TAFAKARI YA DOMINIKA YA PILI YA KWARESIMA MWAKA A WAKANISA: HUYU NI MWANANGU, MPENDWA WANGU, MSIKIENI YEYE
TAFAKARI
YA DOMINIKA YA PILI YA KWARESIMA MWAKA A
MARCH 8th 2020
Masomo:
Somo I: Mwa. 12:1-4a
`Somo II:
2Tim. 1:8b-10
Somo
III: Injili ya Mt. 17:1-9
UTANGULIZI
Leo tunaadhimisha Dominika ya pili ya Kwaresima, kipindi
ambacho kinatuelekeza kwenye safari ya ukombozi wetu kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo: Yesu Kristo na Masiya
wetu anakamilisha wito wake kwa mateso, kifo na hatimaye ufufuko na utukufu wake. Wapendwa tukiwa na lengo hili basi
tuangane na masomo yetu ya leo inayo tualika kutafakari kuusu wito wetu huku
tukitambulishwa na Mungu Masiya wa kweli Yesu Kristo Mwanae Mpendwa. Kwa Hiyo
kwa kutekeleza wito wetu ni lazima kwanza kumzikiliza Yesu kama vile Mungu
anatuamuru katika injili ya leo na pili kuwa tayari kushiriki mateso pamoja
naye huku tukiwa na matumaini ya kupata utukufu na uzima wa milele.
SALA: Tuwaombea na kuwakumbuka wanawake wote ulimwenguni
wanao sherekea leo siku ya wanawake duniani kusudi kwa maombezi ya Mama Bikira
Maria Mama wa Mungu na Mama yetu, wawe wanawake bora katika jamii katika
kutekeleza malezi bora ya ulimwengu mzima.
UFAFANUZI
Wapendwa, wakati
nilipoanza masoma yangu ya Teologia, Mmja kati ya walimu wangu kila
akitufundisha uwa nahimiza na kukazia mambo muhimu mawili ambacho ufafanua
chanzo na chimbuko ya imani yetu leo kama wakristu pia na ya imani ya wana
waisraeli. Alisema hivi: Wapendwa tutakumbue kwamba Biblia ni kitabu
kitakatifu lakini kimeandikwa na wanadamu kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu. Kwa
hiyo wanadamu hawa waliandika kuendana na maisha yawo ya kawaida huku wakitumia
mifano na experience yao ya kawaida. Pili kwa waisraeli, kitabu cha kutoka
katika Torati ya Musa kinanafsi ya pekee katika maisha yao ya imani. Ukombozi
wao kutoka utumwani misri ni hatua ya kwanza ya maisha yao ya imani na ya
kumtambua zaidi Mungu. Lakini kwetu sisi wakristu leo, Ufufuo wa Bwana Yesu
Kristu ni msingi wa imani yetu na chanzo cha matumaini yetu katika safari ya
kumtafuta Mungu zaidi kila siku ya Maisha yetu. Basi mimi na wewe leo
tunatakiwa kwanza kusoma na kuyahelewa mafundisha ya Agano Jipya kabla ya
kutafsiri ukurasa wa agano lakale kwa sababu Yesu Kristo ndiye anae hitimisha
agano lakale.(Cf. Mwalimu wangu wa Introduction to Theology)
Kwa
nini naanza ya kahuli hiyo kwa sababu masomo ya leo hususani somo la injili
tutatambua kwamba tukio la kugeuka sura Bwana wetu Yetu Kristo ni hitimisho ya
baadhi ya sehemu ya maisha ya waisraeli na pia baadhi ya vipengele katika
kitabu cha Kutoka. Kwa hiyo ninawaalika kuwa makini wote pamoja tutafakari huku
tukimualika Roho Mtakatifu kusudi tujaliwe neema ya kuyaelewa mafumbo
matakatifu.
Wapendwa
katika Kristo, kutoka somo la kwanza tumesikia kuusu wito wa Abrahamu. Aliitwa
na Mungu na kuambiwa atoke kwenye nchi na jamaa zake aende ugenini ili maongozi ya
Mungu yatekelezwe,yaani Abrahamu afanyike Taifa kubwa. Katika simulizi hizi
tutambue kuwa wito wetu ni zawadi kutoka kwa Mungu kwa hiyo wito hutudai mambo
muhimu ifatavyo mosi wito hutudai
imani, Pili uamuzi mzito ambao
unaweza hata kuwashangaza wengine. tatu
hutudai utii na uvumilivu kwa kutekeleza sauti na nia ya Mungu. Kwa hiyo kuachana
na ndugu, jamaa na nchi yake aliyoizoea (Harani) humdai Abrahamu uamuzi mzito.
Lakini kwasababu ya utii kwa Mungu, aliyavumilia mateso ya kuachana na jamaa na
nchi yake akawa tayari kupambana na magumu ya safari kwenda ambako Mungu umwamuru.
Aliyapokea yote kwa imani thabiti akitumainia neema na baraka nyingi toka kwa
Mungu: Kwa hiyo kwa wito wa Abrahamu historia nzima ya wanadamu ilifamika kuwa
nafasi ambapo ahadi ya ukombozi wa Mungu uanza kujionesha taratibu ukombozi
ulianza na wana waisraeli utumwani Misri na pia ulio itimishwa na
Kuteswa-Kufa-Ufufuo wa Bwana wetu yesu Kristu alie ukomboa ulimwengu nzima.
Wapendwa
dominika ya Kwanza na pili ya kwaresima utualika kutoa mahamuzi yetu katika
safari yetu ya imani. Katika dominika ya kwanza Adamu na Eva walichagua kifo
ambacho uonyesha kutokua na neema ya Mungu leo katika dominika ya pili,
Abrahamu anachagua uzima na tegemezi kutoka kwa Munga ndio sababu alizawaidiwa
kuwa mwenye haki na baba wa mataifa-dini. Ndio maana zaburi yetu ya leo inasema
ivi: Kwa
kuwa neno la Bwana lina adili kwetu, na kazi yake yote huitenda kwa
uaminifu...Nafsi zetu zinamngoja Bwana yeye ndiye msaada wetu na ngao yetu. Ee
Bwana, fadhili zako zikae nasi, kama vile tulivyokungoja wewe. Basi leo Mungu anatualika mimi na wewe
kuchagua na kutoa mahamuzi yetu katika safari ya kumrudia Yeye. Basi kwa Upendo
wake kwetu Mungu katika injili anatupa chaguo lenye baraka na neema tele: ndio
maana anamtubulisha Mpendwa Mungu na Masiya wetu na kutuomba tumsilkilize na
kumtafuta.
wapendwa
simulizi ya kugeuka sura Bwana wetu Yesu Kristo mbele ya wanafunzi wake watatu
mlimani Tabor ni kielelezo wazi kwa wafuasi wake kwamba mateso na utukufu
vinaambatana na hiyo ni sifa na utukufu wa Mungu. Wapendwa kabla ya tukio ya
kugeuka sura watu wengi hata mitume walikuwa bado hawajamtambua Yesu ni nani.
Yesu alipo wauliza swali “Wengi husema
Mimi ni nani?” walishindwa kulijibu swali hili kwa ufasaha. Kwa nafasi hii
mtume Petro anafanikiwa kujibu swali hilo vizuri kuwa Yesu ni Masiha, Mwana wa
Mungu baada ya kupewa ufunuo na Mungu Baba. (Mt16:13-15) Yesu anapoona wanafunzi wake wamemtambua yeye ni nani,
tukio linalofuata anawafunulia yatakayompata. Anatabiri juu ya mateso, kifo na
ufufuko wake. (Mt 16:21-22) Cha
kushangaza tena Mtume Petro hakubaliani na mpango wa Yesu kupitia mateso na
kifo cha msalaba. Basi mwishoni Yesu anahamua wazi kutoa fundisho zito kwamba
anayetaka kuwa mfuasi wake,auchukue msalaba wake na kumfuata katika njia yake ya
mateso. (Mt16:24). Basi mara baada
ya fundisho hili baada ya siku sita Yesu anawachugua Petro, Yakobo na Yohana
ndunguye huku akigeuka sura.
Ndugu
zangu basi tulifafanue tukio hili la Yesu kugeuka sura na kuona yaliyomo. Injili
iko wazi na tumesikia kuwa Yesu aligeuka sura mbele ya wanafunzi wake Petro,
Yakobo na Yohane. Tunaweza kujuliaza kwa nini awa wanafunzi watatu kila mara
wanaonekana kwenye matukio na Yesu: kwa mfano tukisoma Luka sura ya 8: 40-56 tutasikia
tukio ya uponyaji wa mwanamke alie tokwa na damu kadiri ya miaka kumi na miwili
pia Yesu anamfufua binti wa Yairo na ukiendelea hadi mustari wa 51 utasikia
ivi: alipofika
nyumbani hakuchukua mtu kuingia pamoja naye, ila Petro na Yohana na yakobo…hata
tena katika bustani ya gestemani walikuwapo… lakini tutambue kwamba tukiambatana
na kumfuate yesu tutafunuliwa mambo mengi kwa sababu Yesu katika injili ya
Mathayo sura 13:11 aliwaambia mitume hivi: Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa
mbinguni, bali wao hawakujaliwa. Na mmja ya siri ya ufalme wa
mbinguni ni tukio ya kugeuka sura Bwana wetu Yesu.
Wapendwa
katika tukio ya kugeuka sura ya Bwana wetu Yesu Kristo tutambue mambo ifatavyo:
Mosi Katika tukio la Yesu kugeuka
sura walitokea Musa na Eliya wakiwa wanazungumza na Yesu. Tunasoma katika
maandiko Matakatifu kuwa:Waisraeli waliongozwa na wingu kule jangwani(Kut13:21).
Wingu liliifunika hema ya kukutania(Kut 40:34).Pia Musa alipokea amri za Mungu
juu ya mlima uliofunikwa na wingu (Kut24:16-18) Je kiini cha mazungumzo yao
kilikuwa nini? Muenjili Luka peke yake anatujulisha kuwa walizungumza juu ya
kifo cha Yesu ambacho kingekamilishwa kule Yerusalemu(Lk.9:31). Kwa upande
mwingine uwepo wa hawa wawakilishi wawili Agano la Kale hutoa ushuhuda kuwa
sheria na manabii vinapata utimilifu katika Yesu Kristo mkombozi kwa njia ya
mateso, kifo na ufufuko wake.
Pili Wapendwa katika
hali ile ya utukufu waliyoonjeshwa wafusi wa Yesu: Petro, Yakobo na Yohane pale
mlimani, iliwavutia na kuwafurahisha sana.Wakatamani hali hiyo iwe ya kudumu
hata wakataka kubaki pale Mlimani.Rejea pendekezo la Petro,nitajenga vibanda
vitatu; kimoja chako Wewe, kimoja cha Musa na Kimoja cha Eliya. Petro kama
myaudi anakumbuka namna gani wayaudi wanavyo sherekeye sherehe ya Vidanda
katika siku sita ao 8. Katika sherehe ya vibanda wayaudi kwanza wanamshukuru
Mungu na kukumbuka ukombozi wao utumwani Misri, huku katika jangwa walijenga
vibanda na kuwasha taa wakiimba zaburi
na kucheza huku wakimsifu Mungu, kutoa sadaka na angona tena kwa Mungu pia
kumuomba na kusubiria ujio wa Masiya kwao…ukisoma Mambo ya walwi 23: 33-34,
kumbuku ya Torati 16: 13-16… sasa Yesu akagundua kwamba Mtume Petro anafunuliwa
tena na Mungu kwa mara ya pili kusudi afahamu vizuri mafumbu matakatifu lakini
bado kwanza mda wakumushudia Masiya ulikua aujafika na pili kuna kasoro katika
kuelewa kwake kuusu Masiya basi kwa ujio wa Masiya sio kwa wana waisraeli tu
kwakulinjenga hema tatu ya Yesu-Musa-Eliya lakini kwa kulihubiri injili popote
ulimwenguni. kwa hiyo anawakemea mitume watunze siri hadi pale wataimarika kwa
kushudia mateso-kufa na ufufuo wake. Na hayo hutimishwa katika injili ya Yoane
sura 7:1-4: na baada ya hayo Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya, maana hakutaka
kutembea katika uyahudi, kwa sababu wayahudi walikuwa wakitafuta kumwua. Na
sikukuu ya wayahudi, sikukuu ya vibanda, ilikuwa karibu. Basi ndugu zake
wakamwambia, ondoka hapa, uende uyahudi, wanafunzi wako nao wapate kuzitazama
kazi zako unazozifanya. Kwa maana hakuna mtu afanyaye neno kwa siri, naye mwenyewe
ataka kujulikana. Na haya tunashuhudia katika kitabu cha matendo ya
mitume mara baada ya ufufuko Yesu Kristo Petro na Mitume wenzake walihubiri
injili bila woga na kwa watu wote.
tatu kitu kingine
kinachoambatana na tukio la Yesu kugeuka sura ni sauti kutoka katika wingu: Huyu
ni mwanangu, Mpendwa, ninayependezwa naye, msikieni yeye. Wapendwa
katika Biblia neno Mwana wa Mungu ni jina alikua napewa mfalme wa wayaudi
katika Yerusalemu na mfalme kwao nimwakilishi wa Mungu pili neno Mpendwa ni
jina aliopewa Mtumishi wa Mungu. Na ukisoma Isaya 42 utasikia wimbo wa kwanza
wa mtumishi wa Bwana: Tazama Mtumishi wangu, nimtegemezaye naye,
mteule wangu, ambaye nafsi yangu imependezwa naye. Nimetia roho yangu juu yake;
naye atawatolea mataifa hukumu. Hatalia,
wala hatapaza sauti yake, wala kuifanya isikiwe katika njia yake…Bila shaka
Mtumishi wa Bwana, Mwanae Mpendwa ni Yesu Kristo na ndiye yeye Masiya wa
kwaeli. Ndio sababu Mungu anatualika kumsikiliza Yesu Masiya aliechugua hali
yetu ya kibinadamu ili atukomboe. Na haya Mitume wanaoshudia leo Mungu
aliwagizi wanawe tangu zamani. Rejea Kumbu kumbu la Torati sura 18: 15: Bwana,
Mungu Wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndungu zako kama nilivyo mimi;
msikilizeni yeye. Na mwishoni kabisa nabi Danieli anatuambia hivi: Nikaona
katika njozi za usiku na tazama, mmja aliye mfano wa mwanadamu akaja na mawingu
ya mbingu; akamkaribia huyu mzee wa siku, wakamleta karibu naye. Naye akapewa
mamlaka, na utukufu, na ufalme ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha
zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo haitapita kamwe, na
ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.
KATIKA MAISHA
Wapendwa simulizi la kugeuka
sura Bwana wetu Yesu mbele ya wafuasi wake ni ufunuo wa utukufu wa yesu atakaoupata
kwa njia ya mateso,kifo na ufufuko wake. Hali hiyo ni mwanzo wa kuimarisha wito
na imani wa mitume na kuwafanya kusudi wakuwe tayari kuyapokea, kumfuata na
kushiriki katika mateso na utukufu wa Kristo kadiri ya mpango wa Mungu Baba. Nasi
leo, tunafunzwa kuwa tayari kuyapokea mateso tunayopata katika kutekeleza wajibu wetu wa kumfuata Kristo kwa sababu
utimisho wa mateso yetu ni msalaba wa yesu unao tuletea uzima.
Kwa kushirika katika mateso
na utukufu wa Kristo ni kuwa tayari kuyabeba msalaba yetu na kuyapeleka kwa
Yesu yeye aliye itimisho wa mateso katika kuteswa, kufa na kufufuka kwake. Basi
wapendwa ,Wazazi wanahimizwa wawe tayari
kuyavumilia magumu au mateso wanayoyapata katika kuutekeleza wajibu wa kikristo kama wana ndoa pia kwa kuzingatia
malezi bora kama wazazi kwa watoto wao. Yawapasa kuvumiliana tofauti zao kitabia , kimawazo,
kiafya Pia kwa uvumilivu na saburi wanapaswa kuwatunza na kuwalea watoto wao
ipasavyo bila kukata tamaa. Lakini kumbukeni familia bila
mwongozo wa Yesu ni migogoro na ungovi kila siku.
Sisi
tuliowanafunzi ni lazima tuwe tayari kuvumilia mateso tunayoyapata katika
kuitafuta elimu na kufahamu kwamba hakuna pasaka bila ijumaa kuu wala hakuna
furaha bila mateso. Basi tuwaoneye wazazi wetu huruma na tuwape faraja kwa
kuonyesha juhudi yetu ya kuwa tayari kupambana na shule kusudi maisha yetu ya
kesho yawe mazuri. Na leo kwa namna ya peke tunakumbuka siku ya wanawake dunia,
siku kama hiyo kwenye ninyi wanawake iwe siku ya kuthamini maisha yako kwanza
kama mkristu, kama mwanamke mwanafunzi na tatu kama mama wa kesho atakaye
boresha taifa yetu nzima ya Afrika. Tutambue kwamba mwanamke akipewa elimu,
dunia inaona nuru.
Mapadre,walimu na walezi,wanawajibu mzito zaidi. Kutuandaa
sisi vijana, sisi tuliotofauti kwa vitu vingi si kitu rahisi.Wanatumia nguvu,
akili, muda, mali nk kutuunda kiroho, kiakili, kimaadili ili tukawafae watu wa Mungu na kuwaongoza
vema kwake. Ni mateso walioyonayo kwaajili ya kumfuata kristo. Basi tuwape
ushirikiano uku vile vile pia matufundishe kwa uvumilivu na upendo bila kochoka
ao kukata tama. Wapendwa katika Kristo wakati huu wa kwaresima tujitahidi
kumfuata Kristo katika njia hii ya msalaba yaani kuishi maisha ya sadaka kwa
Mungu na jirani. Tutekeleze wajibu wetu wa kikristo kwa uaminifu wote ili
jitihada zetu za kumfuata Kristo mteseka zitupatia matunda mazuri ya kwaresima
Shemasi Bienvenu Kabeya Kungwa Ngungwa Poulain Loquace, SDS
Commentaires