MAHUBIRI YA DOMINIKA YA MATAWI MWAKA A WA KANISA
DOMINIKA YA MATAWI AO
DOMINIKA YA MATESO MWAKA A
MASOMO

Somo I:Isa. 50:4-7.
Somo II:Flp. 2:6-11.
Injili: Mt. 26:14-27:66
SALA: Ee Bwana tunakushukuru kwa wema na
upendo wako mkuu kwa kumtoa Mwanao Mpendwa Yesu Kristu kuwa sadaka kwa ajili ya
wokovu wetu basi e Bwana tunakukabidhi watu wanaoteseka na ugonjwa wa virusi vya Korona: Ee Mungu Baba yetu pokea marehemu wote kaika ufalme wako.
UFAFANUZI WA DOMINIKA YA MATAWI
Ndugu zangu katika Kristo, tangu jumatano ya
majivu tulianza kipindi
cha Kwaresima kipindi ambacho Mama Kanisa anatualika kututafakari kwa kina
mafumbo ya wokovu wetu. Katika kipindi hiki tunaungana na Yesu katika safari
yake ya ukombozi, kwa kufunga, kusali na kutenda matendo ya huruma kwa maskini,
wanyonge na jirani zetu. Basi leo Mama Kanisa anahadhimisha Dominika ya Matawi
dominika amboyo inatuingiza taratibu katika kilele cha imani na matumaini yetu
kusudi tukumbuke na kutafakari pamoja lile fumbo la Pasaka la Bwana wetu Yesu
Kristo, yaani Mateso, Kifo na Ufufuko wake. Wapendwa, Dominika ya leo inasehemu
kuu mbili. Katika sehemu ya kwanza tunakumbuka
kuingia kwa shangwe Bwana wetu Yesu Kristo katika mji wa Yerusalemu,
akishangiliwa kama Mfalme na Masiha, na katika sehemu ya pili tunakumbuka
Mateso na Kifo ya Bwana wetu Yesu Kristo Msalabani.

Basi wapendwa sisi leo tunakusanyika
hapa kwanza kumshukuru Mungu yaani Baba, Mwana na Roho Mtakatifu kwa Upendo wao
mkuu kwetu na pia kumshangilia Yesu Kristo Masiha na Mfalme wetu ambaye kwa
Utii na Unyenyekevu wake akatwaa namna ya mtumwa, akawa mwanadamu,
alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam ya msalaba kwa ajili wa wokovu wetu
na wa dunia nzima: kwa hiyo kwa shangwe na kuimba tumtukuze na kumshangilia
nakusema: hosanna, hosanna juu mbinguni.
UFAFANUZI WA MATESO YA BWANA
Wapendwa katika Kristo, Matukio haya
mawili ya Dominika ya leo yanatuonesha wazi hali alisi, hisia, tabia maisha
yetu sisi wanadamu: wale walikuwa wakibeba matawi mikononi, wakitandaza nguo
zao, wakiimba hosanna mfalme wetu... baadaye wanakuja tena na kupiga kelele:
asulibiwe. Basi wazo hili la kukamatwa Yesu linatuingiza wazi katika sehemu
inayodokeza msingi wa pili wa Dominika ya leo. Kwanza tujiulize kwa nini Yesu
auwawe ili sisi tuokolewe? Nani alimuhuwa Yesu?
Wapendwa kanisa linatufundisha kwamba
kifo kikatili cha Yesu hakikuwa tukio lisilotakiwa, ambalo limetokea kwa bahati
mbaya, kwa kuingiliana na mazingira yasiyotakiwa, bali ni sehemu ya fumbo la
mpango wa Mungu. Na mtume Petro baada ya kujazwa na Roho Mtakatifu aliwahubiria
wayahudi wa Yerusalemu akisema: Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno
haya Yesu wa Nazareti mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu
na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe
mnavyojua, mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa.(Cfr.
Mdo 2:23 na KKK 599) ndio maana Kanisa linahimiza sana kwamba utata wa
kihistoria wa kumhukumu Yesu wadhihirika katika masimulizi ya Injili. Dhambi
yoyote ile ya binafsi ya wahusika wakuu anaijua Mungu peke yake. Hivyo hatuwezi
kuwahesabia hatia wayahudi wote wa Yerusalemu kwa jumla.(Cfr.KKK597).
Basi wapendwa wenye dhambi wote, walikuwa chanzo cha Mateso na Kifo ya Yesu. Na leo hii kila mja wetu mwenye dhambi ni kweli sababu na chombo cha mateso ya mkombozi wetu. Basi ya muhimu leo ni kwamba Je, mimi na wewe tunayatazamaje mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo na mateso yetu ya kibinadamu? Leo hii maisha yetu yamejaa na mateso ya kila hina vita, njaa, maradhi, ya kiafya kama corona virus lakini je mateso haya tunayaelewa namna gani? Na je tunayapokea kwa imani? Je, msalaba unamaana gani kwangu, kwako leo?
Basi wapendwa wenye dhambi wote, walikuwa chanzo cha Mateso na Kifo ya Yesu. Na leo hii kila mja wetu mwenye dhambi ni kweli sababu na chombo cha mateso ya mkombozi wetu. Basi ya muhimu leo ni kwamba Je, mimi na wewe tunayatazamaje mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo na mateso yetu ya kibinadamu? Leo hii maisha yetu yamejaa na mateso ya kila hina vita, njaa, maradhi, ya kiafya kama corona virus lakini je mateso haya tunayaelewa namna gani? Na je tunayapokea kwa imani? Je, msalaba unamaana gani kwangu, kwako leo?
Bila shaka Mateso ya Bwana wetu Yesu
Kristo ni ushindi dhidi ya mahangaiko, woga, shida na mashaka mbalimbali ya
maisha yetu. Kwa hakika mateso haya ya Yesu Kristo yanaimarisha na kuchochea
imani yetu hasa tukikumbuka kuwa hakuna
utukufu pasipo mateso; mateso na utukufu vinaambatana pamoja. Mateso ya
Bwana wetu Yesu Kristo yabadili muono na mtazamo wakibinadamu, kwani Yesu
hatishwi na chochote anakwenda Yerusalemu huku akijua itampasa kukamatwa na
kuteswa ili atukomboe mimi na wewe wadhambi. Yesu anajua kwa hakika thamani ya
roho zetu ndio maana kuteswa, kutemewa mate, kupigwa mijeledi na kuchomwa ubavu
kwa mkuki kwake hayo si kitu ila roho yako na yangu zipate kupona. Kwa upendo
wake kwetu ameamua kuuacha utukufu na kuishi maisha duni ili atukomboe kupitia
njia hii ya msalaba.
Basi wapendwa msalaba kwetu ni
ishara ya ushindi, ishara ya umoja, ni ishara ya upendo ambao hauwezi
kwesabika: kwa hiyo sisi kama wafuasi wake inatupasa kuisha katika umoja,
katika kuvumiliana na katika unyenyekevu. Labda msalaba wako ni uwongo na
majungu katika jumuiya, labda msalaba wako ni utamaduni na mila na desturi yako
katika jumuiya yetu, labda wewe ni zarawu na kuwahonea wengine… lakini Yesu anatuku,busha
mimi na wewe leo kuwa sadaka kwa wenzentu huku tukisaidiana kama jumuiya pamoja
kuchugua misalaba yetu na kuyapeleka kwa Yesu. Lakini kumbuka, kama mateso haya
tunayapokea kwa imani yanathamani kubwa, kwani tutayapokea kwa uvumilivu, upole
na kwa kuwajali wale wote wanaoteseka na kwa mateso hayo tutapata faida zaidi
kiroho na kimwili.
Wapendwa katika Kristo, tumwombe
Mungu atujalie moyo thabiti na wa ujasiri wa kuyapokea mateso kama Kristo
katika maisha yetu ili yatuimarishe na kutunganisha zaidi na Kristo
aliyevumilia mateso kwa ajili ukombozi wetu.
Shemasi Bienvenu Kabeya Ngungwa Kungwa Poulain Loquace, SDS
Commentaires