MAHUBIRI YA SHEREHE YA ASCENSION- KUPAA BWANA: DOMINIKA YA 7 YA PASAKA MWAKA A WA KANISA 2020


MAHUBIRI YA SHEREHE YA ASCENSION- KUPAA BWANA: DOMINIKA YA 7 YA PASAKA MWAKA A WA KANISA 2020

MASOMO
Somo I: Mdo. 1: 1 – 11.
Zaburi: 47
Somo II: Efe. 1: 17 – 23.
Somo III: Injili. Mt. 28: 16 – 20.
SALA: Ee Mungu Baba yetu, kwa nguvu na msaada wa Roho Mtakatifu, tunakuomba uwakinge wanafunzi wote ambao wanajiandaa kurudi shule katika kipindi hiki kiguma cha ungonjwa wa corona-Cov-19 uwazaidia pia walimu wote ili pamoja waepushe na ungonjwa huu ambao hadi sasa hauna tiba wala chanjo. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
UTANGULIZI
Wapendwa Taifa la Mungu, SHALOOM! Ndungu zangu, kwanzia Jumamosi Kuu ya Pasaka katika Misa ya usiku ambamo mama Kanisa alihadimisha sikukuu ya KUFUFUKA Bwana Wetu Yesu Kristu katika wafu hadi leo: Tunahesabu siku 40 ambao ki liturgia na ki theologia ni Hitimisho ya katika kazi ya ukombozi wa Mungu. Ndio maana kwa namna ya pekke, leo tunaadhimisha sherehe ya Kupaa Mbinguni Bwana Wetu Yesu Kristo. Sherehe hii huadhimishwa siku ya arobaini tangu kufufuka kwake Bwana wetu Yesu Kristo, yaani PASAKA. Hivi leo ni siku ya arobaini tangu Pasaka. Katika sherehe hii ya kupaa Bwana wetu Yesu Kristo mbinguni, tunasherehekea kule kuingia katika utukufu wa Mungu na kujichukulia cheo cha juu, juu kabisa katika utukufu huo. Na pia tunaimarishwa na kupewa pia matumaini ya kushiriki utukufu wa Mungu mwisho wa safari ya Maisha yetu hapa duniani.
UFAFANUZI
Wapendwa katika Kanuni ya imani(Credo) yetu tunakiri kama ifatavyo: Na sadiki kwa Mungu Baba Mwenyezi, Muumba wa Mbingu na dunia. Na kwa YESU KRISTO, mwanaye wa pekee, Bwana wetu, aliyetungwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akazaliwa na Bikira Maria, akateswa... akasulubiwa, akafa, akazikwa, akashuka kuzimuni siku ya tatu akafufuka katika wafu, akapaa mbinguni, amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi... wapendwa kila mara tunapo kiri imani yetu, tunasadiki kazi ya ukombozi ya UTATU MTAKATIFU katika safari ya wokovu wetu ambao Kristu yeye aliekuwa Mungu alikubali kwa hiari yake Mwenyewe kuchukua ubinadamu wetu kusudi katika umoja wa Baba na Roho Mtakatifu, mimi na wewe leo tusafishwe na kupewa neema tena ya kuishi katika utukufu.
Basi tunapo sherekeya kupaa kwa Bwana wetu Yesu Kristo tunasherekeya Umungu na Utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristu ambaye kwa kitendo cha kupaa huitimisha kazi ya ukombozi wetu. Kwanza tunaweza kujiuliza: ni Yesu peke yake ambaye katika safari ya mwanadamu alipaa kwenda mbinguni? Jibu ni ndio. Hakuna mtu mwingine katika Biblia alipaa kama Yesu Kristo na kwenda mbinguni. Kwa hiyo Henoko na nabi Elia hawakufa, lakini kwa mapenzi yake Mungu na kwa imani yao walipelekwa mbinguni. Tusome Waebrania (Hebrew) sura 11: 5-6: kwa imani Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu alimhamisha. Maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu. Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza... Tena mafundisho ya Kanisa leo hushuhudia kwamba Bikira Maria Mama wa Mungu, alipalizwa mbinguni mwili na Roho. 
Basi kitendo cha kupaa Bwana wetu Yesu Kristo utuonesha wazi tukio la pekee la kimungu ambao udhihirisha Mwisho na pia Mwanzo. Ni mwisho na hitimisho wa utume wa Yesu na vile vile tena ni mwanzo wa utume wa mitume ambao utaimarishwa zaidi ya kazi ya Roho Mtakatifu katika kazi ya kulijenga ao kisimika Kanisa na kutangaza ufalme wa Mungu kwa mataifa yote: huku wakitumaini na kusadiki uwepo wa Yesu kati yao kila siku ya maisha yao. Hayo tunayasoma katika injili ya Mathayo sura ya 28: 18-20: Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi. Na tazama, mimi nipo nanyi sikuzote, hata ukamilifu wa dahari. Kwa hiyo wapendwa, masomo yetu ya leo utuonesha wazi simulizi ya kupaa kwa Bwana wetu yetu Yesu Kristu na kuingia katika utukufu na kukaa katika upande wa kuume wa Mungu. 
Basi kibiblia kupaa maana yake nini? Kibiblia neno kupaa lina maana ya kuhama kwa mwili wa ufufuko wenye utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo, kutoka duniani na kuingia Mbinguni. Na maana nyingine ya kupaa ni hali ile ya kutukuzwa kwa Yesu ili apate kuwa mkuu na mmiliki wa vyote duniani na mbinguni. Hivyo basi Kupaa ni tendo au hali ya kurudia utukufu aliokuwa nao kabla hajachukua mwili kwa mama Maria yaani umwilisho. Yesu amepaa mbinguni kwanza, ili apokee tuzo kwa kazi nzuri alliyoifanya duniani,yaani kutukomboa sisi wanadamu  kutoka  utumwa wa dhambi na  mauti. Amekwenda kuvikwa taji ya  ushindi. Kristo ni mshindi ameshinda dhambi ambayo hupelekea kwenye  mauti.  Amepaa  kupewa taji aliloandaliwa baada ya ushindi huo mkubwa ambao kwa  kupitia huo tumepewa uwezo wa kwenda kwa  Baba.(rejea injili ya Marko sura16:19). 
Pili tunaweza kujiuliza ni lini Bwana wetu Yesu Kristo alipaa? Wapendwa, katika simulizi ya ufufuko wa Yesu, mwenjili Yohane utuanikia kama ifatafyo. Tusome injili ya Yoane sura ya 20: 16-18: Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia, kwa kiebrania, Raboni.(yaani mwalimu wangu) Yesu akamwambia, usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndungu zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu. Mariamu Magdelene akaenda, akawapasha wanafunzi habari ya kwamba, Nimemwona Bwana, na ya kwamba amemwambia hayo
Kwa maneno ya mwinjili Yohane, Bwana wetu Yesu Kristo, kwa kufufuka kwake,aliingia katika  utukufu yaani siku hiyo hiyo ya kufufuka kwake, Kristo alipaa mbinguni. Hivyo hakukuwa na wakati fulani uliopita kutoka ufufuko mpaka kupaa. Ndio maana mwinjili Luka katika injili yake sura 23: 39-43 udhihirisha kama ifatavyo: Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa pamoja na Yesu alimtukana,akisema, Je wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi. Lakini yule wa pili akamjibu, akamkemea, akisema, wewe hamwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo? Nayo ni haki kwetu sisi... kisha akasema, “Ee Yesu nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako,”  Yesu akamwambia, “Amin, nakuambia , leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.” 
Tunajifunza nini? Bwana wetu Yesu  Kristo alipaa mbinguni siku ya ufufuko wake lakini alijitokeza mara nyingi kwa wafuasi wake na mitume  kwa muda wa  siku arobaini, na leo ndio siku  arobaini tangu ufufuko wake,ili wapate  kuamini kuwa  amefufuka. Mitume walipaswa kuamini kwanza wao  habari za ufufuko ili  baadaye waweze kuwatangazia wengine  juu  ya ufufuko wa  Yesu, ambao ndio  ulikuwa msingi wa matumaini na imani yao pia ya imani na matumaini yangu na wewe utakae somo homelia hii. Mtume Paulo katika waraka wake wa kwanza kwa Wakorinto sura ya 15:14 usema hivi: Tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yetu ni bure. Pia aliendelea kuwatokea kwa lengo  la kuwaimarisha katika imani yao  dhaifu  kabla  hajawatumia  Roho Mtakatifu. Ndugu zangu katika Kristo, kwamaneno mengine siku  arobaini zinamaanisha muda wa kutosha  wa  maandalizi kumpokea Roho Mteakatifu siku ya Pentekoste.
Ndio maana katika somo la kwanza kutoka katika Metendo ya Mitume sura ya 1:11-11: Yesu anawahadia upeo wa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua, wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu... tena Yesu akawaambia mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yeruzalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Katika somo la kwanza tunaambiwa pia, watu wawili walionekana wamesimama karibu  nao wenye mavazi meupe, wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Atakuja jinsi hiyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni (Rejea. Mdo. 1: 11). Watu wa Galilaya ndio mimi na wewe leo. Ndio Kanisa. Kwa ubatizo wetu tunashirikishwa katika umungu na kuzaliwa tena katika famila takatifu na kupewa jikumu ya kumshuhudia na kumuhuburi Kristo kwa mataifa yote. Tena kwa sakramenti ya Kipaimara(confirmation) tunaimarishwa na Yesu na tunajaliwa vipaja vya Roho Mtakatifu ambao vinatufanya sisi kuwa askari hodari wa injili takatifu kwa hiyo kazi yetu sio kusimama tu na kutazama juu na kushangaashangaa, bali ni kutekeleza agizo la Yesu Katika injili yetu ya leo Mathayo sura 28:19: Basi enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. 
Maana yake Kanuni hii ya ubatizo ilivyoandikwa na mwinjili Mathayo, inaonesha kuwa yeyote anayebatizwa anashiriki maisha ya Mungu, ambaye ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Hivyo, kila mbatizwa lazima amwite Mungu Abba, yaani Baba. Kama ishara ya heshima na upendo na kujiweka chini ya ulinzi wa Mungu, kama watoto wake. Kristo anatuahidia atakuwa nasi mpaka utimilifu wa dahari. Hivyo basi, tujitahidi kufuata na kutenda kama alivyotupa agizo la kanuni ya ubatizo ili tuwe naye mbinguni, na kushiriki utukufu wa Mungu ambao utafikia utimilifu wake wote katika ujio wake wa pili Kristo atakapokuja kwa utukufu. 
Pia Yesu mwenyewe alisema, “Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama isingekuwa hivyo, ningalikwisha waambieni. Sasa nakwenda kuwatayarishieni nafasi.” (Rejea Yn. 14:2). Kwa hiyo basi, kupaa mbinguni hapa utuonesha njia ambao mimi na wewe leo tunatakiwa kupita kusudi sote tushirika utukufu wa Mungu siku ya mwisho wa maisha yetu. Kama vile Yesu anavyoingia katika utukufu wa Babake, ndivyo wafuasi wake na wale wote watakaotimiza mapenzi ya Baba yake ndivyo nao watakavyoushiriki utukufu huo. Na nafasi ya kushiriki utukufu huo iko wazi kwa kila mmoja wetu hapa: watoto, vijana, wazee-wake kwa waume, matajiri kwa maskini; kila mtu ana nafasi ya kushiriki utukufu huo ambao leo Bwana wetu Yesu Kristo tunamshangilia kwa kujinyakulia utukufu huo. Basi tufanye nini kusudi tushiriki ufalme wa mbinguni?
Tukisoma injili ya Mathayo sura ya 16: 24-25 tutasikia maneno ya Yesu ambao utuonesha masharti ya kumfuata: wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitikwe msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza, na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona. Basi wapendwa wangu, Yesu anataka kutuambia leo kuwa kila mmoja anajaliwa baraka na neema ya kushiriku umungu na utakatifu ila ajichukulie mwenyewe msalaba wake na kuupeleka kwa Yesu ambao kwa mti wa msalaba wake sisi tunakombolewa. Msalaba waako ni yupi? labda msalaba wako ni mume wako ambaye anashindwa kuteekeleza majikumu yake kama baba na kichwa cha familia, ni mke wako ambaye kwa tabia yake mbaya unashindwa kuona furaha na raha ya ndoa yako, ni maisha magumu ambao unakata tamaa na kupoteza matumaini, ni magonjwa kama corona-Cov-19 leo ambao leo tunaogopa na kuheshimu masharti(conditions) ya wahudumu wa afya kuliko hata amri ya Mungu, ni watoto wako ambao wamenaswa na furaha na anasa ya dunia hadi kupoteza utu wao, ni familia yako ambao kila siku uishi katika fujo, migogoro na ugonvi, ni tabia yako ya usharati, ya uchoyo, ya wivi na ukorofi, ya chuki na tamaa, labda ni uwongo na umbea wako... basi kila mmoja wetu anamsalaba wake basi Yesu anakumbia leo usiogope wala usihofu njoo kwangu na msalaba wako nitakupa faraja, uponyanji, furaha, ukombozi, utajiri wa mwili na roho na utashiriki utukufu  wa Mungu.


SHALOOM!
SHEMASI BIENVENU KABEYA NGUNGWA KUNGWA POULAIN LOQUACE, SDS







           






Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

MAHUBIRI YA SHEREHE YA PENTEKOSTE MWAKA A WAKANISA: ROHO MTAKATIFU HULITAKATIFUZA KANISA

MAHUBIRI YA SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU MWAKA A WA KANISA: ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, MUNGU AMBAYE YUPO, ALIYEKUWAKO, NA ATAKAYEKUJA

MAHUBIRI YA ADHIMISHO YA ALHAMISI KUU TAKATIFU : EKARISTI NI ALAMA YA UPENDO NA UMOJA