MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA


MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA







Somo I : Kut 12 :1-8, 11-14
Somo II : 1Kor 11 :23-26
SomoIII: Yohane 13:1-15



SALA: Tuwaombee mapadre wote ili Mungu awajalie juhudi na ujasiri wa kuwahudumia Taifa lake lote bila ubaguzi wa rangi ao wa taifa tena wabaki imara katika wito wao kila siku ya maisha yao.






UTANGULIZI

Leo Mama Kanisa anaadhimisha Alhamisi Kuu, mmja kati ya siku kuu tatu kabla ya kusherekeya mafumbo ya imani na matumaini ya wokovu wetu sisi wakristu: ndiyo Pasaka ya Kikristo yaani kuteswa, kufa na kufufuka Bwana wetu Yesu Kristu. Katika ukumbusho wa siku ya leo Bwana wetu Yesu Kristo pamoja na wanafunzi wake, saa chache kabla ya kukamatwa na kuhukumiwa kifo, alikula karamu ya mwisho. Katika karamu ya mwisho, alionyesha mfano wa kuishi Amri ya Mapendo na akaweka Sakramenti mbili muhimu kabisa ndizo: Sakramenti ya Ekaristi Takatifu na Sakramenti ya Daraja Takatifu (Upadre).


UFAFANUZI

Katika Somo la kwanza tunasikia historia ya wana wa Mungu wakiongozwa na Musa kuhusu desturi ya hizo za Pasaka: Kawaida na desturi hizo za Pasaka na za Mkate usiotiwa chachu zilikuwa kawaida mbalimbali mwanzoni. Kiwalisia Sikukuu ya Pasaka ni hasa desturi ya Wachungaji na Wafugaji wa wanyamawatoao wazaliwa wa kwanza kama sadaka. na Sikuu ya Mkate usiotiwa chachu ni desturi ya Wakulima watoao mazao ya kwanza ya ardhi kama sadaka. Punde si punde desturi hizo mbili zikaungana katika sikukuu moja. 



Lakini tutambue kuwa desturi hizo za Pasaka na za Mkate usiotiwa chachu yamepata maana mpya wakati Waisraeli kwamwongozo wa Musa walipotoka nchini Misri: na ikawa kwao ishara ya wokovu. Basi wapendwa, Pasaka ya Waisraeli yadokeza Pasaka ya Wakristo, yaani wokovu ulioletwa na Kristo: Mwanakondoo wa Mungu amejidhabihu msalabani, alijitoa kama chakula katika karamu ya mwisho katika juma la Pasaka ya Waisraeli.

Ndio maana kwetu sisi wakristu Agano Jipya ni hitimisho ya Agano la Kale: kwa hiyo Pasaka ya kiyahudi ni mwanzo wa safari ya wokovu wa ulimwengu mzima. Basi Kristo ameiletea dunia yote wokovu kwa karamu yake na msalaba wake. Kadiri ya imani yetu sisi Wakatoliki tendo lilelile la karamu na msalaba linaendelezwa na Kristo katika Misa Takatifu iliyo karamu na sadaka ileile ya Kristo.


Ndio sababu katika somo la pili Mtume Paulo anatuenyesha kusimikwa kwa sakramenti ya Ekaristi Takatifu kama wasimuliavyo wainjili. Wapendwa Ekaristi ni Karamu ya wakristo inao wakumbusha sadaka ya Yesu kama kondoo aliechinjwa kwa ajili ya utakaso wa ulimwengu nzima: kwa hiyo Ekaristi ni upendo na huruma wa Utatu Mtakatifu kwa ulimwengu pia ni ishara ya umoja na ushirika wa wakristu wote.(1Kor 10:16). Kwa hiyo Ekaristi Takatifu hutuunganisha Wakristo wote kuwa ndugu. Pia kila tunapokula vema karamu hiyo tunashiriki na kutangaza kifo na ufufuko wake Kristo.

Lakini hatuwezi kushiriki pamoja kama ndungu bila upendo, bila kiongozi kati yetu, bila msaidizi ao wasaidizi ao wahudumu... ndio maana somo letu la injili linatuonesha kwa kina juu ya uwekaji wakfu wa Ekaristi Takatifu na Daraja la Upadre na Yesu Mwenyewe: na hayo yote aliyafanya kwa upendo mkuu: kwa maneno haya “Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu”. Yesu anaweka wakfu Sakramenti ya Ekaristi Takatifu na Daraja Takatifu la Upadre. Chakula chetu cha roho cha kila siku ni Ekaristi, Wahudumu au Waandaaji ni Mapadre, wakiongozwa na sera ya Upendo.



KANINSA NA EKARISTI
Wapendwa kwanza tutambue kwamba Ekaristi hukamilisha kuingizwa katika Ukristo.Wale walionuliwa katika heshima ya ukuhani wa kifalme kwa Ubatizo na kufananishwa kwa ndani zaidi na Kristo kwa Kipaimara, hushiriki pamoja na jumuiya yote katika sadaka moja ya Bwana pia ni chemchemi na kilele cha maisha yote ya kikristo. Sakramenti nyingine, kama zilivyo pia huduma zote za kanisa za utume, zaungana na Ekaristi na zaelekezwa kwake: kwani katika Ekaristi takatifu mna kila hazina ya kiroho ya kanisa, yaani Kristo Mwenyewe, Pasaka wetu.(KKK 1322-1324)  

Tena Ekaristi ndio ishara thabiti na sababu ya hali ya juu kabisa ya ushirika katika uzima wa kimungu na umoja ule wa Taifa la Mungu ambao unalifanya Kanisa liwepo: Ekaristi ni kilele cha tendo la Mungu la kuutakatifuza ulimwengu katika Kristo, na kilele cha tendo la kumwabudu Mungu wampalo watu Kristo, na kwa njia yake wampalo Baba katika Roho Mtakatifu.(KKK 1325) Na mwishowe, kwa njia ya adhimisho la Ekaristi tunaungana tayari sisi wenyewe na liturjia ya mbinguni na tuaanza kutangulia kushiriki uzima wa milele Mungu atakapokuwa yote ktika wote.


Kwa nini sakramenti ya Ekaristi? Mwokozi wetu kama vile tulivyo sikia katika injili: katika karamu ya mwisho, usiku alipotolewa, aliweka sadaka ya Ekaristi ya Mwili wake na Damu yake. Alifanya hivyo ili kuendeleza sadaka ya msalaba siku zote mpaka atakaporudi, kusudi amwachie Bibi Arusi mpendwa, yaani Kanisa, ukumbusho wa kifo chake na ufufuko wake: sakramenti ya upendo, umoja, kifungo cha mapendo, karamu ya pasaka ambamo Kristo huliwa, na roho ujazwa neema, na ambamo tunapewa amana ya uzima wa milele.(KKK 1223)


Ndio maana yeye Mwenyewe usimika wazi sakramenti ya Upadre kwa hiyo katika utumishi wa kanisa wa mhudumu mwenye daraja, ni Kristo Mwenyewe aliye katika kanisa lake kama kichwa na mwili wake, mchungaji wa kundi lake, kuhani mkuu wa sadaka ya ukomnozi, mwalimu wa Ukweli: basi mapadre ni wahudumu wa Kristo kwa taifa lake. Wajibu huo alioutoa Bwana kwa wachungaji wa taifa lake, ni huduma halisi. Wamtegemea Krsito na ukuhani wake mmja na umewekwa kwa manufaa ya watu na jamii ya Kanisa.



UTUMISHI
Basi ndungu zangu Yesu kama Mwalimu anatoa mfano kwa kuwaosha miguu Wanafunzi wake kwa maana: kuwakumbusha watumishi wake kwa upekee na wakristu wote kwa jumla kwamba (mtumishi yaani padre kwa sakramenti ya upadre ao wakristu wote kama mapadre kwa sakramenti ya Ubatizo) lazima kuwa mdogo mbele ya watu na kuwa mhudumu wa watu bila kujidai maslai binafsi bali kuwatumikia watu bila kujibakiza hayo ndio maana ya kuwa mtumishi wa Mungu.

Basi adhimisho ya siku ya leo (Alhamisi Kuu) tunasherekeya MAMBO matatu mapya: Sakramenti ya Ekaristi Takatifu yaani Chakula cha Wakristo, Sakramenti ya Daraja Takatifu (Upadre) yaani Huduma na Amri ya Mapendo- Sera ya Kanisa. Hivyo kila mara tunapsherekeya Misa Takatifu zinazoadhimishwa na Mapadre popote duniani: tunakumbuka upendo wa Mungu kwetu kwa kutupa chakula yaani Mwanae Mpendwa, kwa kutupa wa hudumu mapadre ni mwisho kwa kutupa Amri kuu ya mapendo ambaye ni sera ya Kanisa letu: kwa hiyo tunaalikwa kuwa watu wa imani kwa Yesu, kwa kuliheshimu Kanisa na Viongozi wake na kwa kusaidiana, kuvumiliana na kupokeana sisi kwa sisi katika hali zetu zote ngumu na rahisi; tukiongozwa na sera ya Upendo.  

SHEMASI BIENVENU KABEYA NGUNGWA KUNGWA POULAIN LOQUACE, SDS


Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA