MAHUBIRI YA SHEREHE YA MTAKATIFU YOSEFU, MUME WAKE BIKIRA MARIA

MASOMO
Somo I: 2Sam 7:12-14
Somo II: Warumi 4:16-18, 22
Somo III: Mt. 1:16, 18-21, 24
 
SALA: Tumuombe Mungu atujalie roho, upole, utulivu na ulimya wa moyo kama Mtakatifu Yusufu kusudi pamoja na katika imani na amani tuweze kushinda maradhi ya ungonjwa wa Coronavirus.

UFAFANUZI WA MASOMO

Wapendwa leo tunaadhimisha sherehe ya Mt. Yusefu, mume wake Bikira Maria. Tukisoma Luka 1: 30-31 tutasikia utabiri wa kuzaliwa kwake Yesu: Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Wapendwa Mpango wa Mungu wa kilikombowa ulimwangu aukumustuwa tu Bikira Maria lakini ulimustuwa pia mchumba wake Yusufu. Lakini kama Bikira Maria, Yusufu alipata pia neema kwa Mungu huku akifunuliwa jina na kazi ya Masiha: basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.
Wapendwa Yusefu ni nani? Mosi tutambuwe kwamba Yusufu anatajwa tu mara 14 katika injili. Ametajwa kuwa mume wa Bikira Maria na baba halali mlinzi na mlishi wa Yesu(Yohane 6: 42: wakasema, huyu siye Yesu, mwana wa Yusefu, ambaye twamjua babaye na mamaye?, Luka2:48: Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni) Yusufu ni mtakatifu anayefamika kuwa na ustaarabu na utilivu wa pekee. Tunamfahamu kwa ukimya wake, upole na utayari wa kufikiri kabla ya kutenda: kwa tabia hizo zilimfanya achaguliwe na Mungu kuwa baba mlinzi na mlishi wa Yesu na mchungaji wa Familia nzima Takatifu. Tena tutambuwe kwamba Kanisa letu Katoliki linawapa na fasi ya pekee Maria na Mt. Yusufu hadi kuwakumbuka na kuwataje katika adhimisho ya Misa kuwa Yusufu ni Mtakatifu aliyeishi nadhiri ya usafi wa Moyo na Maria ni Bikira milele basi kwa mafundisho haya Yusufu na Maria awakuwa na watoto wengine ila Yesu tu.(kwa sababu kuna baathi ya watu utabiri vibaya injili ya Marko 6:3: Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni?) 
Pili tutambuwe kuwa injili ya Mathayo na Luka inatufundisha wazi kwamba ni kupitia Mt. Yusufu, Yesu aliingizwa rasmi katika ukoo wa Daudi.( Luka 3:23-28, Mt.1:1-17), uwepo wa Yesu katika ukoo wa Daudi ni hitimisho wa mpango wa ukombozi wa Mungu kuanzia Abrahamu-Musa-Manabii.(hata Yohane hudhibitisha katika injili yake sura 1:45: Filipo akamwona Nathanaeli, akamwambia, tumemwona yeye aliyeandikiwa na Musa katika torati, na manabii, Yesu, mwana wa Yusufu, mtu wa Nazareti)
Ndiyo sababu somo letu la kwanza linatoka katika kitabu cha 2 cha Samweli ambapo Mungu kupitia nabi Nathani anaahidi kuusimika ufalme wa Daudi milele kwa kupitia mwanae Solomoni alierithi kiti chake na aliyefanikiwa kulijenga Hekalu la Bwana. Kwa hiyo ufalme wa Daudi uliimarishwa milele kwa kuzaliwa kwa Yesu Kristo aliyekuwa mzao wa Daudi na aliyenjenga Hekalu la Mungu na kusimika ufalme wa Mungu Milele kwa mateso, kifo na ufufuo wake. Ndiyo maana injili ya leo utuonyesha wazi namna gani Mt. Yusufu alivyo toa mchango mkubwa sana kwa kukubali kumpokea Mariamu Mkewe aliyepata mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu ili ufalme wa Mungu wa kilikombowa ulimwengu nzima ukamilike. Ndio maana Mt. Paulo katika somo la pili anadhibitisha kuwa: kwa maana ahadi ya kwamba atakuwa mrithi wa ulimwengu alipewa Ibrahimu na uzao wake, si kwa sheria bali kwa haki aliyohesabiwa kwa imani. Basi wapendwa bila imani hatuwezi kuonja utukufu wa Mungu kwetu. Na Yusufu alionja utukufu wa Mungu kwa sababu aliweka matumaini na imani yake kwa Mungu hadi kupokea ujumbe wa malaika na kuhufanyia kazi.
Wapendwa, hapo lazima tujifunze mengi kutoka kwa Mt. Yusufu. Ki ukweli tuko wengi kati yetu tunapoteza baraka ya Mungu kwa sababu ya kutokuwa na utulivu, imani imara na dhabiti, siri na ukimya wa moyo. Hakika Yusufu angelikuwa papara angepoteza bahati ya kuwa mlinzi na baba mlishi wa Yesu. Lakini sisi kwa sababu ya kwenda haraka katika mahamuzi yetu, tumeishia kufanya matendo kama wapagani na wasiokuwa na imani yenye msingi. Wewe kama mtawa, mkristu, shemasi ao padri, nilazima tumbuwe kwamba bila utilivu na ukimya wa moyo hatuwezi kufanikisha kazi yetu ya kitume. Pale tunapopata shida, tatizo kama Corona Virus leo yafaa tutulie kwanza kabla ya kutenda na kupiga kelele. Nilazima kusikia kwanza ushauri utokalo ndani ya mioyo yetu baada ya kutafari kabla yakutafuta ushauri kutoka kwa wenzetu kwa sababu mshauri wa kwanza ni Roho Makatifu katika mioyo yetu. Pia Kwa ndungu zetu wanyonge, wangonjwa wa tabia, wa miili, kwa ndungu zetu watawa na wengine wote tunao waita mizigo kwetu tusiwaepuke lakini tuwe kama Yusufu kwao kwa kuwalinda na kuwasaidia katika shida na matatizo zao. Baba zetu wafamilia nilazima kulinda familia zetu katika upendo na utulivu wa kweli kama Mt. Yusufu. Na jami nzima ni vizuri kutafuta kuzuia unyanyasaji wa watoto na pia utowaji wa mimba. Mungu kupitia malaika wake na kwa utayari wa Mt. Yusufu, Yeye aliye Uzima aliukinga maisha na Uzima wa Mwanae Mpendwa Mungu na Mwokozi wetu. Basi mimi na wewe leo tunaalikwa kuthamini na kuzuia uwaji wowote kuusu maisha ya watoto. Tuwapenda watoto wetu, kwa kuwapa elimu ya kiriho na kimwili kusudi wafanyikiwe kesho na wawe matumisha bora wa taifa na Kanisa letu nzima. 
 
Shemasi Bienvenu Kabeya Ngungwa Kungwa Poulain Loquace, SDS

Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA