MAHUBIRI YA DOMINIKA YA SITA YA PASAKA MWAKA A WA KANISA/2020
MAHUBIRI YA DOMINIKA
YA SITA YA PASAKA MWAKA A WA KANISA/2020: YESU ALISEMA: MTU AKINIPENDA,
ATALISHIKA NENO LANGU, NA BABA YANGU ATAMPENDA NASI TUTAKUJA KWAKE
MASOMO
SOMO I: Acts8:5-8, 14-17
SOMO II: 1Pet. 3: 15-18
SOMO III: John 14: 15-21
SALA: Tumuombe Mungu Baba Mwenyezi, kwa
nguvu ya Mungu Roho Mtakatifu, awasaidiye wale wote ambao wanajitahidi kutafuta
dawa ya ungonjwa huu wa corona waweze kufanikiwa ili Dunia yetu ipate amani na
faraja ya Yesu-Kristo Mfufuka katika wafu na Mkombozi wetu. Tunaomba hayo kwa
njia ya Kristu Bwana wetu. Amen.
UTANGULIZI
Wapendwa Taifa la Mungu, SHALOOM:
leo ni Dominika ya 6 ya Pasaka Katika Mwaka A wa Kanisa letu Katoliki la Roma. Wapendwa
taratibu tunaelekea kuhitimisha Pasaka yetu ambao tunamsherekea Kristu, yaani
Mungu na Mkombozi wetu alieshinda mauti kwa kufufuka katika wafu. Basi tukiwa
na nia hiyo tuungane na masomo yetu la Dominika hii ya 6 ambao inadokeza ujio
wa Msaidizi ambaye Kristu alituahidi mara kabla ya kufa kwake. Na Msaidizi huu
ni MUNGU ROHO MTAKATIFU, yaani ROHO wa kweli
ambaya atakuja kutuimarisha zaidi kiimani. Tutambue ya kwamba ujio wa Roho
Mtakatifu aimanishi ya kwamba tunaanza tena ukurasa mpya wa wokovu wetu, APANA. Lakini Roho Mtakatifu: ni wakili, Msaidizi na
Mshauri...anafanya kazi ileile kama Kristo. Maana yake Yeye ni Nafsi kama
Kristo, ambaye anatuongoza kwenye kweli yote(Jn 16:13) na anamshuhudia Kristo.(Jn10:25,
15: 26 na tena 16: 8) Basi ndungu zangu, tukiwa na dhamira hiyo tumuombe Munga
katika Dominika hii kusudi tujiandae kiroho vizuri ili Roho huyu tuliempokea
siku ya Ubatizo wetu na kuimarishwa zaidi siku ya Kipaimara(confirmation) adumu
ndani mwetu kama Msaidizi-Mungu ambaye utuonyesha na kutupeleka katika njia ya
ukweli na ya imani ya wokovu wetu.
UFAFANUZI
WA MASOMO
Wapendwa, katika somo la kwanza
tunasikia ya kuwa Filipo kwa uweza wa Roho Mtakatifu na mara baada ya
kushuhudia UFUFUKO wa Kristo, Filipo anamuhubiri Kristo. Wapendwa zawadi ya
Roho Mtakatifu ambaye kitabu cha Matendo ya Mitume uongelea, utuonyesha wazi
kuzaliwa kwa jumuiya(Kanisa la mwanzo) ambayo mwandishi Luka hutabiri kuwa
jumuiya ya kimataifa ambayo imejijenga siku kwa siku kwa mafundisho ya Yesu na
kwa nguvu na msaada wa Roho Mtakatifu. Ndiyo maana katika somo letu la kwanza
tunasikia mji wa Samaria ambalo ulihazibiwa na kutengwa na wayahudi kwa sababu
ya dhambi ya kila ina, leo umekubali Neno la Mungu kwa hiyo kuneemeka na kubarikiwa
hadi kujaliwa Roho Mtakatifu.
Katika somo hili la kwanza ni
vizuri kutambuwa kwamba kazi ya wokovu ya wanadamu ni ya Mungu tu. Sio kazi ya
wanadamu wala ya wale walioteuliwa na Mungu kwa ajili ya kulihubiri injili. Swali
la msingi kwetu leo ni kwamba: kweli mimi baada ya
ubatizo wangu, mimi kama mkristu, na muhubiri huyu Kristu kwa watu katika
kweli? Ni ishara gani ambalo watu wale watahubiriwa itokalo katika mahubiri
yangu itawafanya wavutiwe zaidi na Kristo? Bila shaka matendo na
mwenendo wangu, wako ao wetu ni chimbuko ya kuwavuta wengine kwa Yesu. Kama leo
hii tunashindwa kuonyesha huruma kati yetu sisi kama wakristu, tunashindwa kusaidiana,
tunashindwa kuishi uwaminifu katika ndoa yetu, wito wetu katika mahusiano yetu
bila shaka tutashindwa kumuhubiri Kristo kwa ukweli na madhara yake ni kuwa
watu wengine wanaweza kushindwa kuzikiliza Neno la Mungu kwa kasababu ya tabia
na mwenendo wetu mubaya. Basi kila mmoja wetu ni mtume wa Kristu, ni muhubiri
wa Kristo basi tutafiti kwanza maisha yetu kusudi Roho wa Kweli aje ndani mwetu
kutusaidia kila siku katika utume wetu, familia na shuguli zetu za kila siku
ili kwa matendo, mwenendo na mifano yetu wengine wavutiwe na Kristo.
Ndiyo maana katika injili Yesu aliwambia
wafuasi wake na anatuambia sisi leo: Mkinipenda,
mtazishika amri zangu. Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine,
ili akae nanyi hata milele, ndiye Roho wa Kweli... sitawaacha ninyi yatima... wapendwa mara nyingi tunakutana na changamoto nyingi
sana kuusu hali(nature) ya Roho Mtakatifu. Yesu Mwenyewe leo umwita MSAIDIZI
MWINGINE maana MSAIDIZI KAMA YEYE, ambaya atakaa nasi hata milele. Basi wapendwa
Roho huyo ni Mungu ambaye pamoja na Mungu Baba na Mungu Mwana(Kristo) hutimisha
kazi ya wokovu wetu na hii ndio fumbo ya imani ya Kanisa letu: yaani Mungu
Mmoja katika Nafsi Tatu. Basi tusitumiye vibaya tafsiri ya
Biblia wala tusishindwe na mafundisho nyengine ambayo utuonyesha ya kuwa binadamu
anaweza kukushushia Roho Mtakatifu ndani yako lakini tukishika amri ya Mungu na
kuishi kiaminifu kila siku ya maisha yetu: Yesu
atamwomba Baba, naye atatujalia Msaidizi yaani Mungu Roho Mtakatifu.
Katika imani yetu sisi wakristu
wakatoliki, uzawaidiwa na Mungu Roho Mtakatifu siku ya Ubatizo wetu na
uimarishwa zaidi siku ya kipaimara(confirmation) maana yake atuna budi tena leo
kuzurula na kutangatanga kutafuta tena Roho Mtakatifu bali cha msingi wewe na
mimi leo tunatakiwa kuishi katika imani ya kweli kusudi tupate kuona nguvu ya
Roho huyu ndani ya maisha zetu, ndani ya familia yako, ndani ya kazi na shuguli
zetu. Wapendwa kwa sababu ya upungufu wa imani yetu sisi leo tunashindwa kutambuwa
msaada wa Roho Mtakatifu ndani ya maisha yetu. Kama kila siku tungelikuwa
nafanya tafakari(meditation) ya maisha yetu tungetambua kweli Roho huyu
anafanya mambo mengi sana ndani mwetu lakini sisi atuyaoni kwa sababu ya mazoea
ya maisha yetu:
Leo hii labda ulisafiri, ukivaa
barakora(mask) na kuzingatia ushauri wa wahudumu wa afya na kazalika... na
unaitimisha safari yako bila kupata ajali wala mahambukizi ya corona lakini
unajisifia kwamba nilifanya service nzuri ya gari yangu, huyu dereva mzuri
sana, nilijikinga vizuri kwa kutumia barakora kwa hiyo unachukulia kawaida kila
tukio...lakini kumbuka kuko wale wengine binadamu kama wewe, waliozingatia kila
kitu kama wewe lakini leo wametoweka kwa ajali, kwa ungonjwa wa corona... labda
leo unaishi peke yako na watoto inawezekana mume ao mke wako kashafariki ao
mumeshatengana, lakini watoto wanapata elimu, matibabu wanakuwa vizuri bila
changamoto yeyote lakini unajisifia kwamba kazi yangu ni nzuri sana yaani na
pambana sana mimi ni shujaa...ni vizuri. Lakini tambuwa kwamba kuna wale
waliojaliwa elimu kubwa kuliko wewe, kazi nzuri kuliko ya kwako leo wameshindwa
kufanya kazi kwa sababu ya ungonjwa fulani, kwa sababu ya vita na migogoro ya
kila siku.... basi nilazima kumshukuru Mungu ambaya kwa Nguvu ya Roho Mtakatifu
wewe leo umeitwa baba ao mama wa mtu fulani...
Basi ndungu zangu kutambuwa uwepo
wa Roho Mtakatifu ndani mwetu ni kujipimi kiroho kupitia sala. Bila sala sisi
kama wakristu hatuwezi kufanyikiwa. Katika sala tunaboresha mahusiano yetu na Mungu
pia tunampa tena nafasi Roho Mtakatifu atuimarishe zaidi. Katika sala tunakomaa
zaidi ki imani na tunajaliwa vipaji vya Roho Mtakatifu kwa ajili ya kulijenga
kanisa lake Kristu basi wapendwa nilazima kutenga mdaa kidogo hata dakika tano
tu kumshukuru na kumwomba Mungu kwa Nguvu ya Roho Mtakatifu tustawi katika
neema na imani.
Ndiyo sababu Mtume Petro katika
somo la pili utukumbusha leo kwamba tuwe tayari
sikuzote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu,
lakini kwa upole na kwa hofu.(1Pet.3:15ff) maana yake hatuna budi ya
kuwaogopa maadui zetu ambayo wanaweza kuuwa miili yetu kwa sababu ya Kristu
lakini tubaki imara na kuwajibu nguvu ya tumaini lililo ndani mwetu ambayo ni UFUFUKO WA BWANA WETU YESU KRISTU: kwa hiyo nilazima kuwa na dhamiri njema, ili katika neno lile
mnalosingiziwa, watahayarishwe wale waukutano mwenendo wenu mwema katika Kristo.
SHALOOM NA DOMINIKA NJEMA
SHEMASI BIENVENU KABEYA NGUNGWA
KUNGWA POULAIN LOQUACE, SDS
Commentaires