MAHUBIRI YA DOMINIKA YA TANO (5) YA PASAKA MWAKA A WA KANISA : YESU KRISTO NI NJIA, NI UKWELI NA NI UZIMA


MAHUBIRI YA DOMINIKA YA TANO (5) YA PASAKA MWAKA A WA KANISA : YESU KRISTO NI NJIA, NI UKWELI NA NI UZIMA
MASOMO


Somo la I: Mdo 6:1-7
Somo la II: 1Pet 2:4-9
Somo la III: Yn 14:1-12

SALA: Kwa maombezi ya Mama yetu Bikira Maria, tusali kwa ajili ya wahudumu wote wa afya ambao wanajitoa bila kujibakiza hadi kuhatarisha uhai wao kwa ajili ya kuwahudumia wangonjwa wote hususani wale waliohasirika na ungonjwa wa corona-Cov-19 na pia tujiombee sisi wenyewe ili Yesu-Kristo Aliye Njia-Ukweli-Uzima atuongoze kwenye njia bora na kutufundisha ukweli na mishoni atupe uzima wa milele. Anayeishi na Kutawala daima na milele. Amen
UTANGULIZI
Wapendwa Taifa la Mungu shaloom. Leo tunaadhimisha dominika ya 5 ya Pasaka katika mwaka A wa Kanisa. Na Neno la Mungu leo utualika sote kumtambua, kumfuata na kumutumainia Yesu Kristo ambaye anajifunua leo kwetu kuwa Njia-Ukweli-Uzima. Leo Yesu anatufundisha kwamba tusiogope wala tusihofu kila mara tunapo kutana na shida, mahangahiko, mangonjwa, changamoto mbali mbali bali tutambuwe ya kwamba Yeye Ndiye Njia ya mafanyikio yetu, Yeye Ndiye Ukweli wa maisha yetu, mateso na shida zetuvna Yeye Ndiye Uzima wa familia zetu, wa mangonjwa yetu… Basi wapendwa tusihangaike na kutanganga, kuzurula kutafuta njia, ukweli na uzima ambao utokao kwa wanadamu lakini Yesu anakutaka wewe utakaye soma mahubiri hii ubadilishe mtazamo wako pia uwe tayari kumpa Yesu nafasi katika maisha yako, moyo wako, familia yako, mipango, shida, furaha, mateso na changamoto zako. Kwa hiyo tutajaliwa Uzima tele (Cf. Jn10 :10) tutaonyeshwa ukweli na mwisho tutafunguliwa njia ya uzima wa milele.
UFAFANUZI WA MASOMO YETU TATU
Wapendwa somo letu la kwanwa kutoka katika kitabu cha Matendo ya Mitume utuonyesha wazi namna gani Mitume kwa uweza wa Roho Mtakatifu walilijenga Kanisa la Yesu kwa matakwa yeke Mwenyewe. Kwanza Mitume wilijagua kiini cha imani yao yaani Neno la Mungu. Wakisema: haipendezi sisi kuliacha Neno la Mungu na Kuhudumu Mezani. Mitume waligunduwa na kusikiliza manung’uniko ya wayahudi wa kiyunani juu ya waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku. Na hapo walipendekeza kuwachagua watu saba miongoni mwao lakini washuhudiwe kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima kusudi waweze kuwazaidia...
Wakawchagua: Stefano, Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena na Nikolao basi Mitume wakaweka mikono juu yao. Wapendwa, katika desturi na mapokeo ya Kanisa letu Katoliki somo hili utuonesha wazi uwepo wa mashemasi ndani ya Kanisa: mashemasi wapo kwaajili ya kuwasaidia maaskofu na mapadre pia kuwahudumia watu na mara nyingi somo hili linasomwa wakati wa upadirisho wa mashemasi basi pia leo tuwaombeye mashemasi wetu wa mpito ao wakudumu wote kusudi Mungu azidi kuwaimarisha katika kazi ya huduma wao.
Wapendwa somo hili utuonyesha wazi changamoto tunazo kutana nazo katika vikanisa vyetu. Leo viongozi wengi wa vikanisa vyetu, wanajenga imani na matumaini yao katika hela na mali ya dunia na kuwahudumaza waamini yao na mbaya zaidi kuwagawanya wakristu matajiri juu ya masikini na kusau kulihubiri habari njema ambaye ni Kristo Mwenyewe. Leo hii tunafundishwa na wachunganji waovu kwamba pale ambapo unatoa kiasi kikubwa cha hela basi utabarikiwa zaidi na Mungu... kumbukeni kwamba dominika ya 4 ya Pasaka Yesu alituharifu tuwe makini kwani wachungaji waongo wapo na wanatupotosha(Jn10:1-10) kwa hiyo wapendwa, wewe ambaye utusoma mahubiri haya tambuwa kwamba Kanisa letu litastawi pale ambapo kila mmoja wetu atajitambuwa kuwa jiwe lijengalo Kanisa ambalo Kristo Mwenyewe Ndiye Jiwe la Msingi. 
Ndio maana katika somo letu la pili, Mtume Petro utualika tumwendee Yesu, Jiwe lililo hai na uzima... Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmjengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtkatifu, mtoe sadaka za roho, zinazokubaliwa na Mungu, ka njia ya Yesu Kristo. Basi ndugu zangu, mimi na wewe tunaalikwa kwanza kusafisha mioyo yetu na kuitoa kama sadaka kwa Yesu. Tambuwa, utajiri wako sio funguo ya ufalme wa mbinguni pia vile vile umasikini wako sio funguo ya uzima wa milele lakini utayari wako wa kumfuata Yesu na Kumwamini ni mwanzo wa wokovu wako. Hata katika maisha ya ndoa: utajiri ao umasikini sio ufunguo wa kuwa na ndoa nzuri ama wa kuishi kwa amani na furaha katika ndoa bali masikilizano, uvumilivu, ukweli, huruma, kujali na kumwamini mwenza wako ni mwanzo wa kuishi maisha ya raha katika ndoa yenu... hayo yote yatakuwa kwetu somo pale tu tutampa Yesu nafasi apenye mioyo yetu.
Ndio sababu Injili yetu ya leo kutoka kwa Yohane sura ya 14:1-12 utuonyesha wazi kwamba Yesu-Kristo Ndiye: Njia-Ukweli-Uzima: sura hii ya 14 ya injili ya Yohane inatanguliwa na mafundisho ya Yesu ambao aliyatoa katika adhimisho ya Karamu yake ya Mwisho tusomavyo katika sura ya 13 ya injili ya Yohane: Yesu baada ya kutambuwa kwamba saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, aliwapa mafundisho kuusu upendo, na kuwaambia yatakayompata yaani mmoja wao atamsaliti, habari ya kuondoka kwake na utabiri wake kuwa Petro atamkana, wanafunzi wake wanajawa na wasiwasi na kujiuliza maswali mengi. Lakini Yesu baada ya kuwafundisha alitambuwa kwamba wanafunzi wake walishikwa na hofu na wasiwasi ili kuwaondoa wanafunzi wake wasiwasi na kuwaimarisha katika imani Yesu anawaambia wasifadhaike:kwa sababu mnamwamini Mungu, niamini na Mimi. Yesu aliwaambia hivi kwa sababu alijua kuwa yuko njiani kuelekea nyumbani mwa Baba ambomo mna makao mengi na ni Yeye Peke yake ambaye utuandalia mahali, basi Tomaso anapata mashaka juu ya njia ya kufika huko aendako Bwana, ndipo yesu anasema “Mimi Ndimi Njia, Ukweli na Uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya Mimi”. Filipo pia akamwambia, Bwana utuonyesha Baba, Yatutosha. Yesu akamwambia: “Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi sote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona Mimi amemwona Baba...
Wapendwa mimi na wewe leo tunao sababu ya kumshukuru Mungu kwa sababu uwepo wa Yesu kati yetu, mateso, kifo na kufufuka kwake ndiyo habari njema na ya furaha inayotupa amani, imani, utulivu na matumaini katika mioyo yetu na pia inatupa nguvu na ujasiri wa kuendelea kukabiliana na changamoto na magumu katika kumfuata Kristo aliye Njia, Ukweli na Uzima. 
Kwanza tutambuwe kwamba Mitume walipata shida namna ya kuyaelewa mafundisho ya Yesu kwani fumbo kuu la kifo na ufufuko wake lilikuwa halijatimia. Ndio maana baada ya kushudia ufufuo wa Yesu Mitume walisimama imara na kuhubiri bila woga. Sisi leo hatupaswi kuwa na wasiwasi Yesu anasema kuwa ni Njia ambao Yeye mwenyewe kwanza alipita kwa mateso, kifo hadi ufufuko wake. Pili Yesu anasema Yeye ni Ukweli kwa sababu uwepo wake kati yetu ni baraka tosha, ni uponyaji, ni utajiri, mwangaza... na tatu Yesu anasema yeye ni uzima kwa sababu Yeye alishinda mauti na Kufufuka katika wafu. Yesu ni Alpha na Omega, Yesu ni Mzima jana leo na kesho na kwa njia ya ubatizo wetu sisi sote tunaonyeshwa njia na ukweli na tumekimiriwa uzima wa milele, pia kwa neema na huruma ya Mungu tonapoamua kumfuata kwa ukweli na uhuru tunafunguliwa njia na kujaliwa uzima na ukweli na mwisho tunatumaini kuingia katika utukufu wa milele ambaye Yesu Kristo uenda kutuandalia mahali.
Kwani sasa tunahangaika na kutafuta njia za mkato? Kwa nini tunatafuta ukweli utokalo kwa wanadamu kama sisi? Kwa nini tunatafuta uzima wa mda mfupi? Kwa nini tunaamini maneno na mafundisho ya uwongo?
Tuliambiwa kupitia mitandao ya kijamii(facebook, whatsapp…audio zikizunguka apa na pale) kwamba kuanzia tarehe 8 hadi 11 ya Mwezi huo wa Tano mwaka 2020 kutakuwa na giza kubwa: ma mashetani watazunguuka na kutafuna watu wa Mungu... na tukaambiwa tununuwe chakula, mishumaa na mkaa kwa sababu giza itakuwa kubwa mno zaidi...chakushangaza wakristu wengi waliogopa na kuanza kujiuliza na kutafuta msaada kwa wale wachungaji waovu... leo ni tarehe 9 bado mimi sijaona giza wala wale mashetani.... sasa ndugu zangu jenga imani yako katika Yesu-Kristo epukana na mafundisho ya upotovu, umupe nafasi leo Yesu Kristo apenye roho yako, ndoa yako, shida yako, mchumba wako, watoto wako, mahangaiko yako, mateso, furaha, magumu na kazalika utaonyeshwa njia ya kweli, utajaliwa kutambuwa ukweli na kukirimiwa uzima. 
Tusitafute miujuza itokalo kwa watu wanao tuvizia kiimani kusudi watajirike... leo corona-cov-19 inaweza kutupa fundisho kubwa kwa sababu wale walijidai kuwafufua watu leo mujiulize kwa nini wanashindwa kuwaponya wangonjwa wa corona na kutupatia dawa lakini wanabalisha misemo eti Mungu amekasirika, Mungu ametupiga, Mungu ametuazibu.... huku wakiwadai sadaka na michango kusudi Mungu atuhurumie.... Hayo yote ni UWONGO na WIZI. Tutambue kwamba Mungu wetu anatupenda na bado yuko nasi kila siku katika Maisha Yetu: Upendo wake na Uponyaji wake kwetu ni Uwepo wa Yesu Kristo kati yetu ambaye alishinda Mauti na kutuonyesha Njia sahihi ya Kwenda kwa Baba Aliye Ukweli na Uzima. 
Magumu, matatizo, shida na mateso ni sehemu ya maisha yetu ya kikristo kwani yeye Aliye Njia, Ukweli na Uzima alipambana nayo hata akakubali kufa msalabani ili mapenzi ya Baba yatimie. Tusiwe na mashaka wala wasiwasi tunapopata magumu au mateso hayo na kuona kama tumepotea njia bali tujitahidi kuyaweka yote katika Kristo na kujiaminisha kwake Yeye Aliye Njia, Ukweli na Uzima.
SHALOOM
SHEMASI BIENVENU KABEYA NGUNGWA KUNGWA POULAIN LOQUACE, SDS




Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA