MAHUBIRI YA DOMINIKA YA TATU YA KWARESIMA MWAKA A WA KANISA: KWELI UNA KIU CHA MUNGU?
 
MASOMO

SOMO LA KWANZA. Kutoka 17: 3-7
SOMO LA PILI Warumi 5: 1-2,  5-8
SOMO LA INJILI Johane 4: 5-42

WAZO KUU: TUWE WATU WENYE KIU CHA MUNGU NA MATUMAINI KWAKE

UTANGULIZI: BIBLIA NA LITURUJIA
 
Wapendwa Mama Kanisa: Katoliki Takatifu uwa na himiza katika mafundisho yake kuwa: jambo muhimu kuliko yote katika adhimisho la Liturujia ni Maandiko Matakatifu, maana katika hayo huchukuliwa masomo ya kusomwa na kufafanuliwa katika mahubiri, na pia zaburi zinazoimbwa. Sala, maombi na nyimbo hupata uvuvio toka Maandiko, kama vile toka Maandika matendo na ishara hupata maana. Kwa hiyo, ili kufaulu kufanya marekebisho na maendeleo na malinganisho ya Liturujia, ni lazima kuhimiza ule upendo mtamu na hai wa Maandiko Matakatifu, ambao unashuhudiwa na mapokeo mastahiki ya Makanisa ya Mashariki na Maghari.( haya tunayapata katika Hati za Mtaguso Mkuu wa Vatican II katika Constititusio juu ya Liturujia ufahamika kama Sacrosanctum Concilium article 24)
Basi tukiwe na lengo hilo ndani mwetu basi tuangane na Maandiko Matakatifu ya leo inao tutaka leo mimi na wewe kuwa na kiu cha Mungu na matunaini kwake.
SALA: Tumuombe Mungu kusudi tushindwe mateso, magumu, magonjwa... kila mtu kadiri ya wito wake aweze kushinda  kiu chake kama fedha, anasa, madaraka, wizi, ushirikina, mali inao tupeleka kuwahudumaza wenzetu na kumwacha Yeye Aliye Maji ya Uzima. Pia tuombe neema na utakaso wa Mungu katika wakati huu Dunia iko katika shida na hofu ya ugonjwa wa cororavirus.
UFAFANUZI WA MASOMO YETU
 
Wapendwa leo tunahadhimisha Dominika ya tatu ya kwaresima katika mwaka A wa Kanisa. Katika Dominika hii tunaalikwa na Yesu kumfuata Yeye Mungu na Mwokozi wetu kusudi tupate Maji ya Uzima wa milele hili tumalize kiu chetu. Basi nawalikeni sote kutafakari Mafumbo Matakatifu huku tukijiweka tayari kuongea na kumsikiliza Yesu kama yule Mwanamke Msamaria katika injili yetu ya leo.

Wapendwa, katika somo la kwanza tunasikia mwendelezo wa manunguniko na upungufu wa imani wa wana waisraeli. Kitabu cha Kutoka kinatupa picha halisi ya maisha ya wana wa Israeli katika safari yao ya ukombozi katika jangwa. Wapendwa katika sura ya 16 ya Kitabu cha Kutoka, katika Jangwa wana wa Mungu walipatwa na njaa na mkutano mzima wa wana wa Israeli ukawanung’unikia Musa na Haruni, huko barani... wakawaambia: laiti tungalikufa kwa mkono wa bwana katika nchi ya Msri, hapo tulipoketi karibu na zile sufuria za nyama, tulipolula vyakula hata kushiba; kwani mmetutoa huko na kututia katika bara hii, ili kutuua kwa njaa kusanyiko hili lote. Ndipo Bwana akamwambia Musa: tazama, mimi nitawanyeshea ninyi mvua ya mkate kutoka mbinguni... Mungu ni Baba yetu na katika agano lake yeye ubaki kila siku Mwaminifu na Mwenye Haki. Yeye alisikia kilio cha watoto wake naye akawajibu na kuwapa Mana.
Cha kushangaza wana wa Israeli wanashindwa kumtegemea na kumtumainia Mungu kila mara walipata mateso na magumu katika safari ya ukombozi wao. Ndo sababu leo katika somo letu la Kwanza, kutoka katika katika kitabu cha Kutoka sura ya 17. Wana wa Mungu wakawa na kiu huko; nao wakamnungu;unikia tena  Musa kama vile walivyofanya katika sura ya 16... Musa akamlilia Bwana, akisema, niwatendee nini watu hawa? Bado kidogo nao watanipigia kwa mawe... Bila shaka Mungu anawatendea tena muujiza nao wakapata maji. Wapendwa baada ya muujiza kutoka kwa Mungu, Musa alipahita mahali jina lake Masa kwa sababu ya mateto ya wana wa Israeli na Meriba kwa sababu walimjaribu Bwana, wakisema, Je Bwana yu kati yetu au sivyo?
Wapendwa maji bila shaka ni alama ya uzima, maji ni alama ya utakaso katika miili yetu na katika roho zetu, maji inatumika katika sakramenti ya ubatizo. Ndio sababu Mama Kanisa linatufundisha kama ifatavyo kuusu maana ya maji Mosi: katika liturujia ya Usiku wa paska, wakati wa kubariki maji ya Ubatizo, kanisa linafanya rasmi kumbukumbu ya matukio makuu ya historia ya wokovu ambayo yalikuwa kifano cha fumbo ya Ubatizo: kwa hiyo Mungu anatenda kwa nguvu isiyoonekana mambo ya ajabu kwa njia ya sakramenti. Umekifanya kiumbe maji kwa namna mbalimbali kiwe ishara ya neema ya Ubatizo.(cf. Katekisimu ya kanisa katoliki art. 1217 pia kitabu cha mwanzo 1:2) Pili: Maji ya chemchemi yanapokuwa alama ya uzima, maji ya bahari yanakuwa alama ya mauti. Ni kwasababu hiyo maji haya yanaweza kuwa kifano cha fumbo la msalaba. Kwa njia ya mfano huu Ubatizo juashiria ushirika katika mauti ya Kristu.(Cf. Katekisimu ya Kanisa Katoliki art. 1220)
Wapendwa tujiulize sasa kwetu sisi somo hili linatufundisha nini? Kwanza kabisa tutambue kwamba kutokuwa na imani kwa wana wa Israeli kila mara  wanapopatwa na shida, magumu ao mateso, uonyesha picha halisi ya kila mwanadamu anaye tujiuliza kama kweli Mungu yu katika maisha yake hususani pale anapopata shida, magonjwa, mateso,, njaa na kazalika. Lakini tutambue kwamba, jangwa si sehemu ya mateso ya kudumu ila kwa anaye mwamini Mungu, katika jangwa tunasafiri na katika safari kuna vishawishi, changamoto, shida... lakini kwa mkristu nilazima kumtumainia Mungu kama Msimamizi wa safari yetu. Kwa hiyo jangwa inakuwa kwetu sehemu ya kusali, ya kujithamini, kujitakasa na ya kuvumilia mateso...basi kupata maji katika jangwa maana yake ni kuwa na matumaini ya kwamba Mungu yuko nasi hata katika shida, Mungu yuko nawe hata katika magonjwa, hata katika coronavirus, inayoitajika ni kuwa na imani, kuwa na matumaini na kutemgemea Yeye kila siku ya Maisha yetu. Basi tusimjaribu na kumwacha Mungu wakati wa shida ao mateso huku tukitanga tanga ya kutafutu miungu wasiojulikana. Tukimwamini Mungu  tutapata maji ya uzima wa milele.

Wapendwa katika injili tunasikia simulizi ya Yesu na yule mwanamke Msamaria kuusu Maji. Yesu katika safari yake  ya kuelekea Yerusalemu akafika kunako mji wa Samaria, Yeye kama myaudi anamwomba Msamaria akisema: Unipe maji ninye. Bila shaka yule Mwanamke anamjibu na kumwambia kuwa: wayahudi hawachangamani na wasamaria... Yesu akajibu, akamwambia: kama ungalijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, nipe maji ninye, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai. Maneno ya Yesu yanamufanya mwanamke kuvutiwa na mazungumzo na Yesu na kusema: Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai...? Yesu akajibu: kila anywaye maji haya ataona kiu tena; walakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele. Na yule mwanamke akwamwambia: Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.
Wapendwa simulizi hii inaonyesha wazi nia ya Mungu ya kumuokowa kila mtu hata yule alietengwa na wanadamu wenziye, alietengwa na jamii ao ndugu, rafiki huku akionekana kuwa mkosefu zaidi mbele yao. Yesu alikuja kutafuta wakosefu na kuwapa uzima wa milele watu wote. Na injili ya Mathayo 18: 12-14 inasema hivi: Mwaonaje? Mtu akiwa na kondoo mia, mmja akampotea, je hawawaachi wale tisa na tisini, akaenda milimani, na kumtafuta yule aliye potea? Hata akipata kumwona, amin, nawaambia, amfurahia huyo zaidi, kuliko wale tisa na tisini wasiopotea. Vivyo hivyo haipendezi mbele za Baba yenu aliye mbinguni kwamba mmja wa wadogo hawa apotee.
KATIKA MAISHA YETU
Wapendwa, katika simulizi ya leo tutafakari mambo muhimu ifatavyo: Mosi: ni vema kutambua kwamba Mungu anatupenda sisi sote na yuko na mpango na kila mmja wetu. Kwa hiyo katika safari ya wokovu wetu ni Yeye kwanza anayechukua hatua ya kwanza na kuja kwetu kutafuta urafiki nasi basi mimi na wewe tunaombwa kumsikiliza na kuonyesha ushirikiano katika wito wake kwetu. Yesu ni Yeye kwanza alitafuta urafiki na yule mwanamke kusudi amwokowe katika hali yake ya upotovu na yule mwanamke alionesha usikivu na ushirikiano hadi akapatwa na kiu cha Mungu: Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.
Pili katika wito wetu Mungu anayajua mapungufu yetu yote vizuri. Sisi nilazima kuwa wazi mbele yake na kufanya jitihada ya kuyaacha. Yesu alienda kisimani saa sita kusudi akutane na yule mwanamke: watalamu wa Biblia uwa na tafsiri kwamba sio kawaida kwenda kisimani saa situ kwa kina mama. Wanawake wengi uwa naenda kuteka maji asubuhi ao jioni huku mara nyinyi wakiongozana kama kundi ya watu wawili ao watatu ao zaidi... lakini yule mwanamke msamaria inaonekana alikua akitengwa na jamii labda kwaajili ya matendo yake uliokuwa ayendani na mila au desturi ya jamii yake huku akisubiri na kulenga kuwa kisimani hakuna mtu ili awe katika amani na salama... na haya hudhibitiswa wakati Yesu anamwambia: Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa. Yule mwanamke akajibu, sina mume. Yesu akamwambia, umesema vema, sina mume; kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli. Maana yake hatuna budi kujificha mbele ya Mungu ila tujifunze kumwambia Mungu ukweli na uzito wa udhaifu wetu nasi tutapata faraja kama huyu mwanamke...tunaweza kuwakimbia binadamu wenzetu lakini hatuwezi kumkimbia wala kujificha mbele ya Mungu. Tuwe watu wenye kujitambuwa hasa kutambuwa makosa na dhambi zetu.
Tatu: nilazima kumtambua Yesu kupitia mazungumzo naye. Tumumpe Yesu nafasi ndani ya maisha yetu kusudi tupate kumtambuwa yeye kama Masiya. Kwetu ni kama kupitia sakramenti, sala, mioyo zetu, wenzetu,maskinin, wanyonge, mangonjwa, shida, Kanisa... hizi ni nafasi ambao tunakutana na Yesu. Yule mwanamke alimpa Yesu nafasi na kumsikiliza hapo alifunuliwa naye hadi kumkiri na kusema: Bwana, naona ya kuwa u Nabii... Naye Yesu akamwambia: Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu... Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Yule mwanamke akamwambia: Najua ya kuwa yuaje Masiha, aitwaye Kristo; naye atakapokuja, yeye atatufunulia mabo yote. Yesu akamwambia: Mimi ninayesema nawe, Ndiye.
Inne: Tunapo mtambuwa Yesu kama Masiya ni lazima tuondoke, twende kuwapasha, kuwahubiri, na kuwavuta wenzetu pia waje kumtambua. Hii ni jikumu la kila mmja mwetu baada ya Ubatizo kadiri ya wito wake ndani ya kanisa kumtangaza Kristo popote ulimwangani kwa ushuhuda wa maisha na imani yetu kama wakristu, kwa kuwaudumia watu bila kochoka... hayo tunayapata katika injili. Yule mwanamke baada ya kutambua Yesu kuwa ni Masiya akauacha mtungi wake yaani akaacha matendo yake yote ya zamani, akaenda zake mjini na kuwa missionari na muhubiri wa habari njema kwa watu: Njoni, mtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda. Je haimkini huyu kuwa ndiye Kristo? Basi wakatoka mjini wakamwendea.
 
Nataka nikwambiye leo: usikate tama,usichoke kumtafuta Yesu Kristo katika maisha yako hususani katika shida, mateso, magonjwa... usichoke kuungama mbele yake kama mzambi na mkosefu, tambuwa mapungufu yako na utubu naye Yesu atakufunya kuwa chombo cha habari na baraka yake kwa watu wanao kuhukumu wewe kama mkosefu. Ndio maana Mtume Paulo katika somo la pili kutoka katika waraka kwa warumi hutusihi na kutuonya kwamba: Na tuwe na imani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo. Ambaye kwa yeye tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo tunasimama ndani yake; na kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu.


Tumsifu Yesu Kristo

Shemasi Bienvenu Kabeya Kungwa Ngungwa Poulain Loquace

 

Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA