MAHUBIRI YA DOMINIKA YA 12 YA MWAKA A WA KANISA KIPINDI CHA KAWAIDA
MAHUBIRI YA DOMINIKA YA 12 YA MWAKA A WA
KANISA KIPINDI CHA KAWAIDA
MASOMO
SOMO
I:
Yer.20: 10-13
SOMO
II:
Rom.5: 12-15
INJILI: Mt.10: 26-33
SALA: Ee
Mungu Baba yetu, tunakusifu na tunakushukuru kwa sababu ya ulinzi wako kadiri
ya juma nzima. Tunakuja mbele yako kuomba tena msaada wa wiki hii ili kwa nguvu
ya Mungu Roho Mtakatifu tuepushwe na ungonjwa wa Corona pia uwasaidie wote
ambao hadi sasa wanapambana na ugonjwa huu na uwarudishiye afya wale wote
waliopata ugonjwa huo. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amen.
UTANGULIZI
Taifa
la Mungu SHALOOM, TUMSIFU YESU KRISTU.
Wapendwa baada ya Sherehe ya Pasaka, tulisherekeya sherehe ya Pentecost, Utatu
Mtakatifu, Mwili na Damu Takatifu ya Bwana wetu Yesu Kristu na mwisho kabisa tulisherekeya
sherehe ya Moyo Mtakatifu wa Yesu(sherehe hii ya Moyo Mtakatifu wa Yesu inaweza
pia kuadimishwa Jumapili kwa wale ambao viongozi yaani maskofu waliamua hiadimishwe
Jumapili lakini kwetu sisi tulisherekeya sherehe hii ijuma (Friday or Vendredi)
ya wiki hii. sherehe zote izi inne utupa nafasi ya kutafakari kwa kina Upendo na Umoja wa Mungu katika kazi nzima ya uumbaji na ukombozi wetu pia utufunza kusudi tudumishe upendo na umoja huu kati ya Mungu sisi na pia kati yetu sisi kwa sisi kama wanadamu. Basi leo tunaendelea na Dominika ya 12 ya Mwaka A wa
Kanisa katika kipindi cha kawaida. Wapendwa masomo yetu ya leo inatualika kuwa
na nadhamira kama ifatavyo: tusiwaogope wauao mwili
lakini ni afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika
jehanum(enfer). Tumuombe Mungu kwa msaada wa Roho Mtakatifu tubaki
imara katika Imani yetu.
UFAFANUZI
Wapendwa
mara nyingi katika Maisha yetu tunakutana na changamoto nyingi ambao inatufanya tukate tamaa apa na pale: kuna baadhi kati yetu wanakutana labda na Maisha
magumu, wengine ni ndoa ambao inasumbua mume ao mke aeleweki, wengine ni Watoto
ambao wanashindwa kuishi kadiri ya malezi ya wazazi na kumcha Mungu tena
wengine ni shule, mangonjwa kama corona na menginevyo, wengine kutokupata mume ao mtoto… lakini tukiangalia
kiuwalisia ya Maisha yetu, changamoto ni sehemu ya Maisha ya mwanadamu, kupambana na kujaribu kuvumilia na kutatua hizi shida ni mwanzo wa mafanyikio
yetu asa Zaidi sisi tunao weka matumaini yetu kwa Yesu Kristu ambaye utusimamia
Pamoja na Roho Mtakatifu katika Maisha yetu. Ndio maana katika somo la kwanza
nabii Yeremia anakutana na changamoto ambao inahatarisha hata maisha yake, nabii
anakata tamaa na kulia. Wapendwa
tukisoma Yeremia 1: 1-9: tutasikia simulizi ya wito wa nabii huu: Mungu
katika neno lake lilimjia Yeremia na Kusema: kabla
sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa,
nimekuweka kuwa nabii wa mataifa….
Lakini
Yeremia akamwambia Bwana, tazama siwezi kusema, maana mimi ni mtoto lakini
Bwana akamwambia: Usiseme, Mimi ni mtoto maana
utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno
nitakalokuamuru kwake, …. Usiogope kwa
sababu ya hao, maana mimi nipo Pamoja nawe nikuokoe. Lakini Yeremia
baada ya kukutana na changamoto: yakutokukubaliwa na wana wa yuda, wanamkataa
na wanatafuta kumuua nabii anaogopa na kulia hakishikwa na hofu. Yeremia aliishi
katika wakati mgumu saana ambao waisraali walikutana na vita, hekalu
likabomolewa hadi kupelekwa utumwani tena wa Babiloni… kwa izi shida zote ziliwafanya
waisraeli kukataa maneno ya Yeremia yaani maneno ya Mungu na kutaka kumuua.
Wapendwa nilazima kutambua kwamba kazi ya Mungu pia inachangamoto nyingi:
unaweza kusemwa na wenzio kwamba huyu hana kazi ndio maana yupo kanisani, ao ni
umaskini ndio maana amejifanya kuwa mkristu, hana wito huyu ni njaa tu ao unapo
shuhudia ukweli leo katika ulimwengu wetu huu wa kisasa, unaweza kuonekana kama
kero mbele ya watu hadi kutengwa nao… lakini usikate tamaa bali tambua kuwa
Bwana Mungu yu nawe kila upande, Yesu anakutetea kila sehemu usichoke wala
kubadilisha kahuli lako lakini baki katika Imani yako.
Ndio
maana katika Injili Yesu anawapa wanafunzi wake tahadhari ya kuwa wasiogope
nguvu za dunia wala kushindana na furaha ya dunia hii lakini ni lazima kumwogopa
Mungu ambaye anaweza kuangamiza mwili pia na roho: Yesu alitaka kuwaambia
wanafunzi wake na kutuambia mimi na wewe leo kwamba: kwanza Mungu awe chaguo letu kabla ya vitu vingine viote:
Mungu awezi kulinganishwa na wafalme wa kidunia. Injili hii ya Mathayo inatuonesha
wazi namna gani wakristu wa kwanza walikuna na changamoto ya nguvu ya Mfalme wa
Roma ambaye alitawala wakati ule na kunyanyasa watu ili wamwabudu kama Mungu:
wakristu wengi walichinjwa, kupigwa na kunyanganywa vitu vyo licha tu walikataa
kumwabudu Mfalme. Basi mimi na wewe leo tujiulize Mfalme
wangu ni nani? Labda ni feza ambao unatafuta kila siku, usiku na mchana
hadi kutumia njia isiofaa kusudi upate hela hadi kuhisau siku takatifu ya
Mungu, labda wewe Mfalme wako ni tabia ya uzinzi, ya wizi na unyanyazaji, labda
ni ukorofi, labda ni uwongo na umbeya ambao usababisha watu waishi katika vita
na matengano…
Yesu
anakwambia leo wala usikate tamaa na kujilaumu lakini piga hatua moja mbele na
kumfuata kusudi upate kupona. Tena Yesu anasema kwamba: kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele ya
Baba aliye mbinguni. Bali, kila mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami
nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni. Kwa hiyo Yesu ndiye
Mwamuzi na Msaada wetu katika furaha ao katika shida tumuelekeye kila siku ya Maisha
yetu tambua bila Yesu katika Maisha yako, ndoa yako, masomo yako, kazi yako ni
bure lakini ukimweka mbele kuliko kila kitu atakwambia: usiogope kwa maana kwake Yeye hakuna neno lililositirika,
ambalo halitafunuliwa, wala lililofichwa, ambalo halitajulikana.
Basi tikifanya mapenzi ya Mungu tutafananishwa na Yesu ambaye alishinda mauti
ya kifo na kutukomboa sisi katika utumwa wa dhambi bali kinyume chake yaani
tukizingatia mapenzi yetu kuliko Mungu, tutafananishwa na Adamu ambaye kwa
kutomtii Mungu alitenda dhambi na kuharibisha ulimwengu kwa kifo. Basi tuwe
waaminifu katika Imani yetu ya Kumfuata Mungu.
SHALOOM
SHEMASI BIENVENU KABEYA KUNGWA NGUNGWA POULAIN LOQUACE SDS
Commentaires