MAHUBIRI YA DOMINIKA YA 3 YA PASAKA / DOMINIKA YA EMMAUSI: KAA PAMOJA NASI EE BWANA WETU YESU KRISTO KILA SIKU YA MAISHA YETU


MAHUBIRI YA DOMINIKA YA TATU(3) YA PASAKA/ DOMINIKA YA EMMAUS: KAA PAMOJA NASI EE BWANA WETU YESU KRISTO KILA SIKU YA MAISHA YETU

MASOMO 
Somo la kwanza: Mdo 2:14, 22-28
Somo la pili: 1Pet  1:17-21
Injili: Lk 24:13-35


SALA: Ee Bwana Yesu Kristo na Mkombozi wetu, asante kwa kuwa nasi kila siku katika safari yetu ya imani katika furaha ao katika mangonjwa kwa hiyo tunakushukuru sana na kukutukuzwa basi ee Bwana utuimarishe zaidi katika imani yetu na hasa zaidi utupoe katika janga la ungonjwa wa corona.
UTANGULIZI
Wapendwa Taifa la Mungu, SHALOOM. Leo ni Dominika ya Tatu ya Pasaka na tunaendelea kusherekeya hitimisho ya Imani na Matumaini yetu kama wakristu. Yesu Kristu ambaye alishinda mauti na kufufuka katika wafu anaendelea kuimarisha imani ya wafuasi na mitume kwa kujionyesha katika matukio mbalimbali ya maisha yao: Biblia na Kadiri ya Wainjili wote wane, tunaambiwa kuwa baada ya Ufufuko wake, Yesu aliwatokea wafuasi wake mara nane(8). Na leo ni mmoja kati ya haya matokeo nane ya Yesu. Na leo Mwinjili Luka anatuonesha jinsi Bwana Mfufuka anavyowatokea wafuasi wake wawili katika kijiji cha Emmasi baada ya Ufufuko wake. Na watalamu wa Biblia uwa na buni na kusema kwamba sehemu hii ya injili ya Luka 24:13-35 inaweza peke yake kuandika tena Biblia kama Biblia ikipotea. Tena inatupatia sehemu zote ama structure ya Kanisa letu Katolika na kudokeza kila chembe za maadhimisho ya Ekaristi Takatifu. Basi wapendwa tuwe watu wa Imani hata katika shida, hofu, kifo mangonjwa na tujue kwamba Yesu yuko nasi hata katika taabu basi tuwe wakarimu na tayari kumsikiliza na kumtabua katika matukio mbalimbali tunao kutana nazo katika maisha yetu ya kila siku.
UFAFANUZI 
Wapendwa katika Kristo, tunaweza kujiuliza ni kitu gani ambacho kinamfanya Mtume Petro zaidi pia na mitume wengine kusimama imara na kumuhubiri Kristo kwa wale ambaye waliwatishia kuwauwa mara baada ya kumwangamiza kiongozi wao Yesu? Kwa sababu Petro alionesha woga hadi kumkana Yesu na kupungukiwa imani yake, ni nini leo anamfanya kuwa askari hodari wa injili bila kuwaogopa tena watu wa karne yake: wapendwa jibu sahihi ambayo lilihimarisha tena Imani ya Petro na wenzeka na pia inao tuunganisha wewe na mimi leo na kuitwa tena wateule wa Mungu ni TUKIO YA UFUFUKO WA YESU. Basi ndugu zangu ufufuko wa Yesu ni mwanzo wa maisha mapya ambao kwa njia ya ubatizo wetu tunaalikwa na mama Kanisa kuwa mashaidi wa ufufuko huo na kuwa tayari kuhuburi injili kwa mataifa yote kama wamisionari.
Ndio maana katika Somo la kwanza litokalo katika kitabu cha Matendo ya Mitume Petro na wanafunzi mitume kumi na mmoja ufafanua vizuri Tukio la Yesu kusulubishwa na kufa msalabani ambalo liliwakatisha tama wasikilizaji na wafuasi wa kwanza, kwani hawakutegemea kuwa Kristo aliyefahamika kwao kama mfalme mwenye nguvu na Mesiha afe kifo cha aibu kama kile. Ndiyo hapo Petro anapochukua jukumu la kuwajibu na kuwaeleza kuwa kifo cha Kristo Yesu msalabani ulikuwa ni mpango wake Mungu wa kuwakomboa wanadamu (Mdo 2:23). Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu na hivyo kuibuka mshindi dhidi ya mauti na dhambi (Mdo 2:23-24).
Na ni kupitia hofu, kukata tama na upungufu wa imani wa wanafunzi wa kwanza wa Yesu uliomfanya Yesu kuwatokea mitume na wanafunzi na leo katika injili Mwinjili Luka anatuonesha jinsi Bwana Mfufuka anavyowatokea wafuasi wake wawili katika kijiji cha Emmausi. Baada ya Ufufuko wake, Yesu aliwatokea Mitume na wafuasi wake maranyingi ili kuwasadikisha ya kwamba amefufuka kutoka wafu. Na pia alitaka kuwaimarisha katika imani yao ambayo ni msingi wa matumaini, sababu twatumaini wenyewe kufufuka tena baada ya kufa kwetu. Yesu amefufuka akiwa wa kwanza wa wanaolala au akiwa limbuko lao waliolaa (1Kor 15:20).
Kwa nini kila mara Mama Kanisa katika kipindi cha Pasaka uwa natupa nafasi ya kutafakari tokeo ya kujionyesha kwa Yesu mbele ya awa wanafunzi wawili?
Bila shaka Kanisa linatualika mimi na wewe leo kutambuwa kwamba imani ambayo tunaoipata kwa kuona na kuzikiliza ni mwanzo wa matumaini na imarisho ya kuweka wa missionari wa injili ya uzima yaani wa ufufuko wa Yesu Kristo. Wapendwa katika Dominika hii tutazame zaidi tokeo la Emmausi Kati ya wafuasi wawili wanaotokewa na Bwana Mfufuka mmoja anaitwa Kleopa, na mwingine hatajwi jina lake, kila mmoja wetu anaweza kuweka jina lake ili kumshuhudia Bwana Mfufuka.
Kwanza wafuasi ao wawili wanadokeza hali halisi ya maisha yetu sisi kama wanadamu kila mara tunaposhindwa katika maisha yetu: tunakata tama, tunaonyesha huzuni, hofu, aibu kwa sababu kwa akili yetu tunaona kwamba maisha yetu aina tena na thamani... ndio maana kwa yale yote yaliyotokea Yerusalemu baada ya kifo cha Kristo, baadhi ya wafuasi wake walitawanyika toka Yerusalemu na Mitume wake walikuwa wamejifungia ndani ya nyumba kwa hofu ya Wayahudi. Kifo cha Kristo kiliwafanya washindwe kuwa na Imani thabiti juu yake, kwani hapo mwanzo walimwamini kama mfalme mwenye nguvu ambaye hakustahili kufa kifo cha aibu kama hicho. Hiki ndicho kilichowafanya wafuasi hawa wawili kutoka Yerusalemu kwenda Emau. Wakiwa katika safari yao, Yesu anawatokea na anaambatana nao. Yesu anawadodosa juu ya kile walichokuwa wanaongelea. Nao wanamweleza kwa huzuni na uchovu habari za Yesu Mnazareti aliyefundisha na kutenda miujiza mingi na mwisho akatiwa mikononi mwa Mayahudi na kuuawa msalabani... basi wapendwa nawalikeni tutafakari mambo muhimu inne(4) kutoka katika injili ya leo ambao Mama Kanisa uwa nahadhimisha kila siku katika hadhimisho ya misa Takatifu:
Mosi: Njia ya Emmausi uonyesha wazi kwamba Maisha yetu yote ni safari, na katika safari hiyo tunakutana na vitisho, hofu au wasiwasi pamoja na kukata tama kutokana na ugumu wa safari hiyo na mara nyingu tunatenda dhambi kwa sababu ya upungufu wa imani. Hii ni sehemu ya toba katika hadhimisho ya Misa: ndio maana tunaanza na kuungama dhambi zetu kabla ya kusikiliza neno la Mungu na kushiriki chakula cha uzima wa milele yaani Ekaristi. Basi safari ya Emmausi inatualika sisi leo kwanza kumwambia Yesu kila kitu bila kuficha: uzinzi wetu, chuki, ugonjwa, umbea, wizi, umaskini, shida na mahakaingo zetu... pia kufanya mahungamo ya kweli mbele ya Yesu kusudi tumupe nafasi ndani kusudi aje akae nasi.
Pili: Yesu baada ya kuwasikiliza anawaonya: Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote walioyoyasema manabii. Je haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake? Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe. Sehemu hii ya pili uonyesha wazi liturjia ya neno la Mungu ambaye Muhubiri ni Yesu Mwenyewe: wapendwa tutambue kwamba kila mara padri anasoma injili na kuhubiri, kila mara msomaji anasoma somo, ni Yesu Kristo anaeye tusomea kupitia msomaji, ni Yeye Mwenyewe anae hubiri kupitia padre... basi lazima tuheshimu Neno la Mungu na kuthamini ukubwa wake katika maisha yetu: wangapi wanasoma neno la Mungu nyumbani? Wangapi leo wana Biblia? Katika simu zetu tunashindwa kuweka Biblia? Tutambuwe kwamba neno la Mungu hutufanya tumtambue Kristo katika Ekaristi basi bila neno hilo imani yetu ni bure.  
Tatu: wakakikaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, naye alifanya kama anataka kuendelea mbele. Wakamshawisi wakisema, kaa pamoja nasi... Ikawa alipokuwa ameketi nao chakulani, alitwaa mkate, akaubariki, akaumega, akawapa. Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua, kisha akatoweka mbele yao: sehemu hii ya uonyesha wazi liturgia ya sadaka na Ekaristi Takatifu. Wapendwa neno Ekaristi maana yake ni SHUKRANI, tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya Mwanae Bwana wetu Yesu Kristo, aliyekuja kutukomboa sisi wanadamu basi Ekaristi utufundisha leo kuwa wamoja na wenyi ukarimu na upendo: mara ngapi tuko tayari kupokea Ekaristi? tunapokea kwa mazoea ao tunaimani kweli yule mkate na divai ni Mwili na Damu yake Kristo? Nasi pia macho yetu yanafumbuka pale tunapopokea Ekaristi Takatifu na kumtambua Bwana Mfufuka kuwa yupo kati yetu kila siku ya Maisha Yetu katika furaha ao katika shida ao taabu.
Inne: wakaambiana, Je Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisemaa nasi njiani na kutufunulia maandiko? Wakaondoka saa ile ile.... wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli. Nao waliwapa habari ya mambo yale ya njiani... wapendwa sehemu hii uonyesha mwisho wa Misa takatifu ambalo tunatumwa na Kaanisa kila siku baada ya kuungama, kuzikiliza neno la Mungu na kushiriki Chakula cha uzima, kuwa wa missionari wa injili ya Yesu Mfufuka kwa mataifa yote kila mmoja kadiri ya jikumu lake ililolipata ndani ya Kanisa. Kuwa missionari wa Kristo ni kuwa tayari kumweka Kristo mbele ya kila kitu, kujitoa bila kujibakiza na kujali uhai wetu, kuwasaidia na kuwapa matumaini ya Yesu watu mbali mbali hususani wale walio kata tama kwa ajili ya ugumu wa maisha, shida, taabu na mahangaiko, walio achwa na kuzarauliwa na jamii, wanyonge na yatima, maskini na wakimbizi... kusudi kwa utume wako wapate kuyaonja pia utufuku na uwepo wa Mungu katika Maisha Yao. Basi wapendwa. Na mara tunapomtambua, basi tuende hima tukawapashe habari wengine ambao bado hawajui ya kuwa Bwana amefufuka na ametutokea sisi. Habari hiyo wataipokea kutokana na matendo yetu mema yanayodhihirisha uwepo wa Kristo Mfufuka ndani yetu.
Tukifanya hivyo Petro katika somo la pili anaendelea kutuonya kwamba kwa njia ya Yesu sisi tumepewa nafasi tena kumwita Mungu ‘Baba’ kwa sababu tumepokea toka kwake uzima mpya kwa damu ya thamani, kama ya mwanakondoo asiye na hila. Basi tumwamini Yesu Kristo na tumfuate kusudi tupate starehe ya milele.
SHALOOM
SHAMASI BIENVENU KABEYA NGUNGWA KUNGWA POULAIN LOQUACE, SDS

Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA