MAHUBIRI YA JUMAPILI YA 4 YA PASAKA MWAKA A WA KANISA 2020/ DOMINIKA YA MCHUNGAJI MWEMA: DOMINIKA YA MIITO TAKATIFU


MAHUBIRI YA JUMAPILI YA 4 YA PASAKA MWAKA A 2020/ DOMINIKA YA MCHUNGAJI MWEMA: DOMINIKA YA MIITO

MASOMO
Somo la kwanza: Mdo. 2: 14a, 36-41
Somo la pili: 1Pet 2: 20b-25
Injili: Yohane 10: 1-10


SALA: Ee Mungu Baba yetu Mwema, tunakushuru sana kwa kutulinda wiki nzima, kwa kutulisha na kutuopoa katika shida mbalimbali, tunakuomba tena hasa zaidi kwa maombezi ya mama yetu Bikira Maria katika mwezi huo wa rosari takatifu, utuzaidie kusudi kila mmoja wetu kadiri ya uweza wa Roho Mtakatifu aweze kutambua wito wake na awe kweli mchungaji Mwema wa Dunia nzima pia utusaidie kulishinda hili vita litokalo katika janga la virusi vya corona. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amen.
UTANGULIZI
Wapendwa leo tunaadhimisha Jumapili ya 4 ya Pasaka inaofamika kama Jumapili ya Mchungaji Mwema. Yesu leo anatupa tena picha nyingine ya ukombozi wake akijionesha kwetu kuwa Mchungaji Mwema ambaye anayefahamu kondoo wake huku anawaita, anawalisha, kuwaongoza na kuwalinda. Basi kama Yeye ambaye ni Kichwa la Kanisa letu Ndiye Mchungaji wetu Mwema, Kanisa inatupa nafasi leo ya kuombea miito Duniani ili tupate wachungaji wema.
UFAFANUZI
Wapendwa imani ya Petro na wenzeka na pia inao tuunganisha wewe na mimi leo na kuitwa tena wateule wa Mungu ni TUKIO YA UFUFUKO WA YESU. Mungu kwa Nguvu ya Roho Mtakatifu alimfufua Yesu katika wafu na Roho Huyu huyu anawafanya Mitume leo kuwa kweli mashaidi wa habari njema, habari ya wokovu ambaye ni Yesu Kristo Mwenyewe. Basi ndugu zangu ufufuko wa Yesu ni mwanzo wa maisha mapya ambao kwa njia ya ubatizo wetu tumejaliwa neema tena ya kuitwa na Yesu kusudi tuingiye katika zizi lake, kulishwa pia kuongozwa na Yeye Mwenyewe ambaye tunamshuhudia leo kuwa Mchangaji wetu Mwema pia kwa njia ya Ubatizo na Kipaimara tunajaliwa utakaso na vipaji vya Roho Mtakatifu na tunaalikwa na mama Kanisa kuwa mashaidi wa ufufuko huo na kuwa tayari kuhuburi injili kwa mataifa yote kama Mitume.
Ndio maana katika somo la kwanza mtume Petro na wale kumi na mmoja siku ya Pentecoste mara baada ya kupokea Roho Mtakatifu walisimama Imara na kuwahubiria watu kuusu habari ya Wokovu ambayo itokalo kwa Yesu Kristu Mchungaji wetu Mwema: Petro aliwataka watubu pia wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo, kusudi wapate ondoleo la dhambi ili wapate kipawa cha Roho Mtakatifu. Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao na kuonesha nia ya kubadilisha maisha yao basi kwa neema ya Mungu walibatizwa na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.
Basi wapendwa mimi na wewe leo ni vizuri mahubiri ya Petro na wale kumi na mmoja yachome mioyo yetu kusudi kila mmoja wetu atambuwe mapungufu yake na aweze kutubu ili nasi pia Roho Mtakatifu ambaye tulimpokea siku ya ubatizo wetu na kuimarishwa zaidi siku ya kipaimra azidi kukaa ndani yetu. sisi wakristo kwa ubatizo wetu tumefanywa kuwa makuhani, wafalme, na manabii. Kama makuhani inatupasa kumtolea Mungu sadaka na kuwatakatifuza wenzetu kwa sala zetu. Vilevile kama wafalme tumeshirikishwa katika utawala wa Mungu ambapo Kristo ndiye Kichwa chetu na Mchungaji wetu Mwema. Na kama manabii inatupasa kumuhubiri Kristo Mfufuka… lakini tutambuye bila Nguvu na Msaada wa wa Roho Mtakatifu hatutaweza chochote bali licha ya kumuhubiri huyu Kristo tutawahubiria watu kadiri ya maslahi yetu binafsi.
Ndio sababu Katika Injili Yesu anatupa tahadhari ya kuwa tuwe makini na kutambuwa kuwa: Yeye asiyeingia mlangoni katika zizi la kondoo, laikini akwea penginepo, huyu ni mwivi naye ni mnyang’anyi lakini aigiaye mlangoni ni mchungaji wakondoo… na mwishoni wa Injili Yesu anajitambulisha kwetu kuwa Yeye Ndiye Mlango wa Kondoo, Yeye Ndiye Mchungaji Mwema, na yeyote ataingia kwake, atapata malisho, ulinzi na mwishoni atajaliwa wokovu yaani Uzima tele. Wapendwa kwanza nivizuri kutambuwa kuwa katika Agano Lakale Mchungaji ni Mungu Baba, na kondoo, ni Taifa nzima la Israeli ambalo kwa ulinzi wa wafalme wao na manabii walimlulia Mungu katika shida Naye aliwasikiliza na Aliwakomboa.
Lakini kupitia manabii wale wale Mungu alihahidi ujio wa Masiha ambaye atakuja kuwakombowa watu wake wote na kutakasa tena ulimwengu na viumbe vyote: Huyu ni Yesu ambaye Petro katika somo la kwanwa anawahubiria wana Israeli ya kuwa: tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo… kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa Watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu Wetu wamjie. Maana yake atuna budi kuzurula na kuhangaika kutafuta wachungaji wengine isipokuwa Yeye alie fufuka katika wafu. Na hiyo inadhibitishwa katika waraka kwa Waebrania sura 1: 1-2: Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mriithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.
Pili Yesu anajitambulisha kwetu leo kuwa Yeye Ndiye Mlango wa zizi la kondoo, Yesu anasema hivyo kasababu tu anajuwa kuwa Yeye na Babake wanaisha katika umoja usiovunjika na umoja huo ni upendo na uzima ulio kati yao. Sisi tunaunganishwa kwa uzima huo kupitia Yesu. Manake Yesu ni njia ambayo utuunganisha sisi wanadamu na Mungu na Yohane katika injili yake utuonyesha wazi kwamba Yesu ni Njia, Uzima na Ukweli.
Tatu kama leo Yesu Mchunganji Mwema anatuita sisi kwa majina yetu ni kwa sababu Mungu Baba alimpa Jina, jina la upekee ambalo limeandikwa katika kitabu cha uzima. Na Paulo Mtume katika waraka wake kwa Wafilipi sura 2: 9-11: Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina, na kwa jina la Yesu kila koti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana kwa utufufu wa Mungu Baba. Pia kama Yesu leo anatualika kusikiliza sauti yake na kumfuata ni kwa sababu Yeye kwanza alisikiliza sauti Baba na kufanya mapenzi yake.
Na mwishoni kabisa Yesu anatuhahidi uzima wa milele na kutukomboa kwa sababu kwa Nguvu ya Roho Mtakatifu Mungu alimtukuza kutoka katika wafu kusudi mimi na wewe leo tupata ondoleo ya dhambi na tujaliwe uzima wa milele.
Basi ndugu zangu Dominika hii ya leo inatualika sisi sote, kila mmoja kadiri ya utume na nafasi yake ndani ya Kanisa na Dunia kuchunguza na kutafiti wito wake huku tukitafakari maneno ya Yesu ambayo utuonesha wazi tofouti kati ya Mchunganji Mwema na wachungaji wengine waovu. Kila mmoja wetu ni mchungaji, lakini tujiulize sisi ni wachungaji wa namna gani? Kweli tunafahu kondoo zetu? Tuko tayari kuwahudumia na kuwalinda? Ya muhimu kwetu ni kuwa Yesu Kristo Ndiye Mchungaji wa kondoo lake sisi ni vibarua tu amboya tumeshirikishwa na Yesu kwa upendo wake Mwenyewe. Basi tusididai mno kuusu uchungaji tuliopewa bure bila malipo wala rushwa Lakini tutambuwe kwamba bila Nguvu Yake Mwenyewe na Nguvu ya Roho Mtakatifu, bila chembe ya upendo, unyenyekevu busara na uvumilivu sisi hutuwezi kuitwa wachungaji wema bali tutawanyanyasa kondoo na ku wapoteza. Tena wito wetu tunaupata katika zizi lake Mwenyewe yani Kanisa letu ambaye Kristo ni kichwa maana yake kusikia na kufuata sauti ya Kristo Mchungaji Mwema ni kuwa tayari bila kujibaliza kumruhusu Roho Mtakatifu atuvute na kutuongoza kwenye Maisha ya Kristo na mafundisho ya Kanisa kusudi tumshe ndani yetu tamaa, furaha na ujasiri wa kujitowa wenyewe na Maisha yetu kwa ajili ya jumuiya yetu, familia zetu na mwishoni kwaajili ya utumishi wa Ufalme wa Mungu.
Ndio maana Katika somo pili mtume Petro anatuasa kubaki katika imani yetu hata kama ni katika mateso makali. Tunaaswa tuvumilie mateso, na tumwamini na kumtegemea Mungu katika shida na raha hususani janga hili la corona leo. Mateso yasiwe chanzo cha kutufanya sisi tutende dhambi. Inatupasa tumwige Bwana wetu Yesu Kristu ambaye pamoja na kwamba hakuwa na dhambi, alivumilia mateso makali ili aweze kutukomboa kutoka katika utumwa wa dhambi. Hivyo Bwana wetu Yesu Kristu ni kielelezo cha maisha yetu kinacho tuelekeza kwa Mungu.

Shemasi Bienvenu Kabeya Ngungwa Kungwa Poulain Loquace, SDS




Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA