MAHUBIRI YA SHEREHE YA KUPASHWA HABARI YA KUZALIWA BWANA: 25 MARCH 2020

MASOMO
Somo I: Isa. 7:10-14
Somo II: Ebr. 10:4-10
Injili: Luka 1:26-38

SALA: Kwa maombezi ya Mama Bikira Maria, tumuombe na kumshukuru Mungu kusudi atuepushe na maradhi ya ugonjwa wa coronavirus na awape uzima na pumziko la milele wote walio tutangulia mbele ya haki kupitia ugonjwa huo.

UTANGULIZI
Wapendwa leo Mama Kanisa anahadhimisha sherehe ya Kupashwa Habari ya Kuzaliwa Bwana. Sherehe ya leo ilianze kwaadhimishwa na Kanisa tangu karne ya 6-7 huku wa kihesabu miezi 9 kabla ya kuzaliwa Mwokozi wetu Yesu Kristo. Yaani ukihesabu tarehe 25 ya Mwezi wa Tatu hadi tarehe 25 ya Mwezi wa Kumi na Mbili utapata mwezi Tisa. Wapendwa kupashwa habari ya kuzaliwa Bwana ni mwanzo wa muhula mpya na ukombozi wa Mungu kwetu sisi ambao Mungu anaonyesha upendo wake mkuu kwa ulimwengu mzima.

UFAFANUZI
Tukisoma katika Biblia, tutaona kuwa katika historia ya wanadamu na Mungu kuna baadhi ya watu walipashwa vile vile habari ya kuzaliwa kwa watoto wao katika hali ya ajabu mno. Katika kitabu cha Mwanzo 18: 9-14 Ibrahamu kupitia mkeo Sara anapashwa habari ya kupewa mtoto wa kiume: wakamwambia yuko wapi mkeo Sara? Akasema, yumo hemani. Akamwambia, hakika nitakurudia wakati uu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Basi Ibrahaimu na Sara walikuwa wazee, na umri wao mkubwa, na Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake... tena katika kitabu cha Waamuzi 13:2-7, 24-45 Manoa na mkeo alikuwa tasa, hakuzaa watoto anapashwa pia habari za kupata mtoto: Malaika wa Bwana akamtokea yule mwanamke, akamwambia: Tazama, wewe sasa u tasa, huzai; lakini utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume... na wembe usipite juu ya kichwa chake, maaana mtoto huyo atakuwa Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni; naye ataanza kuwaokoa Israeli na mikono ya wafilisti... Basi yule mwanamke akamzaa mtoto mwanamume akamwita jina lake Samsoni... Katika Agano Jipya: tukisoma Injili ya Luka 1:5-25, 57-80 tutasikia kutabiri kuzaliwa kwake Yohane Mbatizaji: ... Akatokewa na Malaika wa Bwana, amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia. Zakaria alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia. Lakini yule Malaika akamwambia, usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohane...(Rejea Luka 1: 11-13) Wapendwa kupashwa habri na Malaika kuhusu kuzaliwa kwa watoto katika Biblia kulionesha uku na uwezo wa Mungu dhidi ya elimu na akili ya wanadamu. Lakini katika tukio ya leo nilazima tulitafakari katika mtazamo wa pekee.
Wapendwa tutambue kwamba tukio ya Kupashwa Habari Kuzaliwa Bwana ni tofauti kabisa na zile matukio mbali mbali katika Biblia ambamo Mungu anajibu na kutenda maajabu kutokana na sala na dua ya watoto wake. Lakini katika sherehe ya leo Mungu kwa hiari yake Mwenyewe anakuja tena kuumba dunia na kutakasa ulimwengu nzima baada ya upotevu ya wazazi wetu wa kwanza. Pili Mungu anamushirisha mwanadamu katika ukombozi wa mafumbo haya matakatifu. Ndio maana Kanisa letu Katolika linatufundisha hivi:
Maandiko Matakatifu ya Agano la Kale na Agano Jipya na Mapokeo ya kale yaonesha wazi zaidi na zaidi dhima ya Mama wa Mwokozi katika mpango wa wokovu, na kuiweka mbele yetu tuifikirie... Mungu wa huruma alitaka Umwilisho(Incarnation) utanguliwe na ukubali wake yeye aliyeteuliwa tangu milele awe Mama, ili kama vile mwanamke alivyoshiriki kuileta mauti, kadhalika mwanamke asaidie kuuleta uzima.(Cfr. Konstitusio ya kidogma juu ya Fumbo la Kanisa, art. 55-56)
Kwa hiyo, katika sherehe ya leo lazima tukumbushane mambo muhimu ifatavyo: Mosi Maria alitakaswa na Mungu na kuwekwa kuwa Mtakatifu na kupewa neema tele kwa nguvu ya Roho Mtakatifu kusudi ya Mungu Yesu akaye kuja kuketi ndani yake. Kwa hiyo hatuwezi kumuongelea Maria bila kumuunganisha na Mwanae Mtakatifu sana Mungu pamoja nasi Emmanueli. Kwa kweli kila mvuto wa wokovu kwa upande wa Bikira Maria kwa watu hautoki katika lazima fulani bali katika mapenzi ya Mungu, na kububujika kutoka wingi wa mastahili ya Kristo. Pili kwa ukubali na utayari wake katika kuifanya mapenzi ya Mungu: Bikira Maria anakweza na Mungu na kuitwa Mwenye heri Mama wa Mungu: wapendwa umama huu wa Maria katika mpango wa neema unadumu bila kukatizwa tangu nukta ile ya ukubali aliotoa kwa imani wakati wa tangazo la kuzaliwa Bwana na alioushikilia bila kusita chini ya msalaba, hadi ukamilifu wa milele wa wateule wote. Tatu Maria alitukuzwa kwa neema ya Mungu, baada ya Mwanawe, kupita malaika wote na wanadamu wote, kwa maana yeye ni mama mtakatifu sana wa Mungu aliyeshiriki mafumbo ya Kristo basi kwa sababu ya hiyo Bikira Maria anaheshimiwa kwa haki na Kanisa kwa ibada ya pekee, nao waumini wote wanaukimbilia ulinzi wake, wakimwomba katika hatari zote na mahitaji yao.
Basi ndugu zanguni, leo ni siku ya furaha kwetu, siku ya kumshukuru Mungu kwa ajili ya upendo wake mkuu kwetu ili tupate wokovu. Pia tunafurahi kwa sababu ya Bibi Yetu Bikira Maria anaye tufundisha kujitoa na kuwa waaminifu na tayari katika kazi ya kumtumikia Mungu: Maria kwa ndio yake neema katika maisha yetu huitimishwa katika tukio nzima ya ukombozi wetu basi mimi na wewe leo kupitia Ubatizo wetu tunaalikwa na Mungu kuwa tayari kusema ndio kwa kufanya mapenzi yake. Basi wapendwa Mama Bikira Maria ni mfano wetu bora wa kuwa mfuasi kweli wa Kristo kwa kujikabidhi na kujitolea bila kujibakiza hadi kushudia mateso, kifo na ufufuko wa Mwanae Mpendwa kwa hiyo tunahitaji waombezi yake kwa Mwanae Bwana wetu Yesu Kristo asa zaidi katika kipindi hiki ya maradhi ya Coronavirus ili tupate utakaso wa miili na mioyo yetu pia tuwe tayari kumtumikia Mungu kupitia wagonjwa, maskini, wafungwa na wahitaji wote.
 
Tusema wote pamoja katika imani: kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, dhabihu na toleo hukutaka, lakini mwili uliniwekea tayari. Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo, ndipo niliposema, Tazama nimekuja katika gombo la chuo nimeandikiwa niyafanye mapenzi yako, Mungu.(Ebr.10: 5-7)

Shemasi Bienvenu Kabeya Kungwa Ngungwa Poulain Loquace, SDS

Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA