mwili ukifamika kuwa gereza ama jeneza ya roho ambao ufunguo wa gereza ao jeneza ya roho ulikuwa tu ni kifo kwa sababu waliamini kwamba wakati kifo kimefika mwili ujifunguwa na kuachana na roho huku roho upata nafasi ya uhuru na ya kuishi milele. Ndio maana wengi utesa miili yao na kuhisi kwamba mwili ndo usababisha mateso na shida...kwa sisi leo wakristu mtazamo huyo sio sahii.
Ndio maana papa wetu utualika kuitazama mafundisho ya Biblia ama njia ya Biblia ambao utufundisha kwamba mwanadamu ni mwili na roho kwa pamoja kwa hiyo tunasema mtu fulani kafariki ila hatusema kwamba mwili wa mtu fulani kafariki...maana yake nini? Maana yake maisha yetu ya ndani lazima yaende sambamba na maisha yetu ya nje, maisha yako ya kimwili lazima yaendane na maisha yako ya kiroho na hayo yote tunayapata katika mateso, kifo na ufufuo wa Bwana wetu Yesu Krsito. Kwa hiyo ufufuo wa Yesu ni matumaini mapya kwetu, Yesu Mfufuka anatupa matumaini kwamba, kwa Neema ya Mungu, mwanadamu baada ya kifo atafufuka katika maisha mpya.
Sasa kifo ni nini? Kwa wale wasio mwamini Yesu kifo kwao ni mwisho wa kila kitu na mwisho wa maisha ya wanadamu na hayo yatabaki kuwa maswali bila majibu kwa watu ambao bado wanashindwa kuweka matumaini yao kwa Mungu lakini kwa yule ambaye Kristo ni Mwanga, Njia na Uhai maswali haya hakika haina nafasi. Kwa sababu kifo kwake ni hatua ya maisha mpya katika neema na baraka yake Mungu ambao Kristo utuonyesha wazi kupitia ufufuo wake.

Kwa mtazamo huyo kila mara tunapo kutana na kifo ni lazima tujiulize kwamba maisha yetu ya kimwili yaendana sare na maisha yetu ya kiroho. Kusudi hatatutakapokufa matumaini yetu kwa Yesu yasififie. Basi wapendwa tukielewa kwamba kifo sio jeneza ao gereza ya mioyo zetu ao sio mwisho wa maisha ya wanadamu tutatafakari vizuri masomo yetu ya leo. katika somo la kwanza Nabii Ezekieli anawatangazia Waisraeli mwisho wa utumwa na kurudi kwao katika nchi ya ahadi toka utumwani. Nabii Ezekieli anaeleza juu ya kupandishwa kwa taifa la Israeli akitumia mfano wa kuyafunua makaburi na kuwapandisha watu wake. Ahadi ya uzima inawekwa tena kwa watu ambao kama mifupa mikavu hawana matumaini ya kuishi. Kuokolewa huko toka utumwani ni mfano wa Kipasaka wa tumaini la ufufuko. Hata maneno ya nabii yana muono wa Kipasaka kwetu sisi: “Nitafunua makaburi yenu…..nami nitatia roho yangu ndani yenu, nanyi mtaishi.” Mungu anaonesha kuwa makaburi si mahali pa mwisho pa kupotea au shimo la kutupa maiti kama takataka...bali ni mahali pa mpito na mwanzo wa maisha mapya ya kipasaka. Ukombozi huo wa kuwatoa katika makaburi ni mfano wa ufufuko wa miili yetu siku ya mwisho. Kumbe, kwa kifo tunapata tumaini la ufufuko
Ndio maana Zaburi(130) yetu leo utuonesha wazi kwamba mbele ya Bwana kuna huruma, kuna fadhili, na kwake kuna ukombozi. Hapo mkosefu ni taifa nzima la Israeli  ambalo utambua upendo usio na mipaka wa Mungu, Neema na Huruma ya Mungu na kuamini kwamba kuhurumiwa na Mungu ni Mwanzo wa maisha mpya, wa agano mpya wa matumaini mpya uliozidi ukosefu wao. Wapendwa hata sisi leo tutambue kwamba sisi ni wakosefu na dunia yetu imechafuka na maovu makubwa kabisa ambao utuweka sisi makaburini na kufutilia mbali matumaini yetu kwa Mungu... lakini tutambue kwamba Mungu ni Mwaminifu na Baba yetu anayekuja na kufungua mikono yake kabla hata sisi atujafungua vinywa vitu( Luka 15) na kutuonyesha huruma na ukombozi wake uliopita ukosefu wetu basi katika shida inaotusumbua leo yaani Coronavirus, tusikate tama tuweka matumaini yetu kwake Yeye ambaye ni kila kitu kwetu na kupiga magoti na kusema: Bwana, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama? Lakini kwako kuna msamaha ili Wewe uogopwe.

Woga wa Mungu ni kwa sababu Mwanadamu amwabudu, aweke matumaini katika Yeye. Ndio maana katika injili Yesu udhiririsha ukubwa wa Mungu kwa kumfufua Lazaro. Kwanza Yesu pia anatupa sisi watumaini kwamba kifo sio mwisho wa maisha yetu na Matumaini na nia yetu ni kumwona Mungu jicho kwa jicho... Ndio maana Yesu utumia waneno ifatavyo: Rafiki yetu Lazaro, amelala maana anapumzika Yesu anataka kutuambia kwamba sio mwisho ya maisha ya mwanadamu, bali ni njia ya kupita kutoka hatua mja na kuelelekea hatua nyingine zaidi mno katika maisha yetu ya neema... na ni Yeye peke yake ambaye uweza kutusafirisha katika safari hio: ndio maana Yesu anasema: Mimi ndimi huo ufufuo na uzima.

Pili Yesu utualika kuwa watu wa imani kwake: Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi, naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, Unayasadiki hayo? Yesu anataka kutufundisha kuwa kifo si kitu cha kutisha kwa yeyote mwenye imani bali ni hatua ya kuingia kwenye upya wa uzima wa milele. Pia tusadiki kuwa utukufu wa Mungu utadhihirika kwa njia yake, yaani kwa kifo na ufufuko wake. Kwa hiyo inaoitajika ni kumtambuwa Yesu kuwa ni Masiya na Mwana wa Mungu pia na kukiri imani yetu mbele yake kama vile Petro na Martha nakusema: Naam, Bwana nimesadiki ya kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.
Basi tukiwa na imani kwa Yesu ni lazima tuishi imani yetu kwa vitendo. Ndio maana katika somo la pili Mtume Paulo anasema: lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake...ikiwa Roho wake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu. Mtume paulo anataka kutuambia kuwa kuishi katika Roho ya Kristo ni kuisha katika roho ya upendo, Roho ambalo utajwa hapa ni Upendo ambao Yesu mwenyewe uonyesha kwa kufa msalabani kwaajili ya dhambi zetu na ndo Roho yule yule ambaye mimi na wewe leo tunaitwa kuufata kwa kujitolea bila kijibakiza kwa wenzetu wanao itaji msaada wetu hususani wakati huu wa Kwaresima.
Wapendwa namaliza tafakari hii na kusema kwamba kifo ni haki yetu mbele ya Mungu. Kwa sababu Mungu ametuumba kwa upendo wake na kwa lengo maalumu. Kwa hiyo, mtu anapokufa anakuwa amemaliza muda wa kuwa hai aliopewa na Mungu. Hivyo basi, mbele ya Mungu aliye Bwana wa uhai na nyakati zote ni safi na ni vema. Lakini kwa sababu ya hali yetu ya kibinadamu tunapata taabu, huzuni kwa vile hatuwezi kuelewa fumbo la Mungu. Basi katika hali hiyo ya kibinadamu, tusihangaike, tujue kuwa Mungu ata katika hali hiyo, shida ao magumu yu pamoja nasi. Pia tutambue kuishi miaka mingi au michache hakutimii kwa hesabu zetu za kibinadamu bali ni zawadi. Tujiandae vyema kupokea kifo, kwani kwa kifo tunapata tumaini la ufufuko.

Shemasi Bienvenu Kabeya Ngungwa Kungwa Poulain Loquace, SDS

Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA